Nadharia hii nani kaipandikiza kwenye jamii?

ilaz

Senior Member
Jul 13, 2017
100
61
Mwezi uliopita nilienda kumtembelea bibi yangu huko kilolo ndani ndani, tangia nchi ipate uhuru hadi leo maji ya bomba wanayasikia kwenye redio tu, umeme ndio kabisa anasa. Bibi bado anatumia maji ya mto. Nikamuuliza bibi kura ulimpigia nani kwenye uchaguzi? Akajibu nilichagua CCM. Nikamuuliza kwanini? Akanijibu ukishinda upinzani nchi itaingia kwenye vita. Nilicheka sana, nikampa zawadi ya solar niliyompelekea nikaondoka zangu.


Jibu linalofanana na hilo nililipata huko morogoro, matombo nilipokuwa kwenye shughuli zangu za kikazi. Mama mmoja mkulima wa mpunga aliniambia kuwa upinzani ukishinda nchi itachafuka. Huyu mama bado alikuwa anatumia jembe la mkono na hali ya maisha pale kijijini ni ngumu wafanyabiashara wanakuja kipindi cha mavuno na kubadilisha mitumba kwa mpunga.

Jibu kama hilo tena nililipata mtaani kwangu kwa motto mmoja wa miaka 13 anaeitwa Nzeimana. Jina la huyu motto lilinifanya niwe mdadisi kidogo kujua asili yake maana haya sio majina ya wazawa wa Tanzania. nilimuuliza nzeimana kwa utaalamu bila yeye kujua akaniambia kuwa baba na mama yake walikufa huko Rwanda na yeye kuchukuliwa na mjomba wake ambae ndio anamlea hadi sasa. nikamuuliza nzeimana ukiwa mkubwa utakuwa chama gani ? Akajibu CCM. Nikammuliza kwann? Akajibu mjomba kaniambia CCM ikishindwa wageni wote tutarudishwa kwenye chi zetu.
Jibu kama hilo nilipewa na dada mmoja mwenye asili ya msumbiji lakini anajiita mmakonde.

Baada ya hapo nikajiuliza swali kuwa ni nani anaisambaza nadharia hii ya upinzani ukishinda nchi itaingia kwenye machafuko?

'' EDUCATION IS ABILITY NOT NOTES''
 
Ni mfumo mbovu wa elimu kwasababu hiyo ni mentality ilopandikizwa tokea enzi
Watu wa vijijini wanaamini hivyo
 
Ule mpango mkakati wa UPE kwenye elimu ndo karata ya CCM..
Schools, schools, schools everywhere..! Free education free of education..!!
Na sasa wameidhinisha hakuna mtoto kufeli wala kurudia darasa...!!
 
CCM naikubali sana katika kitengocha propaganda na huu umekuwa ni mfumo wa muda mrefu wa vyama tawala vilivyokaa madarakani muda mrefu, chama kikishakaa madarakani muda mrefu kinaamua kutumia aina yoyote ya propaganda ili kukiweka madarakani, hata ikibidi kutumia hila na ushirikina, kinaamini kuwa chenyewe ndicho chenye haki ya kutawala na kina uchungu na nchi kwamaana ndicho kilicho leta uhuru.

Na mara nyingi inakuwa wale viongozi wa awali walioshiriki katika kupigania uhuru walikuwa na msimamo wa kati lakini warithi wao ambao wakati wa kupigania uhuru walikuwa bado wanachezea makamasi ndo wanajifanya wanauchungu kupitiliza.
1445436697096-jpg.301273
112380_900.jpg
 
CCM naikubali sana katika kitengocha propaganda na huu umekuwa ni mfumo wa muda mrefu wa vyama tawala vilivyokaa madarakani muda mrefu, chama kikishakaa madarakani muda mrefu kinaamua kutumia aina yoyote ya propaganda ili kukiweka madarakani, hata ikibidi kutumia hila na ushirikina, kinaamini kuwa chenyewe ndicho chenye haki ya kutawala na kina uchungu na nchi kwamaana ndicho kilicho leta uhuru.

Na mara nyingi inakuwa wale viongozi wa awali walioshiriki katika kupigania uhuru walikuwa na msimamo wa kati lakini warithi wao ambao wakati wa kupigania uhuru walikuwa bado wanachezea makamasi ndo wanajifanya wanauchungu kupitiliza.
1445436697096-jpg.301273

umasikini kitu kibaya sana
 
Mwezi uliopita nilienda kumtembelea bibi yangu huko kilolo ndani ndani, tangia nchi ipate uhuru hadi leo maji ya bomba wanayasikia kwenye redio tu, umeme ndio kabisa anasa. Bibi bado anatumia maji ya mto. Nikamuuliza bibi kura ulimpigia nani kwenye uchaguzi? Akajibu nilichagua CCM. Nikamuuliza kwanini? Akanijibu ukishinda upinzani nchi itaingia kwenye vita. Nilicheka sana, nikampa zawadi ya solar niliyompelekea nikaondoka zangu.


Jibu linalofanana na hilo nililipata huko morogoro, matombo nilipokuwa kwenye shughuli zangu za kikazi. Mama mmoja mkulima wa mpunga aliniambia kuwa upinzani ukishinda nchi itachafuka. Huyu mama bado alikuwa anatumia jembe la mkono na hali ya maisha pale kijijini ni ngumu wafanyabiashara wanakuja kipindi cha mavuno na kubadilisha mitumba kwa mpunga.

Jibu kama hilo tena nililipata mtaani kwangu kwa motto mmoja wa miaka 13 anaeitwa Nzeimana. Jina la huyu motto lilinifanya niwe mdadisi kidogo kujua asili yake maana haya sio majina ya wazawa wa Tanzania. nilimuuliza nzeimana kwa utaalamu bila yeye kujua akaniambia kuwa baba na mama yake walikufa huko Rwanda na yeye kuchukuliwa na mjomba wake ambae ndio anamlea hadi sasa. nikamuuliza nzeimana ukiwa mkubwa utakuwa chama gani ? Akajibu CCM. Nikammuliza kwann? Akajibu mjomba kaniambia CCM ikishindwa wageni wote tutarudishwa kwenye chi zetu.
Jibu kama hilo nilipewa na dada mmoja mwenye asili ya msumbiji lakini anajiita mmakonde.

Baada ya hapo nikajiuliza swali kuwa ni nani anaisambaza nadharia hii ya upinzani ukishinda nchi itaingia kwenye machafuko?

'' EDUCATION IS ABILITY NOT NOTES''
Ukweli ni kuwa hao wote mpaka Nzeimana wana akili kuliko wewe. Nisamehe mkuu umeleta hoja acha ijadiliwe,sikutukani.
1; wanajua kuwa maendeleo yao ni wajibu wao wenyewe.siyo ya serikali,chama wala wafadhili. Wanatazama mifano hai kwa majimbo ya kisiasa kusiko na CCM hawaoni tofauti.
2;Wanajua wanahitaji nini katika dunia hii.Wameshaona mkate wa siagi bila amani hauliki,godoro bila amani unasinzia vipi.
3;Hawapendi kitu dharau,wanafuraha vile walivyo wasingehitaji bugdha.
Hayo mengine walikujibu tu kiungwana ili msikerane maana mapenzi pia yanahusika hapo. Ukimpenda mtu huangalii sana eti ni mfupi,mnene,hana pesa au nini sijui...unamtaka tu.

Sent from my TECNO 7C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom