Mzumbe dons in PhD scam

Ndio maana hata Research hawafanyi, wamekalia kuwadisco watoto wa watu tuu. Hivyi vyuo hata WebCT havina yaani huwezi hata kuprove grade za mwanafunzi. what a mess

Kingine ni AIU [American Intercontinental University] chuo kama sebule yetu pale tabata. Nashangaa ukiingia Ebsco kutafuta publication za Tanzania utashangaa waandishi wengi ni Wazungu, sasa najiulizaga huu uyoga wa vyuo una kazi gani??

Sasa kisha mnalalamika credebility za wanafunzi. Bungeni sasa ndio kumejaa hizo degree za London school of commerce. Yaani it's a mess. Na watoto wao wemekuja huku wamekwenda AIU na kuchukua hizo hizo degree feki kama baba zao, na sasa ndio ma Marketing tycoon huko sijui Voda, tigo and zain ndio maana nashangaa baadhi ya strategy zinazokuwa implimented zinanifanya nijiulize who craft that peace of non sense. Mungu ibariki Tanzania
 
BADO YANAKUJA meeengi. Tunaangalia hawa wanaojiita Dr, Dr au maprofessor. Lakini kuna mwanzo, yaani hata wale wanaotafuta Bachellors. Kuna BSc na BA nyingi feki na ziko maofisini. Pale Kampala kuna Chuo kinajiita Kampala International ... Hapo waganda wanafahamu ni chuo cha wa-Tz na wakenya. Waganda hawasomi kabisa maana wanafahamu cheti cha hapo hakiuziki mtaani kwao. Sisi tumejaza watoto wetu ili wapate degree bila ku-disco eti! Rais wetu kaweka na siasa hivi majuzi akafungua tawi la CCM ndani ya chuo kilico ndani ya Uganda!!!!!

Sasa pale UD pia tuambieni. UDSM pamoja na Mzumbe quality ya hizo MBA executive ikoje??? Nasikia inaitwa yebo-yebo. Ndo mambo ya PWU hayo. Ni hakuna kitu!

UDSM na Muzumbe mumekuwa ni wazalishaji wa masters kibiashara. Kila mtu anaqualify kusoma hizo executives zenu. Stupid!
 
BADO YANAKUJA meeengi. Tunaangalia hawa wanaojiita Dr, Dr au maprofessor. Lakini kuna mwanzo, yaani hata wale wanaotafuta Bachellors. Kuna BSc na BA nyingi feki na ziko maofisini. Pale Kampala kuna Chuo kinajiita Kampala International ... Hapo waganda wanafahamu ni chuo cha wa-Tz na wakenya. Waganda hawasomi kabisa maana wanafahamu cheti cha hapo hakiuziki mtaani kwao. Sisi tumejaza watoto wetu ili wapate degree bila ku-disco eti! Rais wetu kaweka na siasa hivi majuzi akafungua tawi la CCM ndani ya chuo kilico ndani ya Uganda!!!!!

Sasa pale UD pia tuambieni. UDSM pamoja na Mzumbe quality ya hizo MBA executive ikoje??? Nasikia inaitwa yebo-yebo. Ndo mambo ya PWU hayo. Ni hakuna kitu!

UDSM na Muzumbe mumekuwa ni wazalishaji wa masters kibiashara. Kila mtu anaqualify kusoma hizo executives zenu. Stupid!



mbona unapaa hivyo, anza na degree kwanza, watu kusikiliza lectures kupitia madirishani! si mchezo
 
PhD za Bongo zimekuwa ni kama fasheni tu, kuna sababu nyingi sana. Kwanza Tanzania ina culture of silence ni hivi majuzi tu watu wameanza kupigia kelele mafisadi na wengine humu kwa majina ya bandia tunapiga kelele kweli huku tukiwa tumejaa woga wa kujulikana.

Utamaduni huu umefanya transparency kuwa ni mwiko kila kitu ni siri, nyaraka za serikali siri, ukitaka information sehemu yoyote ni siri na hata kuipata ni kazi kweliweli na ukiipata imebadilishwa na kupotosha.

