Mzumbe dons in PhD scam

Nadhani mnaangalia Mzumbe tuu. Vyuo vyote Tanzania ni scum yaani i don't care utasema Mzumbe, UDSM, St. Agustino sijui Nyegezi. Sababu hakuna wakufunzi wa kutosha nchini Tanzania hivyo madhara yake ni kuwa na walimu wasio na vigezo.

IFM kuna baadhi ya washikaji zangu wanafundisha wakati wenyewe wana degree moja. Sasa najiuliza how is it posible mtu mwenye BS au BA akafundisha? I understand kama akiwa TA wakati anasoma PhD then anaweza kufundisha, lakini sio pimbi tuu eti kisa ana GPA 4.8 then anaqualify kufundisha. GPA is not a benchmark ya kuwa mkufunzi.

Kisha wao ndio wakwanza kukwambia aaah umesoma degree zako zote USA ooohh hizo ni feki degree.
That is a mess
 
==========================================
The list goes on and on:

Controversy
As Pacific Western University, i.e., prior to changing its name to California Miramar University, the institution was criticized on multiple occasions as a substandard educational institution or diploma mill. [19]
In May 2004 the US General Accounting Office presented the results of an eight-month examination of diploma mills and other unaccredited schools and federal employees holding their degrees to the U.S. Senate Committee on Governmental Affairs.[20] Pacific Western University in Los Angeles was one of the six schools on which the investigation focused.
Later that year, investigative reporters from television station KVOA of Tucson, Arizona described the Los Angeles campus of Pacific Western University: "We don't find students, classrooms or professors. Only a small office with two receptionists and a man who introduces himself as the dean."[21] KVOA noted that federal investigators had identified PWU as a diploma mill.[21][22] The station reported that Pima Community College in Tucson had reduced the salaries of two faculty members who previously had been paid at the Ph.D level based on their degrees from PWU.[21]
Internationally, Pacific Western University has a similar reputation. It was reported in the Irish Independent on 9 October 2005 that the Chief Science Advisor to the government of Ireland, Barry McSweeney, had been found to have advanced his career using a suspect degree obtained from Pacific Western University.[23][24] The newspaper report stated that McSweeney had obtained his Ph.D. in biotechnology and biochemistry from PWU in 1994 after just 12 months of study. It described PWU as having "no merit or standing in the academic world" and having been "the subject of numerous official investigations, state bans and media exposés" during its 28 years of operation.[23] McSweeney was forced to resign his position as a result.[25] In Australia, the Brisbane Courier Mail reported on 6 January 2004 that a lecturer at the University of Southern Queensland was banned from using the title of "Doctor" after it was discovered that his Ph.D. had been obtained from Pacific Western University.[citation needed]
"





Associate Professors
1. Moses M.D. Warioba DPA (IDM), Dip. Publ. Sect. Mgt (Aston), MBIM- (London), M.Sc. Publ. Sec. Mgt (Birmingham), Ph.D. (Public Admin.) PWU, (USA)
2. Leonard .J. Shio B.A (Ed) Hons. (UDSM.), M.A. (Econ. Dev.) (UDSM), Ph.D(Management) PWU, (USA)
3. M.N. Chao B.A (Ed.) Hons. (UDSM), M.A. (Dev. Studies) (UDSM), Ph. D. (PWU), USA Senior Lecturers
4. Raphael J.M. Habi ADPA (IDM), M.Sc.(Pers. Mgt) (Aston) (UK), MIPM (U.K.), Dip. T. & D. (Manchester) (UK), Ph.D(Management) PWU, (USA)
5. Christopher M. Sotta DPA (IDM), PG.D.(Gen.Mgt.)(IDM), MPA (IDM), Ph.D (Public Admin) PWU, U.S.A.
6. Aristarch K. Kiwango B.A. (Soc. Econ Admin) Makerere, M.Sc. (Econ.) Wales, Ph.D. (Econ.) PWU, (USA) PGD. (Project Planning)ISS,The Hague, PGD. (Pop & Dev Plan) ISS, The Hague
7. Colman Riwa B.A. (Education) (UDSM), PGD (Tesol) London, M.A. (Public Policy and Admin.) ISS, The Hague, Ph.D. (Public Administration) PWU, USA. (On leave of absence)

Kuna taarifa kuwa hizi ni habari za siku nyingi na wahusika walipewa maelekezo watafute PHD kwenye taasisi zinazojulikana na pia kuna tetesi MU watatoa clarification
 
LOL. Mzumbe versus UD imerudi? Kabla hamjaenda mbali ningeomba mkasome kule kwenye elimu. Hii ilishajadiliwa sana kule mpaka mwalimu Kichunguu akatoa theory ya Nungwi!
 
