Ndugu hayo ni majira tu unapitia,Kila kitu kina majira yake kama wakristu tunavyoelezwa katika MHUBIRI 3:1-8, kuwa Kuna wakati wa kucheka na wakati wa kulia
Changamoto ya Sasa tunawakosa akina Yusufu kama wa kwenye Bible wa kutufunulia miaka ya njaa na miaka ya Shibe Ili tufanye Maandalizi stahiki kama alivyofanya Pharaoh .
Ushauri wangu ,usiende Kwa waganga watakuvuruga zaidi ni kumuomba Mungu majira ni mzunguko mambo yatakaa sawa.
Hata Mie niliwahi kupitia kipindi kigumu sana mamba kazini na mtaani yakaparaganyika mpaka nikahisi nimerogwa lakn baada ya kupata ushauri wa jinsi majira yanavofanya kazi nikaona Kuna vitu nilikuwa nahangaika navyo wakati ambao sio sahihi na mambo mengine wakati ulipofika yakanyooka bila kutumia ndumba yoyote na sasa nipo sawa