Nahisi simpendi mke wangu

Nahisi simpendi mke wangu

Pole sana Goboshi mmeshaoana au bado? Je ana elimu gani? Je wazazi wake unawajua? hapa nitakushauri uende kwa watu wazima na ujiulize nini unataka? Ufanye maombi, maana kuna mtoto anahusika usikurupuke. At the end wewe ndio unajua hali halisi, Pole sana sana.
 
Last edited by a moderator:
MO11 come this way mchepuko

nimekuja deer

back to the topic

Ulikosea siku ya kwanza kabisa kama mtu hataki kutambulishwa mbele ya kanisa kuna mawili
1) Ana madudu yake ambayo labda baadhi ya watu mule kanisani wanayajua
2) Ana tabia mbaya wengi wa watu wabaya (sio sura) huwa hawapendi macho ya watu ndio maana kila jambo baya likutokealo atajihusisha yeye hivyo hakuwa mke mwema tangu siku ya kwanza.

Ushauri watoto watatu ni wengi kumkabidhi mama wa kambo awalee sio wote ila wengi wao ni tabu
Hope huyo mkeo ni mtu wa pwani
 
Kuna kitu atakua anacho mkeo kwa muda mrefu ila haujamtengenezea mazingira ya kufunguka na kuutua mzigo alio nao moyoni,
 
Nilijaribu kufanya utafiti na nikagundua kuwa kuna mke wa kaka yangu ambaye amemfundisha chuki dhidi ya mama yangu na dada zangu ila zaidi naona ameenda mbali na kunichukia mimi pia. Hali iko hivi,

Baba yangu alikuwa na wake wawili ambapo mama yangu ni bimdogo. Mama ytu mkubwa alifariki mwaka 83 na kubaki na mama yangu ambaye alitulea wote kama ametuzaa. Sasa kuna maneno mengi yaliyozuka baada ya watoto kuanza kujitegemea na hapo familia ikagawanyika kwa matashi ya wachache.

Mwanzo tulish kwa upendo na hata watu wasiofahmu ilikuwa ngumu kutuofutisha kwa jinsi tulivyokuwa tukihudmiwa. Baada mke wangu alijikuta akiingia kwenye darasa la shemeji angu mkubwa ambapo amepewa sumu nyingi mpaka za unichukia mimi. Amewahi kuambiwa kuwa mimi sikufaulu darasa la saba isipokuwa ndugu yangu mwingine ambapo kwa kuwa mama yake alifariki akazuiliwa kwenda shule badala yake niepelekwa mimi. Kidogo nitoe machozi lakini nikamulza kama anajua ukweli juu ya hilo.

Kimsngi badala ya kuwa mtu wa msaada kwangu naona ameungana na maadui zangu kutaka kuukatisha uhai wangu haraka.
 
Kaka pole sana mimi najiuliza kitu gani kinachompa jeuri huyo mwanamke kiasi hicho?

Kwasababu unatafuta pesa una-risk maisha yako mabarabarani hii yote kutafuta kwa aajili ya familia na yeye mkeo akiwa mmoja wa mtu anayeunda hiyo familia kama hujamuoa ndoa ya kanisani mwache asiwe mwiba kwenye maisha yako.

Au kama vipi mpumzishe kwanza aende kwao akakae huko kama miezi sita hivi aone joto ya jiwe labda ataona umuhimu wako.
 
Kaka Goboshi au mkeo anaimani za kishirikina maana hata kama hajaenda shule hana elimu wanawake wangapi hawana elimu lakini wana adabu na utii kwa wanaume zao.
 
Last edited by a moderator:
Sasa unapaswa uanzie hapa,usifanye mambo kwa hasira
Nilijaribu kufanya utafiti na nikagundua kuwa kuna mke wa kaka yangu ambaye amemfundisha chuki dhidi ya mama yangu na dada zangu ila zaidi naona ameenda mbali na kunichukia mimi pia
 
Kuna mengi yanachangia hapo ila kwa ufupi
Pengine ni
Elimu( afu mnasema ooh la saba na f 4 ndo wakuoa on a sasa)
Pengine ni asili yake ya ukorofi mwanzo hakukuonesha
Pengine ushawishi kashikwa akili na anao wajua
Pengine hakupendi kuna kitu alifata kwako keshakipata haoni tena umuhimu wako
Pengine pengine..