Tukirudi kwenye mada PhD ni research training, Yaani ukifuzu kufanya research zenye kiwango kinachokubaliwa basi unakabidhiwa hiyo PhD ili uendeleze Research. Sasa mazingira ya Tanzania Research hazilipi, na nyingi ya research zinakuwa na pre determined results na biasness kama zile za REDET n.k. Upatikani wa data ni mgumu sana hasa secondary data, ambazo huku kwa wenzetu ni za kumwaga na hata ukitaka kila mwezi kutoa paper unaweza. Hilo kwa bongo ni ndoto, watu wanatafuta vyeti ili wapandishiwe mishahara basi. Research hazina incentives.

Pendekezo

Nafikiri kukiwa na Board ya Taaluma ambayo itakuwa na kazi kuwasajili watu wote wenye PhD Tanzania na kuwataka kila mwaka wapublish paper mbili ili PhD zao kuendelea kuwa recognised tutaweza kutenganisha pumba na mchele. usiposubmit paper inayokubalika kwa miaka mitatu whether mfululizo au kuwa na gap basi utatakiwa kuidefend upya thesis yako mbele ya baraza ili uendelee na status ya PhD hapo tutakuwa tumepiga hatua.

Kitu kingine ni kuwa na "pragiarism software", yaani iwe ni lazima kwa kila taasisi ya elimu ya juu kuwa na software hizo ambazo wanafunzi watatakiwa kusubmit kazi zao kupitia software hizo, ili atakaye copy ajulikane.

Kwa jinsi ilivyo sasa ni vigumu kwa mwalimu kugundua kuwa kazi unayosimamia ni original kwani wanafunzi wamekuwa wajanja na wanajifua vilivyo kudefend kazi za watu wengine.
 
mbona fake degree ni nyingi sana na ndugu zetu wakenya wanaongoza afrika mashariki (soma daily news ya leo) jamaa waliapply zaidi ya mia mbili and 12 were shortlisted for the post and only to find that only two held genuine certificate. there one kenyan found with fake degree at St John University at Dodoma. haya ndio mambo yote nasema ya kutafuta njia panda. hata mimi nikitaka hiyo fake degree napata lakini niko busy naandika proposal for PHD ili wakati nikija kusoma na kupata nijisikie furaha kuwa at least i deserve sio kwa kupewa.

Kweli Mzumbe imetia aibu that a perso rose up to Vice Chancelor position with fake PHD certificate. what a shame to all of us. TCU kaza buti.
 
mbona fake degree ni nyingi sana na ndugu zetu wakenya wanaongoza afrika mashariki (soma daily news ya leo) jamaa waliapply zaidi ya mia mbili and 12 were shortlisted for the post and only to find that only two held genuine certificate. there one kenyan found with fake degree at St John University at Dodoma. haya ndio mambo yote nasema ya kutafuta njia panda. hata mimi nikitaka hiyo fake degree napata lakini niko busy naandika proposal for PHD ili wakati nikija kusoma na kupata nijisikie furaha kuwa at least i deserve sio kwa kupewa.

Kweli Mzumbe imetia aibu that a perso rose up to Vice Chancelor position with fake PHD certificate. what a shame to all of us. TCU kaza buti.

Wakenya wamezidi magilini. Kuna jamaa nilikuwa nao shule kipindi flani huko nyuma, karibu wote waliokuwa na scholarship ukiwauliza watakwambia nafundisha university, kumbe wala si kweli coz wengi wao baadae huja kujikuta wanasema ukweli...."aagh nilisema tu ili nipate scholarship, niko mtaani". Kuhusu Mzumbe namesikia kuwa aliyekuwa VC kaingia tena shule apate PhD ya ukweli. Tatizo la wabongo tunapenda short cut!!!! kila kitu tunataka tukipate fasta bila hata ya kukisotea.... hapo ndipo shida inapoanza!
 
mbona fake degree ni nyingi sana na ndugu zetu wakenya wanaongoza afrika mashariki (soma daily news ya leo) jamaa waliapply zaidi ya mia mbili and 12 were shortlisted for the post and only to find that only two held genuine certificate. there one kenyan found with fake degree at St John University at Dodoma. haya ndio mambo yote nasema ya kutafuta njia panda. hata mimi nikitaka hiyo fake degree napata lakini niko busy naandika proposal for PHD ili wakati nikija kusoma na kupata nijisikie furaha kuwa at least i deserve sio kwa kupewa.

