Nabaguliwa kisa dini na kabila

Nabaguliwa kisa dini na kabila

mark11

Member
Joined
Nov 27, 2011
Posts
29
Reaction score
1
salaam wanajamvi,
Leo nimeamua kuandika kuelezea umma namna udini na ukabila ulivyojengeka nchini, hususani katika mapenzi. Mimi ni mhandisi mhitimu wa chuo kikuu nina miaka 28. Mara ya kwanza kujihusisha na mahusiano ilikua mwaka 2006, wakati huo nikiwa form 6. Nakumbuka ilikua Dodoma, nilipokutana na mpenzi wangu huyo wa kwanza katika maisha yangu. Tulipendana sana, na tuliwekeana malengo na mipango mingi ambayo kwa asilimia kubwa tuliweza kkuitimiza.
Matatizo yalianza kuzuka mwaka 2007 huyu binti alipoenda chuo kusoma na mimi nikachagua kufanya kazi kwanza, kampuni flani hivi ya madini. Vikaanza visa kila kukicha , japo nilijaribu kumtimizia kila alichohitaji.....hatimaye aliamua nimwaga rasmi mwaka 2009
Nakumbuka nilimwaga machozi na kuchanganyikiwa. wakati huo nilikua nimejiunga na chuo , niko mwaka wa kwanza.... tulikua katika mitihani...nilifeli karibu nusu ya mitihani yote. ilinichukua miaka miwili kusahau kidogo kilichotokea.
Binafsi, sikuweza kuanzisha mahusiano na binti yoyote kwa kua katika nafsi yangu nilikua nampenda x wangu tu. wapo waliojaribu kunitega, relationships zingine zilivunjika ndani ya usiku mmoja.
Wakati nakaribia kumaliza mwaka wangu wa mwisho chuoni, mpenzi wangu wa zamani alirudisha mawasiliano na akanieleza sababu zilizosababisha aniache. akaniamabia ni kwa kua mimi ni mtu wa musoma , kwao sikubaliki. ati kuna dada yake aliwahi kupata mchumba mtu wa msoma akamsumbua sana, tangu siku hiyo ikawa nongwa kwao. sababu ingine akaniambia pia kwa kua mimi ni msabato.... ati kwao wasabato wanawachukulia kama walokole na wenye imani kali. akaniambia yuko tayari kurudiana na mimi iwapo tu nitaamua kubadili dini na kua mkatoliki kama yeye... ishu ya kabila atanitetea kwa mama yake na dada zake wawili (tena wote wahandisi, wasomi) ambao kila kukicha wamekua wakimpa semina za kutafuta mwanaume ambae ni mkatoliki na asiwe mtu wa musoma
Iliniuma sana, zaidi hata ya aliponipa kibuti mara ya kwanza. kwa kweli japo nampenda sana .. ishu ya kubadili dini nilimkatalia na ndio ikawa nimemkosa milele.
Baada ya miezi kadhaa, nilikutana tena na binti wa kichaga... mwanachuo, mhandisi wa fani sawa na yangu. katika urafiki wetu uliodumu kama miezi 6 , nikajikuta nimezama katika penzi lake na hapo ikabidi nimwambie ukweli mwanzoni mwa mwezi huu nia yangu kwake. yes , nilijua kuna kupata na kukosa.. na ni kweli, alikataa...akadai anafurahia sana urafiki wetu wa kawaida ..na nilipojaribu kumdadisi kama kuna kinachomzuia...story ikawa ile ile...kabila langu na dini yangu kwao havikubaliki....
uchungu niliopata siku hiyo siwezi simulia...nakumbuka nilienda slip way nikasimama na kushangaa bahari huku machozi yananitoka kwa zaidi ya masaa 6...
dini yangu, kabila langu imekua jinamizi kwangu.....nakereka zaidi na kauli kua nisubiri wangu anakuja.
nawashauri wote ambao mnabagua kwa udini na ukabila muache hizo mambo.. mnaumiza sana wengine. mpenzi wa kweli na mwenza wa maisha anapimwa kwa tabia na sio vigezo hivyo.
sina uhakika kama nitakuja kupenda tena, ni ubaguzi ... ubaguzi tu:shut-mouth:
 
