Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

Kwenye utawala wa Magufuli kila mkuu wa wilaya,mkoa pamoja na Mawaziri watacheza sana media ili ionekane wanafanya kazi.
 
Kurupuka, fungia nje maana wana maneno sana utawakuta wanasema nilikuwa namzidi darasani, mara alinyakwa mwaka wa ngapi fungia nje kata kilimilimi mpaka tuheshimiane

Sawa kabisa watu walizidi ugoigoi maofisini. Kuchelewa ndio ada. Na michango ya wanaJF uanatupa picha halisi ya Watanzania. Nidhamu inajumuisha mambo mengi ikiwa pamoja na Kuwahi!!!!!
 
All in all Muomgozo wa siku kama 2 unahitajika kwa ajili ya maelekezo kadhaa ( ila suala la kufungiwa geti sawasawa japo wazi ilitakiwa ale sahani na huyo afisa utumishi ili nae ashuke chini!!!! Jamani nadhani wafanyakazi wa serekali hamtuelewi na mnazidi kututia hasira kwa kukebehi juhudi za kuleta efficiency makazini! Mkumbuke mko hapo kutoa huduma na si kuuza sura!!!
 
Hatimaye ninaona umuhimu wa Watendaji wa Serikali ya JPM kufanya kazi kwa weledi zaidi kuliko kutegemea ziara za kustukiza na maamuzi ya kukurupuka. Kwa moyo mkunjufu natoa maoni yangu mapema ili tuendelee kuwa na imani na Serikali ya awamu ya tano ambayo imejipambanua kuwa Serikali ya hapa kazi tu.

Kwa kuwa watendaji wanafahamu Matatizo yaliyopo katika Ofisi na maeneo mbalimbali ni vyema wakafanya yafuatayo;

1. Kila Kiongozi aweke malengo maalumu kwa watu anao waongoza ili katika utendaji wao wa kila siku yafanyiwe kazi.Mfano:Huduma bora kwa Wagonjwa Hospitalini.(SPECIFIC).

2. Malengo hayo ni sharti yawe yanapimika katika utekelezaji;Mfano;Idadi ya wagonjwa watakaohudumiwa na huduma watakayoipata.(MEASURABLE)

3. Malengo hayo ni sharti yawe yanaweza kufikiwa endapo kutakuwa na rasilimali kama fedha, muda, madawa, vifaa, watu, teknolojia, utaalamu n.k (ARCHIVABLE)

4. Malengo ni sharti yawe yenye tija na yenye kumfanya mtendaji avutiwe na apende kuyatekeleza.Ni vyema lengo likawa la wastani na lenye kutekelezeka (REALISTIC)

5. Malengo ni sharti yawekewe muda wa kuyatekeleza.Sio kukurupuka (TIMELY).

Watendaji wanaofanya kazi zao kwa namna ya kustukiza na kukurupuka kutoa maagizo mbalimbali bila ya kuzingatia hayo wategemee yafuatayo;

1. Kutoa maagizo yasiyotekelezeka;Mfano; Watoto wajue KKK wakati hakuna vitendea kazi.
2. Kutoa maagizo kwa watu wasiohusika na maagizo hayo;
3. Kutoa maagizo katika muda ambao sio muafaka Mfano;
4. Kutoa maagizo pasipo na rasilimali
5. Kutoa maagizo yasiyo na time frame
6. Kutoa maagizo mbele ya Waandishi wa habari bila kufuatilia utekelezaji
7. Kutoa maagizo ambaye ni kinyume na sheria
8. Kutoa maagizo yanayokinzana na haki za binadamu
9. Kutoa maagizo yenye nia ya kujikweza mbele ya wana habari
10. Kutoa maagizo yenye kuumiza upande mmoja.

Ni vyema pia Watendaji wa JPM wakaachana na suala la kuambatana na Waandishi wa habari katika utekelezaji wa Majukumu yao. Sioni mantiki ya kila walifanyalo kuwa karibu na wanahabari.
 
watanzania bila kutumia udictator... mambo hayaend.. yan utaongea watu hawatekelezi...
af watanzania bhaana daaah.. kikwete alikua hafanyi lolote alikua mpole watu wamemponda.. amekuja mwenye kutenda watu hao hao tena wameongea.. duuu... me hata cjui niwaweke kundi gan sasa.
 
watanzania bila kutumia udictator... mambo hayaend.. yan utaongea watu hawatekelezi...
af watanzania bhaana daaah.. kikwete alikua hafanyi lolote alikua mpole watu wamemponda.. amekuja mwenye kutenda watu hao hao tena wameongea.. duuu... me hata cjui niwaweke kundi gan sasa.
Likizo ni haki ya mfanyakazi, sasa ukimnyima atakuwa na moyo wa kufanya kazi? Wajibu unatakiwa uendane na haki!
Pia anatakiwa aongeze mishahara, sio kukimbilia tu "Hapa Kazi tu" wakati mshahara haufiki hata wiki moja!
 
Magufuri kinacho mpa shida nikutaka kujipa uperfect nakutaka kufata mfumo wa mwalimu ambao hauwezekan kwa sasa.
Hata huyo Rais Nyerere aliipeleka nchi mrama. watu walifika wakila sembe la yanga, kununua chakula kwa kadi na idadi maaalum, kuendesha gari mpaka jumapili, kupiga mswaki kutumia dawa ni kosa la jinai. mikoa kusini watu kwenda uchi na alipon'gatuka T anzania ilikuwa bankrupt. je kwani lengo ni kutupeleka huko?

 
Hata huyo Rais Nyerere aliipeleka nchi mrama. watu walifika wakila sembe la yanga, kununua chakula kwa kadi na idadi maaalum, kuendesha gari mpaka jumapili, kupiga mswaki kutumia dawa ni kosa la jinai. mikoa kusini watu kwenda uchi na alipon'gatuka T anzania ilikuwa bankrupt. je kwani lengo ni kutupeleka huko?

Nyerere si maraika
 
Tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kukaa mwezi mzima bila ya Baraza la Mawaziri na alipotokea kutangaza baraza lenyewe akaacha Wizara nne bila ya Mawaziri ila aliweza kuwapata Manaibu wake. Siku moja baada ya kuapishwa kwake Rais Magufuli akaenda Wizara ya fedha na kukagua Mahudhurio ya wafanyakazi. Tangu hapo serikali yetu kwa sasa imekuwa ni ya kuviziana!

Alipokwenda Muhimbili wengine tulihoji mantiki ya kwenda kule, Maana matatizo ya Muhimbili kama ikifikia yatatuliwe na Rais maana yake Serikali nzima chini yake imeshindwa kufanya hivyo. Lakini yale matatizo yameendelea kuwepo na yataendelea kuwepo kwa kuwa chanzo au kiini cha matatizo yenye hakijashughulikiwa!

Lakini watanzania walikuwa wamechoshwa sana na hali ya ulegevu wa serikali iliyopita, kiasi kwamba kauli mbiu ya "Hapa Kazi" iliwavutia hasa pale walipoona mtoa kauli mwenyewe anapiga "Push Ups" majukwaani. Lakini matatizo yetu haya tuliyonayo hayatatatuliwa kwa mitulinga bali kwa kutumia akili. Hizi "Ziara za Ghafla" "Kufunga mageti" au "kuvamia" ni maonesha ya nguvu walizonazo watawala wetu, lakini si njia mujarabu za kuelekea kwenye lengo la kuwa na serikali Imara na taifa linalojitegemea!!

Kwa mfano tatizo la wagonjwa kulala chini Muhimbili halikuwa ni la vitanda bali aina ya huduma zinazotolewa huko wanakotoka hao wagonjwa wanaolala chini. Kama wagonjwa wote wanaokwenda kwenye Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya, za Mikoa na Hospitali za Rufaa za Kanda madaktari wanawaandikia wagonjwa waende Muhimbili kupimwa kwa kuwa huko tuu ndiko kwenye CT Scan na MRI basi bila shaka kulala chini kutaendelea mpaka pale vifaa hivyo vitakapokuwa kwenye ngazi za wilaya na Mkoa!!

Huu ni mfano mmoja tu ambao unaonesha kwamba hii staili ya kuviziana ambayo Ben Saanane ameiita "Slack Management" haina tija hata kidogo, ni staili ya kutaka wengine waumbuke na wengine waonekane ni wachapa kazi, itatuvuruga tu wala haitatutoa hapa tulipo. Kama tunataka kuendelea nayo Muasisi wake bado yupo, tumpe kazi na ataifanya kwa ufanisi sana. Augustine Lyatonga Mrema!![
Huna jipya
/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:
Viongozi wengi wa awamu ya tano ni Magumashi.Wengi wao wapo kuboresha maslahi binafsi na umashuhuri wao.Mathalani huyu Naibu aliyewafungia wafanyakazi saa moja na nusu asubuhi akiwa na waandishi wa habari kibao alfajiri ile ili wamripoti.
Ukifanya tathmini ya haya maamuzi ya kukurupuka utagundua kuwa hayana tija kwa mwananchi wa kawaida.
 
Back
Top Bottom