Kweli Mzumbe imetia aibu that a perso rose up to Vice Chancelor position with fake PHD certificate. what a shame to all of us. TCU kaza buti.

Haya matatizo na msimamo finyu tulionao, Huwezi kuhalalisha uchafu wako kwa kulinganisha na wa mwenzako kwa kusema kuwa mimi nina uchafu mdogo kuliko jirani yangu, uchafu ni uchafu tu ni lazima usafishwe wote hata kama ni kwenye kinibu. Eti umefumaniwa ugoni unasema wewe ndiyo mara ya kwanza kufumaniwa kwani fulani kisha fumaniwa mara kumi. Hii haihalalishi ugoni wako hata kidogo
 
......Kuhusu Mzumbe namesikia kuwa aliyekuwa VC kaingia tena shule apate PhD ya ukweli.

Tatizo kubwa hapa ni cost benefits. Ni haki kumpeleka mtu wa close to the age of 60 kusoma PhD? Anasoma kwa kutumia pesa ya nani na kwa faida ipi? Kama ni pesa ya Serikali, basi ni aibu. Yaonekana wamepania angalau waitwe Drs ki-halali.

Hizo pesa zingetumika kumusomesha kijana wa miaka 25 ili akitumikie chuo kwa miaka zaidi ya miaka 30! That is another leadership failure.
 
Tuwe na mahali pa kuanzia. Wakati wa vitendo ni huu. Tuanzie kwa kuipa meno kisheria TCU (kama bado haina meno hayo) ifanye ukaguzi kwa academic staff vyuo vyote vikuu nchini (public and private) kubaini wahadhiri vihiyo. Tusichelewe zaidi maana kila mwaka tunatoa matunda dhaifu mengi ambayo ni mabomu kwa maendeleo ya taifa. Ukaguzi ukianza, wahadhiri wenye shahada feki watajiondoa wenyewe kuogopa mkono wa sheria. Walau tuanze kuwaondoa vihiyo hao katika system ya ufundishaji vyuo vikuu na tuanze kuwa serious kuunda cream. Utitiri wa vyuo vikuu nchini, na uhaba wa wahadhiri uliopo, na bila ya kuwepo ukaguzi, basi vihiyo wengi watashika chaki vyuo vikuu na kupoteza maana kabisa ya university which is supposed to a centre of academic excellence in research, training and outreach (consultancies). lecturer mwenye PhD au Masters ya copying and pasting atawezaje kukifanya chuo kikuu a centre of academic excellence! Ni aibu kuwa sasa tumefikia mahala hata wakenya wanajazana vyuo vikuu vyetu kufundisha wakati hawana taaluma hizo. Private universities hasa zimulikwe sana. Zimejaa wakenya wasio na taaluma husika kwa kazi wanazoombea. Wanatudanganya kwa kuongoea kiingereza, na kwakuwa VCs au deputy VCs tulionao au afisa utumishi au bodi ya uajili ina vihiyo wa shahada feki kibao, basi wakati wa usaili mkenya huyu akiongea kiingereza (tena kibovu)wanamuona ndiye mtaalamu babu kubwa na kumpa ajira hapohapo. TCU ikiwa na meno kamili na kufanya compulsory (regular) inspections, uchafu huu utakimbia wenyewe.
 
Last edited:
Wakenya wamezidi magilini. Kuna jamaa nilikuwa nao shule kipindi flani huko nyuma, karibu wote waliokuwa na scholarship ukiwauliza watakwambia nafundisha university, kumbe wala si kweli coz wengi wao baadae huja kujikuta wanasema ukweli...."aagh nilisema tu ili nipate scholarship, niko mtaani". Kuhusu Mzumbe namesikia kuwa aliyekuwa VC kaingia tena shule apate PhD ya ukweli. Tatizo la wabongo tunapenda short cut!!!! kila kitu tunataka tukipate fasta bila hata ya kukisotea.... hapo ndipo shida inapoanza!

