Na kweli Diamond na wengine mna damu ya kunguni

BilioneaPATIGOO

JF-Expert Member
Jun 23, 2012
12,321
11,315
Bwana Diamond na wengine wachache waache kuleta siasa, utani na unafiki kwenye roho na maisha ya watu.

Inaonesha wazi hauna msimamo, mara umeamua kukaa kimya mara unajishtukia unajidai "Kwakweli kwa hili siwezi kukaa kimya" , ...mara ghafla tena "Nina damu ya kunguni wacha nikae kimya...halafu bado unaawambia watanzania masikini wa download nyimbo yako kwa shilingi 300 kwamba mambo ya kuogofya ambayo hatujayazoea nchini kwetu unataka watanzania wakae kimya, mambo ya ovyo ovyo tu, sinema sinema tu za ovyo ovyo zinatokea vijana wakae kimya,wasanii wakae kimya, na kutafuta mikwaruzano na mtu kama Gwajima.. halafu wakishanunua hako kanyimbo utabaki kua tajiri, kumbuka aliepatwa na matatizo hayo ni baba mwenye familia kama wewe tu. Na ni kijana mwenzio. Sasa nashangazwa na akili zako finyu. Halafu useme Mungu atawasaidia watakua salama, lakin kama hatupazi sauti ina mana gani kumtaja Mungu akusaidie na wewe hujajisaidia hujachukua hatua ? Tunashukuru Mungu hata hivyo wamepatikana.

Na naona ume retreat ghafla baada ya kuona gwajima ametoa warning kesho kwamba " almasi itageuka maji" kwamba tutaelezwa yote na watanzania watajua mbivu na mbichi. Ama kweli una damu ya kunguni.
 
87aa644b902c83835d166b9150aa35f6.jpg

Maigizo ya kumteka mwenzao afu kinajifanya kutuimbia ushuzi eti tukae kimya
 
Wanaopigania uhuru wa kutoa maoni na kujieleza....na wao pia hawaheshimu maoni ya wengine.......

Wao maoni ya wengine yanayopendeza ni yale yanayopendeza masikioni mwao.....na yanayoendana na mihemko yao.....ukitoa maoni yenye kwenda kinyume na utashi wa nafsi zao.....utatukanwa kila aina ya tusi.....

Haishangazi kuona leo Nape akipata mikusanyiko mikubwa kwenye vikao vyake....kwa kuwa wanajua atazungumza yale wanayotaka kuyasikia......Nape huyo huyo alipoongea yasiyopendeza masikioni mwao....aliitwa kila aina ya jina baya.....

Msawazo kwenye jamii unaletwa na wanajamii kuvumiliana na kuheshimiana.....,

Vile ambavyo wewe unapenda maoni yako na mitazamo yako iheshimiwe ndivyo na wewe unapaswa kuyaheshimu maoni na mitazamo ya wengine...hata kama inatofautiana na ya kwako.....
 
Wanaopigania uhuru wa kutoa maoni na kujieleza....na wao pia hawaheshimu maoni ya wengine.......

Wao maoni ya wengine yanayopendeza ni yale yanayopendeza masikioni mwao.....na yanayoendana na mihemko yao.....ukitoa maoni yenye kwenda kinyume na utashi wa nafsi zao.....utatukanwa kila aina ya tusi.....

Haishangazi kuona leo Nape akipata mikusanyiko mikubwa kwenye vikao vyake....kwa kuwa wanajua atazungumza yale wanayotaka kuyasikia......Nape huyo huyo alipoongea yasiyopendeza masikioni mwao....aliitwa kila aina ya jina baya.....

Msawazo kwenye jamii unaletwa na wanajamii kuvumiliana na kuheshimiana.....,

Vile ambavyo wewe unapenda maoni yako na mitazamo yako iheshimiwe ndivyo na wewe unapaswa kuyaheshimu maoni na mitazamo ya wengine...hata kama inatofautiana na ya kwako.....
COMMENT OF THE DAY.
 
Nilipousikiliza huo wimbo na kuona amemtaja Mange kwamba eti ndiye anaye wachonganisha Gwajima na Bashite nikamhurumia huyu dogo. Atafunuliwa mpk kunako pahala. Chezea Mange na Gwajima wewe!! Anajifanya eti analea. Kana kwamba yeye ndiye wa kwanza kuzaa hapa Tanzania.
 
Huyu Daimondo anaweza kuharibu jina lake zuri katika muziki kwa kujikomba komba kwa zero Daudi Bashite. Tunaonunua nyimbo zako ni sisi. Tunaoingia kwenye shoo ni sisi watu wa kawaida. Huyo Daudi si wa kudumu. Atakuharibia.

Kwa hyo wewe kununua kazi za msanii na kunamnyima yeye moja kwa moja kutoa maonu yake ambapo kikatiba ni haki yake.....!!??

Kwa hiyo msanii anapaswa kuwa mtumwa wa maoni na utashi wa mashabiki wake.....!!?
 
Bwana Diamond na wengine wachache waache kuleta siasa, utani na unafiki kwenye roho na maisha ya watu.