Hivi kwani ukiwa na Advanced diploma hairuhusiwi kuchukua Masters degree?

Mbona Sumaye kachukua Masters na advanced diploma yake?

Au mi ndo sielewi wandugu?
 
BADO YANAKUJA meeengi. Tunaangalia hawa wanaojiita Dr, Dr au maprofessor. Lakini kuna mwanzo, yaani hata wale wanaotafuta Bachellors. Kuna BSc na BA nyingi feki na ziko maofisini. Pale Kampala kuna Chuo kinajiita Kampala International ... Hapo waganda wanafahamu ni chuo cha wa-Tz na wakenya. Waganda hawasomi kabisa maana wanafahamu cheti cha hapo hakiuziki mtaani kwao. Sisi tumejaza watoto wetu ili wapate degree bila ku-disco eti! Rais wetu kaweka na siasa hivi majuzi akafungua tawi la CCM ndani ya chuo kilico ndani ya Uganda!!!!!

Sasa pale UD pia tuambieni. UDSM pamoja na Mzumbe quality ya hizo MBA executive ikoje??? Nasikia inaitwa yebo-yebo. Ndo mambo ya PWU hayo. Ni hakuna kitu!

UDSM na Muzumbe mumekuwa ni wazalishaji wa masters kibiashara.
Kila mtu anaqualify kusoma hizo executives zenu. Stupid![/
[/
QUOTE]

Kuna madogo wamemaliza chuo cha Uhasibu Arusha na wengine wamemaliza Tanzania Institute of Accountancy (zamani DSA) wengine CBE, hawa wote wamemaliza mwaka jana Advanced diploma na mwaka huo huo 2008 wamejiunga na Mzumbe university wanachukua Masters degree.

UPO hapo?

Mzumbe geukeni! Masters sio biashara!
 
Nadhani mnaangalia Mzumbe tuu. Vyuo vyote Tanzania ni scum yaani i don't care utasema Mzumbe, UDSM, St. Agustino sijui Nyegezi. Sababu hakuna wakufunzi wa kutosha nchini Tanzania hivyo madhara yake ni kuwa na walimu wasio na vigezo.

IFM kuna baadhi ya washikaji zangu wanafundisha wakati wenyewe wana degree moja. Sasa najiuliza how is it posible mtu mwenye BS au BA akafundisha? I understand kama akiwa TA wakati anasoma PhD then anaweza kufundisha, lakini sio pimbi tuu eti kisa ana GPA 4.8 then anaqualify kufundisha. GPA is not a benchmark ya kuwa mkufunzi.
Kisha wao ndio wakwanza kukwambia aaah umesoma degree zako zote USA ooohh hizo ni feki degree.
That is a mess

Mtanganyika punguza hasira. GPA ni kigezo mama katika kazi ya Taaluma ya elimu ya juu. Labda inawezekana hujui ni jinsi gani rank hizi zinaenda. UDSM na vyuo vingi vyenye kuzingatia uwezo wa mtaalam, wana minimum qualification ili uweze kufundisha nakumbuka kipindi mi namaliza ilikuwa ni GPA ya 3.8 or above. Ukiwa na degree moja huruhusiwi kutoa lecture bali ni kufanya Tutorial wakati ukisubiri kwenda kufanya masters au unafanya masters. Ukipata Masters unapandishwa rank na kuwa Assistant Lecturer, hapa unaweza fanya lectures kwa undergraduates chini ya usimamizi au ukishirikiana na Lecturer. Ukipata PhD unakuwa Lecturer na hapo sasa kupanda kuwa senior lecturer, Associate professor or full professor hutegemea na kazi yako ya Taaluma kama research na kuandika papers.

Kinachozungumziwa hapa ni hawa Malecturer ambao wana PhD zilizo chini ya kiwango na si kufundisha. Kwani kwa rank yao wanakuwa na majukumu makubwa sana ukilinganisha na TA au Ass Lecturer. Huu ndiyo mfumo wa kitaaluma katika elimu ya juu bongo ulivyo. Na vyuo makini hata ukiwa na PhD lakini kama GPA yako ya undergraduate ni below 3.8 hupewi nafasi ya kufundisha ulielewe hilo.
 
