Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

Kwani haya wanayoyafanya wameyapata wapi kama sio kufuata nyayo za bwana mkubwa wao? Unataka semina elekezi gani? Unategemea rais atawaelekeza nini zaidi ya hayo hayo wanayotenda? Unataka awaelekeze mara ngapi kama ameshawaelekeza kwa vitendo alipofanya hivyo hivyo hazina na muhimbili? Mmeanzaaa!!!!! wakati wa kitwete milisema watendaji ndiyo wabaya yeye akabaki kama malaika! Sasa waziri amewaeleza cha kufanya kwa vitendo watendaji wanatekeleza mnasema awapesemina elekezi!!!! mpaka sasa kuna tofauti gani ya wanayofanya mawaziri na rais? Hapa Kazi tu!

Mimi naona il hotuba aliyotoa siku alioungua bunge inatosha kuwa SEMINA ELEKEZI. Mawaziri na watumishi wengine wa umma Ila mmiliki wa Ngurdoto hotel hawezi kufurahi hata kidogo maana zilitengwa 2bl!
 
Tutafika kwa kuwa nimeandika kuhusu "Push Ups" ukahisi ni wa kupuuzwa. Unajua zilitolewa Shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kutengeneza mashine zilizoharibika Muhimbili na leo hii bado ni mbovu. Yule aliyedhani tatizo ni bilioni tatu na si idadi ya wagonjwa wanayotumia mashine kwa siku, naye ni wa kupuuzwa?
 
Last edited by a moderator:
Semina elekezi ya 2 bilioni. Ngoja wadunge hivyo hivyo. Mkuu wa kaya atakuwa na urahisi wa kuchambua wasofaa pale atakapoamua kuangalia tija ya kila mmoja wao.
 
Watu walitaka mabadiliko. Swali ni je.....walikuwa tayari kwa haya wanayoyaona? Tatizo la Tanzania wengi wetu tumezoea maisha ya kuungaunga tuu.....Lazima hii kasi ya Magufuli iwaumize wengi na bado!
 
Khamisi Kigwangwala anafanya nini wizara ya afya?
Kuviziavizia tu!
 
Watu walitaka mabadiliko. Swali ni je.....walikuwa tayari kwa haya wanayoyaona? Tatizo la Tanzania wengi wetu tumezoea maisha ya kuungaunga tuu.....Lazima hii kasi ya Magufuli iwaumize wengi na bado!

hamna anayepinga kasi na mabadiliko but yafuate utaratibu na yawe na tija. Sijawahi kusikia eti njia moja wapo ya kumonitor utendaji kazi ulio na ufanisi ni kufungia watu nje ya ofisi
 
Naona MMEFUNGIWA NJE HAPO WIZARANI MNATWEET TU CHUKI ZENU......................
 
mtoa mada ni mtu aliekata tamaa kabisa hii ni serikali ya magufuli ni kaz tu ww endelea kuzunguka na fisadi lowassa mikoani baada ya kusimamisha zoezi kwa muda
 
Naona MMEFUNGIWA NJE HAPO WIZARANI MNATWEET TU CHUKI ZENU......................
Ndiyo tunaandika maelezo kwa nini tunakaa Mbagala na Kibamba halafu tunafanya kazi Mjini kati. Kwani huko tunakoishi hakuna kazi zinazofanana na taaluma zetu ili tuwe tunawahi kufika kazini?
 
Pigeni kazi siyo kulalamika kila siku

Mlizoe kufanya kazi kwa mazoe sasa mabadiliko yamekuja mmebaki kulalama kila siku
 
Umekuwa ni mtindo wa wanasiasa kutafuta umaarufu ili waonekane ni watenda kazi huu mtindo wa kuita waandishi wa habari na kufanya kufanya maamuzi ni masuala ya kipumbavu na yasiyo na tija kwa taifa
Haiwezekani kila viongozi wetu wanachokifanya waandishi wa habari wawepo au ina maana siku hizi viongozi wanaambatana na waandishi kila mahali?
Hizi ni siasa za kutafuta umaarufu.
 
Watu wanatafuta kick kwa nguvu........na hii itasababisha chuki maofisini, mfano anayofanya Mh.Kigwangala sidhani kama ni sahihi, nadhani atulie na kutafakari vizuri.
 
hamna anayepinga kasi na mabadiliko but yafuate utaratibu na yawe na tija. Sijawahi kusikia eti njia moja wapo ya kumonitor utendaji kazi ulio na ufanisi ni kufungia watu nje ya ofisi

Umetafsiri vibaya tena nasema vibaya suala la kuwafungia nje wachelewaji. Ebu tusubiri tuone kama ataendelea kuwafungia au hatua hiyo ni msisitizo kwa wafanyakazi kuwahi kwenye majukumu yao??? Tafsiri jamani.
 
Ha! Ha! Ha! ww kuna watu sasa ni fasheni kukurupuka na mahali pekee kwa kupandia ni kwa watumishi wa umma. Kama RC anasema kuwa kuanzia sasa hataki vikao vilipwe ilihali vishaidhinishiwa fedha na bunge na hajatoa maelekezo ya kufanya REALLOCATION hii ina maana kwamba fedha hizo zitakuwepo tu bila kazi?

Hapa ilitakiwa Makatibu Wakuu kama wataalam washauri nini kifanyike ktk baadhi ya vitu visivyokuwa na tija kwa taifa kama vile
  • Vikao, warsha na mikutano;
  • Fedha wa watumishi kushiriki michezo ya kitaifa ya SHIMIWI;
  • Fedha zilizotengwa kwa ajili ya safari za nje;
  • Fedha zilizotengwa kwa ajili ya Mwenge n.k
Bila watu hawa kutoa ushauri wa kitaalam nategemea mwaka ujao utakuwa na hoja nyingi za ukaguzi toka kwa CAG bila sababu yoyote. Lakini pia hadi sasa hakuna miongozo mipya iliyotolewa na wizara ya Fedha kwa ajili ya kuandalia bajeti ya mwaka 2016/2017 hili nalo lisipoangaliwa vizuri utakuta mkoa fulani umeweka bajeti za kutekeleza sherehe na kazi zilizopigwa marufuku

Ninayo mengi ila naishia hapa
 
Hamnaa! Hawa wote waliishakwenda semina elekezi. Kwani Magu ameleta watu wageni?
 
Back
Top Bottom