Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Nikiwa kazini katika kampuni ya ujenzi barabara hapa mjini iringa nilishuhudia kihoja hiki.Kampuni ya Interbeton baada ya kupata hasara kubwa kutokana na wizi wa mafuta,imeamua kuajiri wazungu ili kudhibiti wizi wa mafuta.
Basi bwana,tukiwa site alikatiza jamaa mmoja akiendesha baiskeli yake huku akiwa amepakia dumu kubwa taaratib akitokea Tanangozi kwenda Iringa mjini. Mzungu kuona lile dumu,akawasha hardbody yake na kumfukuzia yule bwana akidhani ni mwizi wa mafuta.
Alipomfikia,akafunga breki kali sana mbele ya mwenda kwa baiskeli, akashuka bila hata ya kuzima gari vizuri,akamvaa mnyalu wa watu na kufungua mfuniko wa lile dumu.
Looh! Kumbe lile lilikuwa limejaa ulanzi,na kwa sababu ulanzi wenyewe ulitembezwa juani muda mrefu,alipofungua tu,ulanzi wote ulifoka juu kama champagne na kumchafua mzungu wa watu sura yote na shati lake lote.
Sikufuatilia zaidi kama yule mzungu alimlipa yule mnyalu hasara ya ulanzi uliomwagika.
Basi bwana,tukiwa site alikatiza jamaa mmoja akiendesha baiskeli yake huku akiwa amepakia dumu kubwa taaratib akitokea Tanangozi kwenda Iringa mjini. Mzungu kuona lile dumu,akawasha hardbody yake na kumfukuzia yule bwana akidhani ni mwizi wa mafuta.
Alipomfikia,akafunga breki kali sana mbele ya mwenda kwa baiskeli, akashuka bila hata ya kuzima gari vizuri,akamvaa mnyalu wa watu na kufungua mfuniko wa lile dumu.
Looh! Kumbe lile lilikuwa limejaa ulanzi,na kwa sababu ulanzi wenyewe ulitembezwa juani muda mrefu,alipofungua tu,ulanzi wote ulifoka juu kama champagne na kumchafua mzungu wa watu sura yote na shati lake lote.
Sikufuatilia zaidi kama yule mzungu alimlipa yule mnyalu hasara ya ulanzi uliomwagika.