Yaani kuna watu nilisoma nao wakapata GPA ya lower 2nd they were so weak kitaaluma...you can imagine!

Nimekutana nao juzi wana masters za MU tayari...sasa sijui waliandikiwa au walitoa pesa..au ilikuwaje!

Nachokiona sii kazi kupata Masters ya MU!

Guys we thrieve for quality and we should not compromise it!
 
Yaani kuna watu nilisoma nao wakapata GPA ya lower 2nd they were so weak kitaaluma...you can imagine!

Nimekutana nao juzi wana masters za MU tayari...sasa sijui waliandikiwa au walitoa pesa..au ilikuwaje!

Nachokiona sii kazi kupata Masters ya MU!

Guys we thrieve for quality and we should not compromise it!

Mbona kuna wajinga wajinga tena kibao ninaowafahamu wana Masters za UDSM? Masters kwa vyuo vyetu imeshakuwa biashara! Mapungufu kwenye mfumo wa elimu ya Tanzania kwa ujumla kwa sasa ni tatizo.

Serikali inaongeza shule za kata bila walimu, na vyuo vikuu bila walimu pia. Ni jana tu nimeambiwa kwamba University of Dodoma mwaka huu wame-enroll wanafunzi elfu nane!!!! Huu ni mwaka wao wa pili tangu Chuo kifunguliwe!! Hiyo academic staff iko wapi? Si lazima watakuwa wamebeba tu hizo hizo Masters za UDSM na Mzumbe ambazo msimamizi wako wa thesis mnakutana naye Break Point kwenye ugali wa muhogo na samaki Sato kisha anakufanyia marekebisho?

Hizo hizo Masters za UD mnazosema eti zina usimamizi, niliwa kukutana na washkaji zangu wako bize kumsubiri mtu ambaye wamemwandikia thesis na wanamdai pesa za kumfanyia hivyo!!!!! Tena pesa zenyewe wanadaiana baa! And he graduated!!!

Acheni ushabiki wa vyuo! The whole education system has to be overhauled!!!
 
Kwa hiyo mtu akiwa na lower 2nd or even Pass asiruhusiwe kufanya Masters?
 
Kwa hiyo mtu akiwa na lower 2nd or even Pass asiruhusiwe kufanya Masters?

unaruhusiwa, inategemea ni master gani na masharti ya chuo au faculty husika. Ila huruhusiwe kuwa lecturer hata kama utapata PhD. Vyuo vingi vinaangalia sana GPA ya first degree iwe kuanzia 3.8.

Nchi za kifaransa (Francofonie) wao unaweza kuchukua PhD hata ukiwa na diploma (bila Bachelor wala masters).

Hofstede: ....lakini sio pimbi tuu eti kisa ana GPA 4.8 then anaqualify kufundisha. GPA is not a benchmark ya kuwa mkufunzi.

Niambie aliyewahi kupata GPA hii mimi binafsi nitamzawadia, actually kwa vyuo serious hasa vilivyo katika mfumo wa common wealth naona kama haiwezekani kupata hii.
 
Kwa hiyo mtu akiwa na lower 2nd or even Pass asiruhusiwe kufanya Masters?

Mzee mtu kilaza?????

Kwani ni sheria au lazima kuwa na masters hata kama ni weak candidates?

Kwani hawa watu hawawezi kufanya kazi zingine?

Unakuta mtu is so weak eti naye anataka kuwa MD? Au engineer?

Sii kuna vyuo vya VETA au Diploma?
 
Hofstede: ....lakini sio pimbi tuu eti kisa ana GPA 4.8 then anaqualify kufundisha. GPA is not a benchmark ya kuwa mkufunzi.

Niambie aliyewahi kupata GPA hii mimi binafsi nitamzawadia, actually kwa vyuo serious hasa vilivyo katika mfumo wa common wealth naona kama haiwezekani kupata hii.

Mkuu Nziku, naomba sana urekebishe hiyo quote yako, mimi sijaandika hayo maneno uliniyo quote please!
 
Hivi kwani ukiwa na Advanced diploma hairuhusiwi kuchukua Masters degree?