Mkuu,

Hao Mzumbe wote wameambiwa warudi kusoma shule za kweli kweli na wamepewa muda vinginevyo hizo Ph.D zitafutwa.

Hizo shule zetu kwa sasa ni mungu ibariki Tanzania, tusitegemee wasomi walio wengi ambao wanatumia vichwa vyao kufikiri yaliyo ya maana. Ukifundishwa na walimu kama hao unategemea nini?
 
........akishirikiana na MUSHOBOZI..........naye sijui yuko wapi.......

niko masomoni, ninabukua, sikotayari kuunganisha mambo zaidi na mwishowe nikaambulia ukihio. muda ukifika nitarudi. ila ninadharau hadidhi za abunuswi. wewe unaonekana mwanahesabu, hivi, vihio 7 kati ya wazuri 200 inaweza kufanya chuo feki au ni probability inapiga chenga. any way ninachokiona ni ushindani wa kichuo na ushindani huu ni advantage kwa mzumbe kujipanga upya. hata nkunya ni mshindani maana ni walewale waliokuwa wanazibia vyuo vingine kuwa vyuo vikuu akiwa DVC academic pale UDSM.
 
niko masomoni, ninabukua, sikotayari kuunganisha mambo zaidi na mwishowe nikaambulia ukihio. muda ukifika nitarudi. ila ninadharau hadidhi za abunuswi. wewe unaonekana mwanahesabu, hivi, vihio 7 kati ya wazuri 200 inaweza kufanya chuo feki au ni probability inapiga chenga. any way ninachokiona ni ushindani wa kichuo na ushindani huu ni advantage kwa mzumbe kujipanga upya. hata nkunya ni mshindani maana ni walewale waliokuwa wanazibia vyuo vingine kuwa vyuo vikuu akiwa DVC academic pale UDSM.

Buana Mushobozi, in fwacti lazima ukubali kuwa hadhi ya Mzumbe imedidimia from bad to worse kwa hii revelation.
Probability yako ya kiMzumbe ina dosari.Vihiyo 7 , tena akiwemo VC,toosha kabisa kuua morali ya kwenda pale, kwa mtu aliye serious na masomo.
Nakubaliana kuwa kuna ushindani ,lakini ushindani huu si wa kupapatikia titles, bukua bwana utoe researches za kuleta matumaini kwa watanzania, sio kujibanza katika vichochoro vya PWU or whatever that stands for.
Pata PHD safi, na hata mtu ukitoa mada wasomi waseme yes, we have gained from this fellow.
 
Buana Mushobozi, in fwacti lazima ukubali kuwa hadhi ya Mzumbe imedidimia from bad to worse kwa hii revelation.
Probability yako ya kiMzumbe ina dosari.Vihiyo 7 , tena akiwemo VC,toosha kabisa kuua morali ya kwenda pale, kwa mtu aliye serious na masomo.
Nakubaliana kuwa kuna ushindani ,lakini ushindani huu si wa kupapatikia titles, bukua bwana utoe researches za kuleta matumaini kwa watanzania, sio kujibanza katika vichochoro vya PWU or whatever that stands for.
Pata PHD safi, na hata mtu ukitoa mada wasomi waseme yes, we have gained from this fellow.

that's what i do with alot of publications in the web, though by then I had a single degree. the first thing as others have said is what I should do for the purpose of poor citzens, sio what I am with poor citzens.

sitetei uvihio, ila bwana mzumbe is the best to compare, agree with me or not.
 
