malisoka
JF-Expert Member
- Jul 8, 2012
- 1,860
- 2,638
Baada ya kutokea vifo zaidi ya watu 15 katika mkanyagano wakati waamini wanaohisiwa ni wa dini ya kikristo wakigombea kwenda kukanyaga mafuta ya upako" huko moshi, mkoani kilimanyaro.
Kutokana na mashinikizo mbalimbali kutoka kwa Wakristo wasiokuwa na Imani kwa maji ya upako na mafuta ya upako, na hata kwa kebehi za dini zingine, kuna uwezekano wa Nabii Mwamposa kufikishwa mahakamani.
Kama atafikishwa mahakamani atakuwa shaihidi na sio mtuhumiwa. Atakuwa mtuhumiwa tu iwapo mafuta hayo yamewadhuru hao waliofariki au kujiruhiwa.
Kwa nini:
Tanzania inaruhusu wanachi wake kuamini kitu chocho ili mradi hawavunji sheria.
kwa hiyo kuamini kukanyaga mafuta sio kosa la walipata shida au sio kosa kwa Nabii Mwamposa.
Pili: Sio kosa la kidini kupaka mafuta.
Hapo kabla kwenye biblia watu na wafalme na manabii walipakwa mafuta ili kuwa na upako wa kufanya majukumu yao waliyopewa na munu pia yalitumika kwa ajili ya uponyaji. kama ninavyonukuu hapa chini.
Mafuta ya kutia, ambayo imetajwa mara 20 katika Maandiko, yalitumiwa katika Agano la Kale kwa kumwaga juu ya kichwa cha Kuhani Mkuu na uzao wake na kuinyunyiza hema na vyombo vyake vya ili kuzifanya kama takatifu na ambazo zimetengwa kwa Bwana (Kutoka 25 : 6; Mambo ya Walawi 8:30; Hesabu 4:16). Mara tatu imeitwa ", mafuta takatifu ya kutia" na Wayahudi walikatazwa kabisa kuitengeneza kwa matumizi binafsi (Kutoka 30: 32-33). Viungo vya mafuta ya kutia hupatikana katika Kutoka 30: 23-24 na vilikuwa na manemane, sinamoni na viungo vingine vya asili. Hakuna dalili kwamba mafuta au viungo hivi vina nguvu yoyote isiyo ya kawaida. Badala yake, ukali wa miongozo ya kuunda mafuta hayo ilikuwa mtihani wa utii wa Waisraeli na maonyesho ya utakatifu kabisa wa Mungu.
Hapo hakuna kosa la kidini/ Ukristo. kwa sababu pia yalitumika
Vifungu vinne tu vya Agano Jipya hurejelea mazoezi ya kupaka mafuta na hakuna hata mmoja wao anayoelezea matumizi yake. Tunaweza kutekeleza hitimisho letu kutoka kwa muktadha. Katika Marko 6:13, wanafunzi wanawapaka mafuta wagonjwa na kuwaponya. Katika Luka 7:46, Maria anatia mafuta miguu ya Yesu kama ibada. Katika Yakobo 5:14, wazee wa kanisa wanatia wagonjwa mafuta ya uponyaji. Katika Waebrania 1: 8-9, Mungu anasema kwa Kristo Anaporudi kwa ushindi mbinguni, "Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitakaa milele na milele ..." na Mungu anamtia mafuta Yesu "kwa mafuta ya furaha".
Haja ya kisheria.
lazima tujiulize nini chanzo cha vifo na majeruhi?
Chanzo ni umati wa watu kugombania kuwahi kukanyaga mafuta ya upako yaliyobarikiwa na nabii Mwamposa,
Ni kama kuwe na mkutano wa siasani na watu wakakanyagana au ni kama watu wakiwa kwenye mpira wa miguu halafu kwa sababu moja au nyingine wakakanyagana.
Sasa nani mwenye kosa?
Mkuu wa Polisi wa Mkoa, (kutokuwajibika ulinzi na usalama)
Mkuu wa polisi wa wilaya,(kutokuwajibika ulinzi na usalama)
Mkuu wa mkoa (awajibike kisiasa).
Nabii Mwamposa na waandaaji wake ni kama mashahidi ili kuthibitisha mashitaka ya hao hapo juu. (g vibali, mandalisi na mkusanyiko mkubwa.)
Viongozi hawa wanatakiwa kuchuliwa hatua za kindhamu na kisheria kwa kutokutimiza majuku yao vizuri.