Mbona Sumaye kachukua Masters na advanced diploma yake?

Au mi ndo sielewi wandugu?


Hakuna sababu ya mtu asiye na advance diploma kuchukua Masters. Kama nilivyosema katika posti yangu moja ni kuwa Master hata Phd zinaangalia credits na masomo aliyochukua mwanafunzi katika college level education.

Mtu mwenye Bachelor katika Civil Engineering anaweza kuchukua master katika Economics lakini itabidi achukue masomo mengine ya economics ambayo hakuyachukua akiwa undergraduate.

Ufumo wa elimu ya Tanzania hauna hizo flexibility. Mtu akiwa na Bachelor ya Economics anafikiri yeye pekee yake ndio mwenye haki ya kusoma Economics.

Na mwenye bachelor anafikiri ni ndio mwenye haki ya kusoma Masters. Na mwenye PCM mwenye haki ya kuchukua Engineering.

Huku mtoni elimu ni chaguo la mwanafunzi. Kinachotakiwa ni mwanafunzi kufuata masharti ya shule anayosomea.
 
Mzee mtu kilaza?????

Kwani ni sheria au lazima kuwa na masters hata kama ni weak candidates?

Kwani hawa watu hawawezi kufanya kazi zingine?

Unakuta mtu is so weak eti naye anataka kuwa MD? Au engineer?

Sii kuna vyuo vya VETA au Diploma?


Hapa mzee unaboronga. Weakness au strongness haipo kabla mwanafunzi hajaanza program yenyewe.

Unapimaje hiyo weakness ya mwanafunzi :confused: Kuna wana-sayansi mashuhuri dunia kama Albert Einstein ambao walikuwa mediocre darasani lakini walionyesha vipaji vya juu baadaye.
 
Kuna madogo wamemaliza chuo cha Uhasibu Arusha na wengine wamemaliza Tanzania Institute of Accountancy (zamani DSA) wengine CBE, hawa wote wamemaliza mwaka jana Advanced diploma na mwaka huo huo 2008 wamejiunga na Mzumbe university wanachukua Masters degree.

UPO hapo?

Mzumbe geukeni! Masters sio biashara!
Mkuu ulitaaka wasome nini?......nyie ndio wale mnaoongeza miaka ya kusoma na kufanya vijana wapate hela wakiwa wazee.....
 
Waliokutwa na vyeti haramu Mzumbe wavisafisha
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Monday,February 16, 2009 @20:11


Uongozi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe umesema wahadhiri waliobainika kuwa na vyeti kutoka vyuo visivyotambulika, wanasoma sasa kwenye Chuo Kikuu cha Malawi kwa ajili ya kusafisha vyeti hivyo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Joseph Kuzilwa, alitoa taarifa hiyo leo Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba tatizo halikuwa la kughushi kama ilivyoelezwa awali kwenye baadhi ya vyombo vya habari.

"Tatizo halikuwa la kughushi au vyeti feki, bali ni wahusika kusoma na kupata shahada ya uzamivu kutoka vyuo ambavyo havina ithibati na wala hawakufanya suala hilo kwa makusudi, kwani kughushi cheti au kutoa cheti feki ni kosa la jinai," alisema Kuzilwa. Profesa Kuzilwa alitumia mkutano huo kufafanua kwamba hahusiki na sakata hilo la kuwa na cheti kisichotambulika.

Alisema suala hilo lilitokea miaka ya 2004 na 2005 na wahadhiri hao saba waliomba udahili katika vyuo vyenye ithibati inayotambulika, lakini kwa bahati mbaya wawili kati yao walifariki dunia. Kuzilwa alisema watano waliobaki wako katika hatua inayoridhisha ya kukamilisha utafiti wa tasnifu za Shahada ya Uzamivu na wanatarajia kuhitimu mwakani na si kweli kuwa na yeye alikuwapo kwenye suala hilo.

Alisema kuhusu uongozi wa chuo kuwafutia au kuwanyang'anya sifa wahadhiri hao, Baraza la Chuo liliagiza wahadhiri kutotumika katika shughuli za chuo mpaka watakapohitimu katika sifa za Udaktari na Falsafa katika udahili huo mpya. Hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wahadhiri wanane wa Chuo Kikuu cha Mzumbe akiwamo Makamu Mkuu wa Chuo waligundulika kuwa na shahada za uzamivu za kughushi.
 