Haya matatizo na msimamo finyu tulionao, Huwezi kuhalalisha uchafu wako kwa kulinganisha na wa mwenzako kwa kusema kuwa mimi nina uchafu mdogo kuliko jirani yangu, uchafu ni uchafu tu ni lazima usafishwe wote hata kama ni kwenye kinibu. Eti umefumaniwa ugoni unasema wewe ndiyo mara ya kwanza kufumaniwa kwani fulani kisha fumaniwa mara kumi. Hii haihalalishi ugoni wako hata kidogo

nO! SIO MATATIZO, huwezi kukaa, kulala na kufikia decision kwenye pandora's box bila kujua wengine wanaishije. ndio maana tunatumia syllubi zilizojaa case studies za nje in order to develop and advance. hatutakaa na kujua kama tumepiga hatua au la kama hatulinganishi maendeleo yetu na maendeleo ya wengine, au na weekness ya wengine. ndio maana tunaweza sema kuwa US is a superpower and Tanzania is a poorest country. All these a comparative analysis. be careful
 
I stand to be corrected. Taasisi tangulizi ya TCU, yaani HEAC -High Education Accredation Council, ilikwishapiga chini chuo hiki kisiwe chuo kikuu kutokana na mapungufu mengi ikiwemo academic staff chovu isiyokidhi mahitaji ya kitaaluma na mitaala isiyokubalika kitaaluma katika hadhi ya chuo kikuu. Zengwe likapikwa na chuo kikaanzishwa kupitia Act of the Parliament (siasa) badala ya mchakato wa kawaida wa tathmini (taaluma). Matokeo yake ndiyo hayo kuwa copying and pasting ya thesis zimekithiri chuoni hapo. Wanafunzi wake wamekuwa less challenging academically na hata socially. Hata masuala yanayohusu maslahi yao wenyewe wanafunzi wanashindwa kuhoji. Chuo kipo kama kimemwagiwa maji. Kimelowa. Chukulia sakata la vyuo vikuu hivi majuzi vilivyoelekea vyuo karibu vyote vya serikali kufungwa, umesikia nini kutoka MU? Kimyaaaaaa. kisingizio eti wanafunzi wana tabia nzuri!!!!. But it could be they are incapacitated to analyze and raise their demands at the right time of need. Unapokuwa na academic staff ya online PhDs (or masters acquired based on advanced diplomas!!!) unategemea output ya aina gani kwa wanafunzi![/QUOTE]


Mzumbe! Hii aibu, ila ninajiuliza mambo yafuatayo.

1. hivi mgomo ni standard ya kufanya watu wajione wao wanamapinduzi, ambao hawagomi ni mazezeta? na kuwa watu wanaoenda vyuo vya UDSM na vingine na kugoma wametoka shule tofauti na wale wanaokwenda MU? hata hilo ninalipinga maana 1st year akiwa na miezi miwili hana tofauti na yule 1st year wa miezi miwili MU. ninakumbusha kuwa qualifications hazina tofauti mpaka sasa hivi kuingia vyuo vyote hivi.

2. hivi kama syllabi hazina tofauti, mfano sheria kwa vyuo vyote, unadhani mwaka huu UDSM watasema wamesoma kisawasawa na hii fukuza fukuza kulinganisha na MU kitivo hicho hicho? maana sasa hivi UDSM habari nilizonazo kutoka kwa Lecturers wenzangu ni kuwa wametoka nyumbani walipokuwa baada ya migomo, sasa hivi wanafanya test baadaye 1st semieter exam, na kufunga huku wengine ndio wanafanya registration. migomo hii haina msaada wowote kwa maendeleo ya inchi na kwa mtu mwingine. ila vijana wa MU wako darasani.

3. migomo mara nyingi huwa inaanzishwa na watu wasiokuwa na chakufanya"the idol mind is the workshop of Devil" wangekuwa na la kufanya wasingekuwa na migomo,

4 niambie chuo yaani UDSM kina watu zaidi ya 16 elfu, ni lini kwenye maandamano na migomo ukaona angalau watu 4000. hamna. ni vitisho tu na viboko na kejeri zinawafanya watu wabaki nyumbani kwa kuogopa kudharirishwa na wanafunzi wachache. au kama waligoma kutolipa, mbona walipotakiwa kulipia na kujiregister kama kweli mgomo haukuwa upepo fuata bendera ni wanafunzi 2000tu hawakujaa formu na wengine waliapologize. je unaweza kuita huo mgomo? la hasha! hata hao 2000tayari wamelipa tayari na sasa wanarudi chuoni.