Wanasema kosea kujenga lakini si kuoa wala kuolewa

Ushakosea toka mwanzo
Angalia utaratibu was maisha yako na wanao
As long as hamjafunga
Ndoa nenda Naye taratibu MPE anachotaka anza upya
Yanini MTU mmekutana ukubwani akufanye uishi kama mtumwa ? Hiyo siyo definition ya ndoa
Sepa atakuua huyo.
 
Duh kuna watu ni so destructive pole sana kaka angu kwa magumu unayopitia. Divorce haitasaidia hususani kama unawapenda watoto wako. Jitoe kafara tu.

Huyo mwanamke mpotezee najua ni ngumu ila inapobidi inabidi ui force akili yako ikubali uhalisia jali watoto wako hebu wafanye wanao wawe faraja na furaha yako.

Usimjibu vibaya fanya vile anavyotaka trust me kama ana akili timamu ipo siku atakupigia magoti.

Kuna bwana mmoja alikuwa akipewa habari za maovu ya mkewe na kuna siku alipishana na mkewe njiani akiwa na jamaa kabisa wameshikana ki mahaba. Jamaa alimpa hi poa. Mwanamke alipatwa na hofu jioni wakakutana home jamaa haku react wala nini wakalala kawaida asubuhi jamaa kaacha hela ya matumizi kamsalimia mke wake huyo kazini. Ikawa kawaida kama hamna tatizo yule jamaa hakumuweka mke wake hata wajadili kitu. Mwisho mwanamke alijishtukia hadi akakimbia maake alitegemea jamaa ange react lakini wapi alihisi jamaa anaweza kumuua kumbe jamaa alisham delete zamanii.

We mdelete tu huyo atajishtukia mwenyewe
 
Nilijaribu kumpeleka kwao lakini hata mwezi haukuisha akarudi na fujo zake. Nikimsihi kubadilika yeye anasisitiza juu ya mali. Kwa hiyo kutafuta kwangu inakuwa mwiba kwangu.

Mali zangu zinataka kunitoa roho mwenyewe kwa kujaribu kuvumilia ili niokoe mali zangu ninazopata kwa shida. Nimejenga nyumba nzuri ila nalala kama mara sita kwa mwezi, muda wote niko field kutafuta, wanaojivunia nilicholeta hawataki kuuona mzigo niliobeba. Na kwa tabia yangu kila nikija lazima nibebe kifurushi lakini kuna muda huwa sipokelewi.

Kuna kipindi nilikuja Dar na samaki kutoka Mwanza nikatamani zingeibiwa maana baada ya kushuka kwenye taxi nilibeba mizigo yangu watu wamesimama kwenye nyumba wananiangalia bila hata kuja kunipokea. Niliwaza sana nikasema kwa sauti nimepotea nyumba???
 
Duh kuna watu ni so destructive pole sana kaka angu kwa magumu unayopitia. Divorce haitasaidia hususani kama unawapenda watoto wako. Jitoe kafara tu.

Huyo mwanamke mpotezee najua ni ngumu ila inapobidi inabidi ui force akili yako ikubali uhalisia jali watoto wako hebu wafanye wanao wawe faraja na furaha yako.
Kumfukuzia mbali au kumpa muda aondoke mwenyewe mbona ni kujichelewesha kuanza upya. Ukigundua mtu humtaki mtimue tu asogee mbali na mambo yako kuliko kukaa na mtu ambaye huna matumizi naye leo wala kesho!!!!!

Na hii misimamo tukiiweza adabu itarudi miongoni mwetu we mtu anakuambia wazi usijenge au ajali nimekuombea mimi bado tu hata "mapumziko" humpi????!!!
 
Nilijaribu kumpeleka kwao lakini hata mwezi haukuisha akarudi na fujo zake. Nikimsihi kubadilika yeye anasisitiza juu ya mali. Kwa hiyo kutafuta kwangu inakuwa mwiba kwangu.