Bado naamini kuwa watz wengi hatuhitaji elimu ya Juu!

VETA kila wilaya..na utundu wa wanafunzi wetu ktk vyuo vyao vya Ufundi.....yaaani we invest massively ktk middle level vyuo vya ufundi!

Hata China investment kubwa sana ni ktk Ufundi!

Sasa angalia Dodoma...80% wanafunzi ni Social Sciences...je hii itatufikisha wapi?

je mapinduzi ya Kilimo na Sayansi ni ktk NgwiNI???

Something is wrong!
 
Last edited:
Waliokutwa na vyeti haramu Mzumbe wavisafisha
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Monday,February 16, 2009 @20:11


Uongozi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe umesema wahadhiri waliobainika kuwa na vyeti kutoka vyuo visivyotambulika, wanasoma sasa kwenye Chuo Kikuu cha Malawi kwa ajili ya kusafisha vyeti hivyo.

Of all universities, including vyuo vyetu hapa Tanzania, kwa nini Chuo Kikuu Cha Malawi? Mbona naanza kuhisi kama kamchezo flani hivi kanaendelea

Alisema kuhusu uongozi wa chuo kuwafutia au kuwanyang'anya sifa wahadhiri hao, Baraza la Chuo liliagiza wahadhiri kutotumika katika shughuli za chuo mpaka watakapohitimu katika sifa za Udaktari na Falsafa katika udahili huo mpya. Hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wahadhiri wanane wa Chuo Kikuu cha Mzumbe akiwamo Makamu Mkuu wa Chuo waligundulika kuwa na shahada za uzamivu za kughushi.

Binafsi sijaielewa hiyo sentensi, huo ni udanganyifu waliufanya na wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria. 'KUTOTUMIKA kwenye shughuliza chuo ina maana wanaendelea kupata mshahara na marupurupu mengine huku wakiwa hata hawafundishi?
 
Baraza la Chuo liliamua lini wahadhiri hao wasitumike? Na kwanini lilikaa kimya muda wote huo na ilihali hizi habari zilikuwa zimeandikwa kwenye magazeti mengi nchini kwa kipindi kirefu sasa?
 
Bado naamini kuwa watz wengi hatuhitaji elimu ya Juu!

VETA kila wilaya..na utundu wa wanafunzi wetu ktk vyuo vyao vya Ufundi.....yaaani we invest massively ktk middle level vyuo vya ufundi!

Hata China investment kubwa sana ni ktk Ufundi!

Sasa angalia Dodoma...60% wanafunzi ni Social Sciences...je hii itatufikisha wapi?

je mapinduzi ya Kilimo na Sayansi ni ktk NgwiNI???

Something is wrong!

Mzalendohalisi:


Wewe sio educator na sababu unazotoa zinaboronga. Kwa maendeleo ya automation yaliopo sasa vyuo vya ufundi wa kati havina tena mpango.

Hata hayo mapinduzi ya kilimo unachosema wewe hayaji kwa kuanziswa shule za VETA. Kumbuka kuwa kila wilaya ilikuwa na shule ya sekondari ya kilimo na vyuo kibao vya maafisa kilimo wa ngazi mbalimbali na bado output ya mavuno kwa heka moja kwa Tanzania ni ndogo sana hata kwa kulinganisha na nchi za kiAfrika.

Nchi zinazoendelea zimehamua kufuata R&D (Research and Development) approach. Vichwa vinafanya kazi (R&D) na baadaye instructions zinapewa kwa watu wanaofanya production kufuatwa. Mtu yoyote mwenye akili timamu akipewa masharti ya kupanda mpunga atafuata na hakuna sababu ya kumpeleka chuo miaka mingi.

Kwa mtaji wa niliyoyasema vyuo vikuu ni muhimu. Na kama tunataka middle level, hicho ni kitu rahisi sana. Tuanzishe system ya entry level. Mtu yoyote anayemaliza chuo kikuu basi afanze kazi kama entry level kwa muda wa zaidi ya miaka miwili. Na kutokana na juhudi zake za kazi basi middle na senior level zifuate.

Hule utaratibu wa kuwa mtu ametoka chuo kikuu basi anakuwa Injinia umeharibu sana ufanisi wa makazi. Watu wengi wana akili za kufaulu mitihani lakini ni mabox kwenye kazi.
 
Back
Top Bottom