5. can we say UDSM students walikuwa na upeo wa juu kuhusu madhara, matokeo, na hatima ya mgomo kuliko wale wa MU.

6. VC UDSM; Mkandala aliwahi toa sababu za migomo pale UDSM kuwa ni pamoja na poor management na ndio maana MU management yao inaepuka migomo kwa utaratibu mzuri waliojiwekea na hivyo kuahidi kufuata mfumo huo huo.

7> tuwe waangalifu na hoja zetu vinginevyo zinatia wasiwasi wa fikra zetu. Ila Mzumbe kwa hili ni aibu sana.
 
I stand to be corrected. Taasisi tangulizi ya TCU, yaani HEAC -High Education Accredation Council, ilikwishapiga chini chuo hiki kisiwe chuo kikuu kutokana na mapungufu mengi ikiwemo academic staff chovu isiyokidhi mahitaji ya kitaaluma na mitaala isiyokubalika kitaaluma katika hadhi ya chuo kikuu. Zengwe likapikwa na chuo kikaanzishwa kupitia Act of the Parliament (siasa) badala ya mchakato wa kawaida wa tathmini (taaluma). Matokeo yake ndiyo hayo kuwa copying and pasting ya thesis zimekithiri chuoni hapo. Wanafunzi wake wamekuwa less challenging academically na hata socially. Hata masuala yanayohusu maslahi yao wenyewe wanafunzi wanashindwa kuhoji. Chuo kipo kama kimemwagiwa maji. Kimelowa. Chukulia sakata la vyuo vikuu hivi majuzi vilivyoelekea vyuo karibu vyote vya serikali kufungwa, umesikia nini kutoka MU? Kimyaaaaaa. kisingizio eti wanafunzi wana tabia nzuri!!!!. But it could be they are incapacitated to analyze and raise their demands at the right time of need. Unapokuwa na academic staff ya online PhDs (or masters acquired based on advanced diplomas!!!) unategemea output ya aina gani kwa wanafunzi![/QUOTE]


Mzumbe! Hii aibu, ila ninajiuliza mambo yafuatayo.

1. hivi mgomo ni standard ya kufanya watu wajione wao wanamapinduzi, ambao hawagomi ni mazezeta? na kuwa watu wanaoenda vyuo vya UDSM na vingine na kugoma wametoka shule tofauti na wale wanaokwenda MU? hata hilo ninalipinga maana 1st year akiwa na miezi miwili hana tofauti na yule 1st year wa miezi miwili MU. ninakumbusha kuwa qualifications hazina tofauti mpaka sasa hivi kuingia vyuo vyote hivi.

2. hivi kama syllabi hazina tofauti, mfano sheria kwa vyuo vyote, unadhani mwaka huu UDSM watasema wamesoma kisawasawa na hii fukuza fukuza kulinganisha na MU kitivo hicho hicho? maana sasa hivi UDSM habari nilizonazo kutoka kwa Lecturers wenzangu ni kuwa wametoka nyumbani walipokuwa baada ya migomo, sasa hivi wanafanya test baadaye 1st semieter exam, na kufunga huku wengine ndio wanafanya registration. migomo hii haina msaada wowote kwa maendeleo ya inchi na kwa mtu mwingine. ila vijana wa MU wako darasani.

3. migomo mara nyingi huwa inaanzishwa na watu wasiokuwa na chakufanya"the idol mind is the workshop of Devil" wangekuwa na la kufanya wasingekuwa na migomo,

4 niambie chuo yaani UDSM kina watu zaidi ya 16 elfu, ni lini kwenye maandamano na migomo ukaona angalau watu 4000. hamna. ni vitisho tu na viboko na kejeri zinawafanya watu wabaki nyumbani kwa kuogopa kudharirishwa na wanafunzi wachache. au kama waligoma kutolipa, mbona walipotakiwa kulipia na kujiregister kama kweli mgomo haukuwa upepo fuata bendera ni wanafunzi 2000tu hawakujaa formu na wengine waliapologize. je unaweza kuita huo mgomo? la hasha! hata hao 2000tayari wamelipa tayari na sasa wanarudi chuoni.