Mali zangu zinataka kunitoa roho mwenyewe kwa kujaribu kuvumilia ili niokoe mali zangu ninazopata kwa shida. Nimejenga nyumba nzuri ila nalala kama mara sita kwa mwezi, muda wote niko field kutafuta, wanaojivunia nilicholeta hawataki kuuona mzigo niliobeba. Na kwa tabia yangu kila nikija lazima nibebe kifurushi lakini kuna muda huwa sipokelewi.

Kuna kipindi nilikuja Dar na samaki kutoka Mwanza nikatamani zingeibiwa maana baada ya kushuka kwenye taxi nilibeba mizigo yangu watu wamesimama kwenye nyumba wananiangalia bila hata kuja kunipokea. Niliwaza sana nikasema kwa sauti nimepotea nyumba???
Mkuu tafuta suluhu mapema maana kuongea peke yako ni mwanzo wa kuchanganikiwa, tatizo limeanzia katika familia yako, anga kuweka sawa huko then utamalizia na kwa mkeo
 
Sasa unapaswa uanzie hapa,usifanye mambo kwa hasira

Hapo nimeshafanya jitihada zote lakini naona kichwa hakitaki kubadilika. Nimekaa nae mara nyingi kumpa ukweli lakini naona anasikia ya maadui kuliko ya kwangu.

Na pia hakuna jema analoliona kwenye maisha yake isipokuwa mabaya tu, na mpinzani kwa kila ninachoamua ama kufanya kiasi kwamba hata nyumba ya pili niliamua kujenga kwa nguvu kuanzia kununua kiwanja mpaka ujenzi. Ilipoisha ndo anapigia simu ndgu zake kuwajulisha amajenga nyumba.

Mtu hata kwenda kusimama na mafundi wasiibe cement haendi, kila kitu nafanya mwenyewe na kiwa safari natumia marafiki kusimamia ujenzi
 
Nilijaribu kumpeleka kwao lakini hata mwezi haukuisha akarudi na fujo zake. Nikimsihi kubadilika yeye anasisitiza juu ya mali. Kwa hiyo kutafuta kwangu inakuwa mwiba kwangu.

Mali zangu zinataka kunitoa roho mwenyewe kwa kujaribu kuvumilia ili niokoe mali zangu ninazopata kwa shida. Nimejenga nyumba nzuri ila nalala kama mara sita kwa mwezi, muda wote niko field kutafuta, wanaojivunia nilicholeta hawataki kuuona mzigo niliobeba. Na kwa tabia yangu kila nikija lazima nibebe kifurushi lakini kuna muda huwa sipokelewi.

Kuna kipindi nilikuja Dar na samaki kutoka Mwanza nikatamani zingeibiwa maana baada ya kushuka kwenye taxi nilibeba mizigo yangu watu wamesimama kwenye nyumba wananiangalia bila hata kuja kunipokea. Niliwaza sana nikasema kwa sauti nimepotea nyumba???
Mkuu pole ila una mawili ya kufanya, moja fuata dini yako na wenye "busara" na uwe tayari hata kuishi maisha ya kufurahisha wengine huku we ukiumia au kaa kama mtoto wa kiume consult nafsi yako thoroughly then amua once and for all
 
Mimi ni mpenzi wa kusoma vitabu hasahasa vya saikolojia, nimejaribu mbinu mbalimbali zinazoelekeza kumfanya mtu akupende na kuwe na amani ndani lakini wapi.

Kwa mfano kuna kipindi nawapeleka kanisani na baada ya hapo nawaambia hakuna kupika leo tunaenda kula hotel. Tukifika huko wengine wanafurahi na watoto wanafurahia ma-burger na vingine lakini yeye naanza kufoka kuwa nachezea hela na vyakula vibaya.

Yaani ni mtu wa tofauti. Siku moja nikasema leo hatulli nyumban tunaenda hotel, nikachukua chumba hotel (Kunduchi) nikijua tutauwa tunahuisha mapenzi lakini nichopata natamani kulia. Unamlazimisha mtu ku-do kama umembaka, hakuna kushikana shikna wala nini.

Maisha yananitesa mimi, inaniuma kwani kuna warembo wanakuwa wanaonyesha interest
 
Mkuu pole sana,kama uyasemayo ni kweli me naona utakua umekosea heading badala ya kusema "nahisi simpendi mke wangu" ungesema "nahisi naishi na pepo"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom