Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,579
- 161,432
Hivi Haya mambo ya kupigana risasi kisa tu madaraka unayaona ya kawaida? Tunisia ilichafuka na nchi haikutawalika tena, Na Rais ataondolewa madarakani kwasababu ya mwanafunzi mmoja muuza nyanya kusumbuliwa Na askari wa mji. Maelfu walipoteza maisha yao. Nchi ikichafuka bata tutalia wapi? Nani ataenda club kukiwa kunarindima mambomu? Nani ataenda kwenye ulabu risasi zikiwa zinapishana hewani? Nyumba za wageni zina Raha gani Na nje ni vufaru na mizinga ndivyo ninavyotamani? Tunahitaji kutubu kwa ajili ya ardhi ya Tanzania, wengi hawajui Hali hii ni ishara mbaya. Tukizizoea risasi hatutaziogopa tena. Tukizoea maiti tutazipenda Na hatutaona faida ya kuishi. Huo utakuwa ndio mwanzo wa Vita ya wenyewe kwa wenyewe. Pole najua hupendi kusoma maelezo marefu. Uwe na siku njema