Hawezi kuja mtu ambaye ni maarufu (Public figue) halafu wakakaa na kubweteka maofisini bila kuchukua taadhali ya mkusanyiko mkubwa wa watu. Hasa mashitaka yao yatanoga iwapo Nabii Mwampsa alikuwa na kibali cha Mkutano.
huu ndiyo ukweli kwa mtazamo wangu
Kutokana na mashinikizo mbalimbali kutoka kwa Wakristo wasiokuwa na Imani kwa maji ya upako na mafuta ya upako, na hata kwa kebehi za dini zingine, kuna uwezekano wa Nabii Mwamposa kufikishwa mahakamani.
Kama atafikishwa mahakamani atakuwa shaihidi na sio mtuhumiwa. Atakuwa mtuhumiwa tu iwapo mafuta hayo yamewadhuru hao waliofariki au kujiruhiwa.
Kwa nini:
Tanzania inaruhusu wanachi wake kuamini kitu chocho ili mradi hawavunji sheria.
kwa hiyo kuamini kukanyaga mafuta sio kosa la walipata shida au sio kosa kwa Nabii Mwamposa.
Pili: Sio kosa la kidini kupaka mafuta.
Hapo kabla kwenye biblia watu na wafalme na manabii walipakwa mafuta ili kuwa na upako wa kufanya majukumu yao waliyopewa na munu pia yalitumika kwa ajili ya uponyaji. kama ninavyonukuu hapa chini.
Mafuta ya kutia, ambayo imetajwa mara 20 katika Maandiko, yalitumiwa katika Agano la Kale kwa kumwaga juu ya kichwa cha Kuhani Mkuu na uzao wake na kuinyunyiza hema na vyombo vyake vya ili kuzifanya kama takatifu na ambazo zimetengwa kwa Bwana (Kutoka 25 : 6; Mambo ya Walawi 8:30; Hesabu 4:16). Mara tatu imeitwa ", mafuta takatifu ya kutia" na Wayahudi walikatazwa kabisa kuitengeneza kwa matumizi binafsi (Kutoka 30: 32-33). Viungo vya mafuta ya kutia hupatikana katika Kutoka 30: 23-24 na vilikuwa na manemane, sinamoni na viungo vingine vya asili. Hakuna dalili kwamba mafuta au viungo hivi vina nguvu yoyote isiyo ya kawaida. Badala yake, ukali wa miongozo ya kuunda mafuta hayo ilikuwa mtihani wa utii wa Waisraeli na maonyesho ya utakatifu kabisa wa Mungu.
Hapo hakuna kosa la kidini/ Ukristo. kwa sababu pia yalitumika
Vifungu vinne tu vya Agano Jipya hurejelea mazoezi ya kupaka mafuta na hakuna hata mmoja wao anayoelezea matumizi yake. Tunaweza kutekeleza hitimisho letu kutoka kwa muktadha. Katika Marko 6:13, wanafunzi wanawapaka mafuta wagonjwa na kuwaponya. Katika Luka 7:46, Maria anatia mafuta miguu ya Yesu kama ibada. Katika Yakobo 5:14, wazee wa kanisa wanatia wagonjwa mafuta ya uponyaji. Katika Waebrania 1: 8-9, Mungu anasema kwa Kristo Anaporudi kwa ushindi mbinguni, "Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitakaa milele na milele ..." na Mungu anamtia mafuta Yesu "kwa mafuta ya furaha".
Haja ya kisheria.
lazima tujiulize nini chanzo cha vifo na majeruhi?
Chanzo ni umati wa watu kugombania kuwahi kukanyaga mafuta ya upako yaliyobarikiwa na nabii Mwamposa,
Ni kama kuwe na mkutano wa siasani na watu wakakanyagana au ni kama watu wakiwa kwenye mpira wa miguu halafu kwa sababu moja au nyingine wakakanyagana.
Sasa nani mwenye kosa?
Mkuu wa Polisi wa Mkoa, (kutokuwajibika ulinzi na usalama)
Mkuu wa polisi wa wilaya,(kutokuwajibika ulinzi na usalama)
Mkuu wa mkoa (awajibike kisiasa).
Nabii Mwamposa na waandaaji wake ni kama mashahidi ili kuthibitisha mashitaka ya hao hapo juu. (g vibali, mandalisi na mkusanyiko mkubwa.)
Viongozi hawa wanatakiwa kuchuliwa hatua za kindhamu na kisheria kwa kutokutimiza majuku yao vizuri.
Hawezi kuja mtu ambaye ni maarufu (Public figue) halafu wakakaa na kubweteka maofisini bila kuchukua taadhali ya mkusanyiko mkubwa wa watu. Hasa mashitaka yao yatanoga iwapo Nabii Mwampsa alikuwa na kibali cha Mkutano.
huu ndiyo ukweli kwa mtazamo wangu