Nafikiri mmeona tofauti ya Messi na Ronaldo

Nafikiri mmeona tofauti ya Messi na Ronaldo

Mbona hata Messi ana umri mkubwa miaka 38 mkuu ni midogo? Lakini anafanya vitu vyote assist na kufunga kitu ambacho usichojua Messi ana natural talent ambayo inamfanya afanye vyote kwa pamoja hata akifika huo umri maana tofauti yao ni miaka miwili tu. Na Mimi sijasema Kama Ronaldo ni mchezaji mbaya ni mchezaji Bora naheshimu Hilo kutokana na mambo alivyofanya kwenye mpira ikiwemo kufunga 950+ goal lakini ukija kumfananisha na Messi ndipo watu wanapoharibu kwasababu Messi ni full package ya mchezaji ni sawa na Leo hii umfananishe Ronaldo De Lima na Hallaand ni kuukosea mpira heshima ingawa Hallaand ana goal nyingi lakini Ronaldo De Lima ni striker mwenye package ya kipekee hakupi magoal pekee sanaa yake ya mpira ndio inayomtofautisha na ma strikers wengine hiyo ndio maana kuitwa bora
Naona kama wanaomfananisha na Messi ni wanaomsifia Messi. Embu fanya utafiti, huenda sipo sahihi.

Naona kama wengi wanaomsifia Messi wanamtaja Ronaldo, ila wanaomtaja Ronaldo hawamtaji sana Messi. Am i wrong?
 
Haaland damu bado mbichi, mtu kama Ronaldo ana zaidi ya miaka 40, hivi unategemea kweli akasimame na vijana kushindana nao kasi? Sio kweli.

Kuna muda nalazimika kuamini kuwa Ronaldo anapata namba pale Portugal kutokana na nguvu yake kifedha kumshawishi kocha. Hata Neymar unaona tu huyu jamaa kuna sehemu kamwaga ela ili tu aitwe timu ya Taifa.
Kuitwa ni sahihi ila sijaelewa kwanini anacheza FT, kwa umri wake angekuwa na impact zaidi kwenye hamasa na kucheza kuanzia dk ya 70, esp pale ambapo timu haina cha kupoteza tena, either imefungwa inahitaji kushambulia au imeshinda goli ambazo haziwezi kurudi. Awe anatupiwa tu kwenye Box maana jamaa kufunga anajua.
 
Naona kama wanaomfananisha na Messi ni wanaomsifia Messi. Embu fanya utafiti, huenda sipo sahihi.

Naona kama wengi wanaomsifia Messi wanamtaja Ronaldo, ila wanaomtaja Ronaldo hawamtaji sana Messi. Am i wrong?
Sio kweli wanaomsifia Ronaldo lazima wamponde Messi hivyo hivyo wanaomsifia Messi
 
Mbona hata Messi ana umri mkubwa miaka 38 mkuu ni midogo? Lakini anafanya vitu vyote assist na kufunga kitu ambacho usichojua Messi ana natural talent ambayo inamfanya afanye vyote kwa pamoja hata akifika huo umri maana tofauti yao ni miaka miwili tu. Na Mimi sijasema Kama Ronaldo ni mchezaji mbaya ni mchezaji Bora naheshimu Hilo kutokana na mambo alivyofanya kwenye mpira ikiwemo kufunga 950+ goal lakini ukija kumfananisha na Messi ndipo watu wanapoharibu kwasababu Messi ni full package ya mchezaji ni sawa na Leo hii umfananishe Ronaldo De Lima na Hallaand ni kuukosea mpira heshima ingawa Hallaand ana goal nyingi lakini Ronaldo De Lima ni striker mwenye package ya kipekee hakupi magoal pekee sanaa yake ya mpira ndio inayomtofautisha na ma strikers wengine hiyo ndio maana kuitwa bora
Messi ni mchezaji mzuri ila yupo chini ya NEC
 
Kwakweli mimi sio mshabiki wa Messi wala Ronaldo,ila kwenye hili kombe la dunia ukiangalia hawa wawili uchezaji wa Ronaldo ni wa kipuuzi sana,anachosubiria ni kutengenezewa mipira ili afunge,wakati ukiangalia kwa mechi ya jana Messi anapambana kila kona,kutafuta mipira ili afunge na hata kuwatengenezea wenzake.Ukienda mbali zaidi ni bora hata kuwa na mtu kama Haaland kuliko kuwa na Ronaldo...
Kazi na umri. Miaka 41 na kudrible wapi na wapi?. Halafu angalau angekuwa mfupi. Laiti angejua angekuwa supersub ya dakika za jioniiii,apishe vijana Kwanza kwa manufaa ya timu!
 
Kwakweli mimi sio mshabiki wa Messi wala Ronaldo,ila kwenye hili kombe la dunia ukiangalia hawa wawili uchezaji wa Ronaldo ni wa kipuuzi sana,anachosubiria ni kutengenezewa mipira ili afunge,wakati ukiangalia kwa mechi ya jana Messi anapambana kila kona,kutafuta mipira ili afunge na hata kuwatengenezea wenzake.Ukienda mbali zaidi ni bora hata kuwa na mtu kama Haaland kuliko kuwa na Ronaldo...
Kazi na umri. Miaka 41 na kudrible wapi na wapi?. Halafu angalau angekuwa mfupi. Laiti angejua angekuwa supersub ya dakika za jioniiii,apishe vijana Kwanza kwa manufaa ya timu!
 
Najivunia sana kuona era ya Messi bila kuhadithiwa kwa kweli kumpata mchezaji aina ya Messi itachukua muda sana ila ni rahisi kumpata Ronaldo.

Mara ya kwanza kumshuhudia Messi kwa macho yangu ilikuwa mechi za Olimpiki ya Beijing, wakati huo nilikuwa naishi kwa macho madogo...

Halafu Messi alikuwa ni kijana mdogo sana bado, ndio kwanza alikuwa ameanza kuchipukia kwenye timu yake ya taifa...

Ni burudani sana ukiwa jukwaani unamtazama "little magician", kwa muda mrefu sana sikuwa nimeona mchezaji anayetumia mashoto mwenye mbwembwe na kachumbari kachumbari kama za Edibily Lunyamila...
 
Kwakweli mimi sio mshabiki wa Messi wala Ronaldo,ila kwenye hili kombe la dunia ukiangalia hawa wawili uchezaji wa Ronaldo ni wa kipuuzi sana,anachosubiria ni kutengenezewa mipira ili afunge,wakati ukiangalia kwa mechi ya jana Messi anapambana kila kona,kutafuta mipira ili afunge na hata kuwatengenezea wenzake.Ukienda mbali zaidi ni bora hata kuwa na mtu kama Haaland kuliko kuwa na Ronaldo...

CR7 zama zake zimeisha kwa sababu ya aina ya uchezajo wake hauwezi tena kuendana na umri...

CR7 alikuwa ni mtu mwenye kutegemea nguvu na kasi zaidi, kitu ambacho kwa sasa mwili lazima ukatae kutokana na umri...

Messi yeye ni tofauti, utegemezi wake upo kwenye akili ya kusoma mchezo, kasi inapobidi na kuunganisha timu hivyo bado ana uwezo wa kucheza kwa kuhifadhi energy hata umri wake ambavyo umekuwa mkubwa...
 
CR7 zama zake zimeisha kwa sababu ya aina ya uchezajo wake hauwezi tena kuendana na umri...

CR7 alikuwa ni mtu mwenye kutegemea nguvu na kasi zaidi, kitu ambacho kwa sasa mwili lazima ukatae kutokana na umri...

Messi yeye ni tofauti, utegemezi wake upo kwenye akili ya kusoma mchezo, kasi inapobidi na kuunganisha timu hivyo bado ana uwezo wa kucheza kwa kuhifadhi energy hata umri wake ambavyo umekuwa mkubwa...
Cr7 unamkumbuka akiwa manjesta?
 
Cr7 unamkumbuka akiwa manjesta?

Naam,

Akiwa Man U alianza kwa kupenda uchezaji wa chenga zisizo na manufaa, kiasi cha kumkasirisha Ruud Van na hahata babu Ferg...

Baadaye akafundwa na kubadili uchezaji kuwa wa kasi kwenda mbele, na pia kufunga na hii transition ndio ikaanza kumfanya CR7 awe tishio, the rest is history...

Angeendelea kuwa mchezaji wa "anakwendaaa, anakwenda na mpira", angeishia kuwa kama Robinho au Denilson wa Brazil...
 
Ukitoa FIFA Messi ni kama Samatta
Wewe umeamua kujinyima raha ya kuangalia mpira mzuri wa Messi watu kama Messi huwa hawatokei mara kwa mara ni vizuri huu muda uutumie vizuri ili upate cha kuwadithia vizazi vijao kama ambavyo tulivyokuwa una hadithiwa kuhusu Pele na Diego Maradona
 
Wewe umeamua kujinyima raha ya kuangalia mpira mzuri wa Messi watu kama Messi huwa hawatokei mara kwa mara ni vizuri huu muda uutumie vizuri ili upate cha kuwadithia vizazi vijao kama ambavyo tulivyokuwa una hadithiwa kuhusu Pele na Diego Maradona
Mpira mzuri nliuona kwa Ronadho, Kaka, Zidane,Okocha Juninho hawakuwa sponsored by FIFA
 
Binafsi naona kabisa
Messi ni natural talent
Ronaldo ni hard worker

Messi ana mia tisa na ushee...
Ronaldo ana mia tisa na ushee...

Messi ana ballon de ore 8
Ronaldo ana ballon de ore 5

Messi ana
World cup 2
Copa America 2
Finallisima 1

Ronaldo
World cup 0
Uefa Euro 1, goli limepatikana bila uwepo wake na kuchukua kikombe😄
Uefa nations league 😄


N.k
N.k
N.k
N.k
N.k
N.k
 
Back
Top Bottom