I hate people wa hivyo wote mnaabudu Yesu mnatofautiana madhehebu tu nao ni tatizo.
Am sorry to say this dini/imani haina nafasi kwangu zililetwa na wazungu na waarabu kugawa watu.
Leo hii mimi amu muislam sababu nimezaliwa dar pwani ila ningezaliwa Mbeya au Bukoba ningekuwa mkristo.
Siku zote mahusiano ni uamuzi wa mtu those excuses are just rubbish
 
Last edited by a moderator:
Ndugu ukweli ndo huu watu wengi wanadai hamna ukabila bongo ila kidesgn upo ingawa chini chini tatizo watu wa musoma inaaminika wanapiga sana wanawake na wakatili kinoma kuhusu usabato watu wengi wanachukulia kama kitu ch ajabu maana nackia hamna pasaka wala christmas sasa unaweza hoji unajiita mkristo lkn hau acknoledge sherehe hizo chamsingi we tulia tu watu kibao wanamatizo ya kukataliwa kwa vitu vngne mf pesa,sura mbaya etc so usiwaze sana tafuta hela mengine yatafwata mapenz hayajengi nyumba wala nin over
 
I hate people wa hivyo wote mnaabudu Yesu mnatofautiana madhehebu tu nao ni tatizo.
Am sorry to say this dini/imani haina nafasi kwangu zililetwa na wazungu na waarabu kugawa watu.
Leo hii mimi amu muislam sababu nimezaliwa dar pwani ila ningezaliwa Mbeya au Bukoba ningekuwa mkristo.
Siku zote mahusiano ni uamuzi wa mtu those excuses are just rubbish

kweli watu wa design hiyo sio wazuli. kumbagua mtu kwa kabila ,Dini, kazi yake ,maeneo anayoishi. kwa kweli sio vizuri
 
mhhhhh!pole sana ila usikate tamaa
utampata uliepangiwa na mungu
vuta subra wa kwako yupo njiani,usijutie kua wa
kabila lako,jivunie hilo!hao wasomi hewa ujinga haujawatoka bado!

 
Hijabaguliwa wala nini.. Hesabu kama kibuti cha kawaida tu , wasichana wapo kibao mjini wewe unslialia
 
Tafuta Msabato mwenzako ikiwezekana awe anatokea Mara...problem solved!!!
Otherwise nina uhakika bandiko lako ni kind of an indirect advert, wapo watakaokuPM pindi waonapo hii makitu...problem solved again!!!!
Halafu una uhakika wazazi wako watamkubali mtu asiye Msabato??? naona umesukumia mzigo huo wa ubaguzi kwa jamii nyingine ya imani (believe me Wasabato pia mna tabia ya kuchaguana wenyewe, nina shahidi kibao)
 
Mhh pole sana...Dah Sema mngeoana halafu kila mtu abaki na dini yake...Kwa Mchagga kutosherekea Xmass na Pasaka kisa kaolewa na Msabato ni kitu kigumu aisee...Sema mngekaa myaongee kwamba mkiona mtaheshimiana na dini zenu...

Halafu kwanza nahisi wewe ndo utakuwa umeleta chokochoko za udini kwa hao Wapenzi wako kwani navyojua hakuna watu duniani wenyesisa kali kama wasabato kuanzia chakula, vinywaji, na niwadini kweli...huwa mnawishi hii dunia mkaishi wenyewe...Napatwa na mashaka kweli na bandiko lako....

Huenda uliwakwaza na udini wako ndo wakakumwaga....
 
Kaka rafiki zangu 10 kutoka mkoa wa mara ambao nimeweza kuwa nao karibu toka primary hadi sasa nilikwisha kuwa mtu mzima,huwa wanaukorofi fulani hata kama hauonekani basi hupo wachini chini.
Niliama chumba wakati nikiwa chuo sababu jamaa yangu wa msoma nilishidwa kuishi naye alikuwa mbinafsi kupitiliza.

Swala na imani hapo nijingine hilo halina shida,shida ni vyakula mnavyokuwa mnachagua kupitiliza.

Ila anyway badilisha mtazamo wako sana na kuwa mpole na ishi maisha yakawaida.
 
Kuepuka kadha hii rudi Musoma ukaoe tu, jamaa angu Mwita Chacha aliamua kurudi Musoma akabeba jiko anaishi kwa roho safi alikumbana na vioja kama vyako.
 