Inaonesha wazi hauna msimamo, mara umeamua kukaa kimya mara unajishtukia unajidai "Kwakweli kwa hili siwezi kukaa kimya" , ...mara ghafla tena "Nina damu ya kunguni wacha nikae kimya...halafu bado unaawambia watanzania masikini wa download nyimbo yako kwa shilingi 300 kwamba mambo ya kuogofya ambayo hatujayazoea nchini kwetu unataka watanzania wakae kimya, mambo ya ovyo ovyo tu, sinema sinema tu za ovyo ovyo zinatokea vijana wakae kimya,wasanii wakae kimya, na kutafuta mikwaruzano na mtu kama Gwajima.. halafu wakishanunua hako kanyimbo utabaki kua tajiri, kumbuka aliepatwa na matatizo hayo ni baba mwenye familia kama wewe tu. Na ni kijana mwenzio. Sasa nashangazwa na akili zako finyu. Halafu useme Mungu atawasaidia watakua salama, lakin kama hatupazi sauti ina mana gani kumtaja Mungu akusaidie na wewe hujajisaidia hujachukua hatua ? Tunashukuru Mungu hata hivyo wamepatikana.

Na naona ume retreat ghafla baada ya kuona gwajima ametoa warning kesho kwamba " almasi itageuka maji" kwamba tutaelezwa yote na watanzania watajua mbivu na mbichi. Ama kweli una damu ya kunguni.

Sijapenda tu alivyotumia picha ya Nyerere kwenye wimbo usioendana na heshima ya kiongozi mwenyewe.

Otherwise namuonea huruma kujihusisha na mambo ya siasa kwa nchi yetu ambayo kila mwanasiasa anayeingia madarakani anafanya yake bila kubanwa na katiba.
 
Wanaopigania uhuru wa kutoa maoni na kujieleza....na wao pia hawaheshimu maoni ya wengine.......

Wao maoni ya wengine yanayopendeza ni yale yanayopendeza masikioni mwao.....na yanayoendana na mihemko yao.....ukitoa maoni yenye kwenda kinyume na utashi wa nafsi zao.....utatukanwa kila aina ya tusi.....

Haishangazi kuona leo Nape akipata mikusanyiko mikubwa kwenye vikao vyake....kwa kuwa wanajua atazungumza yale wanayotaka kuyasikia......Nape huyo huyo alipoongea yasiyopendeza masikioni mwao....aliitwa kila aina ya jina baya.....

Msawazo kwenye jamii unaletwa na wanajamii kuvumiliana na kuheshimiana.....,

Vile ambavyo wewe unapenda maoni yako na mitazamo yako iheshimiwe ndivyo na wewe unapaswa kuyaheshimu maoni na mitazamo ya wengine...hata kama inatofautiana na ya kwako.....
Kinachojadiliwa hapa ni connection ya hayo maoni na magtukio yanayoendelea, ni suala la kupanua tafakuri tu-shida kubwa tuliyo nayo hapa ni idadi kubwa ya akina Bashite ambao hawataki kushirikisha ubongo wao. Kamsome vizuri Maulidi Kitenge, hicho ndicho watu wanatafakari na wala hawana tatizo na maoni ya watu na ndio maana kilio cha wengi ni kuona wanakuwa huru kutoa maoni!
 
Sijapenda tu alivyotumia picha ya Nyerere kwenye wimbo usioendana na heshima ya kiongozi mwenyewe.

Otherwise namuonea huruma kujihusisha na mambo ya siasa kwa nchi yetu ambayo kila mwanasiasa anayeingia madarakani anafanya yake bila kubanwa na katiba.

Unapingana na wasanii kujiingiza na mambo ya siasa au unapingana na wasanii wanaotoa maoni ya kisiasa yanayokinzana na maoni yako.....!!??
 
Kwa hyo wewe kununua kazi za msanii na kunamnyima yeye moja kwa moja kutoa maonu yake ambapo kikatiba ni haki yake.....!!??

Kwa hiyo msanii anapaswa kuwa mtumwa wa maoni na utashi wa mashabiki wake.....!!?
mkuu humu jf nilidhani kuna ma GT lakini ni aibu. Wao wanadhani kupiga marungu ni kuhusu serikali tu bali ukiwasema wengine ni dhambi. Roma leo shujaa lakini roma akiwalima kina mbowe tu ataambiwa amenunuliwa na CCM. Ndiyo hapo utajua Tanzania tunalinganishwa na misukule maana hatujui hata tunataka nini. Unaposema uhuru lazima ukubali kuutumia na uruhusu wengine wautumie huo huo uhuru bila bughuudha ili mradi hawavunji sheria.
 
Diamond mi ni shabiki yake mkubwa lakini kwa wimbo huu hapana amejiharibia sana na nimemshusha
 
Kinachojadiliwa hapa ni connection ya hayo maoni na magtukio yanayoendelea, ni suala la kupanua tafakuri tu-shida kubwa tuliyo nayo hapa ni idadi kubwa ya akina Bashite ambao hawataki kushirikisha ubongo wao. Kamsome vizuri Maulidi Kitenge, hicho ndicho watu wanatafakari na wala hawana tatizo na maoni ya watu na ndio maana kilio cha wengi ni kuona wanakuwa huru kutoa maoni!

Hata kama ni connection ya gani lakini yanabaki kuwa ni maoni yake kama ambavyo msanii Ney wa Mitego alivyotoa maoni yake kupitia wimbo wake.......

Kilichopo ni kwamba watu si wavumilivu kuvumilia maoni ya wengine hasa yale wanayokinzana na maoni yao......na hiyo ni nafsi ya udikteta.....kwa hiyo watu hao hawana uhalali wa kupigania uhalali uhuru wa kutoa maoni kwa kuwa hata wao si waumini huo uhuru.......
 
Back
Top Bottom