Kusema ukweli Sabato ni Wakristo, lakini kidogo mna mambo magumu , na ndiyo maana mnahisi kubaguliwa.
Mambo kama yafuatayo ni ishu sana:
-Kutokula nyama
z
-Kutokunywa soda

-Kutokula baadhi ya samaki.

-kutokunywa chai na kahawa.

-kutopika wala kugusa chochote jumamoc.

-chakula cha jmosi kupikwa ijumaa.

-jua likizama ijumaa sabato ishaanza.

-mambo ya lesoni, pathfinderz, makambi etc

-hakuna sikukuu zozote za kikristo.

-hakuna vipindi maalum vya kanisa kama vile Majilio, Kwaresma, Ijumaa kuu na Jumatano ya majivu.

-masharti kama kutokutengeneza nywele kwa mwanamke, wakati mnajua MWANAMKE NYWELE.

-Kutumia na kuamini zaidi agano la kale kuliko jipya.

Kweli mdada anahitaji maamuzi magumu kabisa kuamua kuachana na mambo aliyozowea na kuwa msabato.
Dadaangu wa tumbo moja akiamua kuwa msabato nitamkubalia, lakn nitalia sana na machozi yataenda tumboni.
 
Tafuta Msabato mwenzako ikiwezekana awe anatokea Mara...problem solved!!!
Otherwise nina uhakika bandiko lako ni kind of an indirect advert, wapo watakaokuPM pindi waonapo hii makitu...problem solved again!!!!
Halafu una uhakika wazazi wako watamkubali mtu asiye Msabato??? naona umesukumia mzigo huo wa ubaguzi kwa jamii nyingine ya imani (believe me Wasabato pia mna tabia ya kuchaguana wenyewe, nina shahidi kibao)

Hapo ni sawa na mlokole aoteshwe aende kuoa kwa lmamu wa msikiti wa Makunduchi.
 
Kusema ukweli Sabato ni Wakristo, lakini kidogo mna mambo magumu , na ndiyo maana mnahisi kubaguliwa.
Mambo kama yafuatayo ni ishu sana:
-Kutokula nyama
z
-Kutokunywa soda

-Kutokula baadhi ya samaki.

-kutokunywa chai na kahawa.

-kutopika wala kugusa chochote jumamoc.

-chakula cha jmosi kupikwa ijumaa.

-jua likizama ijumaa sabato ishaanza.

-mambo ya lesoni, pathfinderz, makambi etc

-hakuna sikukuu zozote za kikristo.

-hakuna vipindi maalum vya kanisa kama vile Majilio, Kwaresma, Ijumaa kuu na Jumatano ya majivu.

-masharti kama kutokutengeneza nywele kwa mwanamke, wakati mnajua MWANAMKE NYWELE.
R
-Kutumia na kuamini zaidi agano la kale kuliko jipya.

Kweli i see mi nilishindwa kabisa kuchumbia binti wa kisabato nilichoka alipo nambia lmani yao inazuia kunywa pepsi/coca cola/azam cola marufuku kula kiti moto, kambale lazima kunyoa panki
 
I hate people wa hivyo wote mnaabudu Yesu mnatofautiana madhehebu tu nao ni tatizo.
Am sorry to say this dini/imani haina nafasi kwangu zililetwa na wazungu na waarabu kugawa watu.
Leo hii mimi amu muislam sababu nimezaliwa dar pwani ila ningezaliwa Mbeya au Bukoba ningekuwa mkristo.
Siku zote mahusiano ni uamuzi wa mtu those excuses are just rubbish

And good enough u did nothing kuzaliwa pwani, it's just a matter of chance...nd as far tunaamini kwamba kila kitu kinatokana na mungu, then kama Mungu angeamua uzaliwe Mbeya, ungezaliwa tu huko coz' u'd no control over the issue nd leo hii ungekuwa Catherine!
 
Sijaona ubaya hao wapenzi wako kukwambia ukweli, kwanza wameelezea vikwazo vya penzi kati yako na wenyewe.

Ukweli ni uhuru.

Endelea kuwalaumu maana hata wewe hujaamua kuyapatia tiba matatizo yako,tafuta msabato pia mkurya yanini shida'
 
Back
Top Bottom