5. can we say UDSM students walikuwa na upeo wa juu kuhusu madhara, matokeo, na hatima ya mgomo kuliko wale wa MU.

6. VC UDSM; Mkandala aliwahi toa sababu za migomo pale UDSM kuwa ni pamoja na poor management na ndio maana MU management yao inaepuka migomo kwa utaratibu mzuri waliojiwekea na hivyo kuahidi kufuata mfumo huo huo.

7> tuwe waangalifu na hoja zetu vinginevyo zinatia wasiwasi wa fikra zetu. Ila Mzumbe kwa hili ni aibu sana.


Mkuu Mushobozi, karibu tena jamvini na pole kwa shughuli nzito ya kisomo uliyonayo.

NAPENDA SANA UNAVYOITETEA MU, that shows a passion you have for your alma mater.

Hivi Mushobozi tuwe wakweli..hivi kweli kwa Tanzania yetu..ukipata admission ya MU na UDSM...where are you likely to go? (ceteris peribus). Ukweli ni kwamba MU is also a good University, lakini is not all that glamorous as you would want us to believe. Chukulia publications za walimu wa Muzumbe na UD? can you even compare? Wewe umeshasema ni lecturer...unajua kabisa tunapima ubora wa vyuo kwa kuangalia input za walimu..I have ample example..walimu wa MU bado kabisa...ni wachache kama wapo wame publish kwenye international journals zenye academic credibility) ( I stand to be collected). This however does not imply kwamba hawana strength maeneo mengine. Mfano MU ni wazuri katika management (whatever that means), lakini ukweli unabaki pale pale, na madudu ya UD akina Mkandala (By the way Mkandala ana PhD ya Berkeley contrast na WARIOBA ana PhD ya Pacific Western University) Hapa tofauti ni kubwa hata kama Mkandala is not living to the expectations za wengi. Ukichukulia hata publications za Mkandala..WARIOBA au hata Kuzilwa...is no where! Please...Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Au mwanafunzi aliyefundishwa Constitutional Law na Shivji pale UD...can you ever compare him na mtu aliyefundishwa somo hilo hilo MU na mtu kama Binamungu? (hata kama jamaa ni kiazi..lakini uwezekano wa kuwa na uelewa mpana ni mkubwa)

MU hawawezi kushindana na UD..bado sana. Ila haina maana kwamba hawawezi kufikia standards za UD....wanaweza kufika na wakasurpass. Cha kufanya:

1. Waanze kuajiri walimu walioenda shule "ndefu" ukiangalia majorities wana masters..ni wachache wenye PhD. na wengi ni hizo hizo za kuunga unga..Tofauti na fani nyingi..academics lazima mtu awe kichwa hasa..na siyo hizi shule za kuunga unga...

2. Waanze kutafuta academic exchange na vyuo vikubwa vikubwa huko duniani (and you can also help kama uko nje ;-) wafanye exchange..kusudi wajulikane. Ukienda huko nje wengi wanajua University of Dar Es Salaam. Ni kitu ambacho inabidi wakifanyie kazi.

3. Wawatake walimu wao kufanya publications kwenye "referred journals" internationally.

4. wawa-encourage waalimu wao kuomba admission kwenye vyuo makini. Maana walimu ni kioo...kama ulisoma Pacific western University..usitegemee mwanafunzi wako unayemfundisha ataomba shule Yale au Cambridge (just an example). Ni vyema walimu wakasoma shule makini..siyo hizi shortcut, za ilmradi kuwa na PhD.

5. MU wajue kabisa wana weakness kuattract the best and the brightest. Waweke scheme ya kuattract vijana wenye exposure na shule nzuri. Wasiwe conservative na GPA factor kama ya UD, ofcourse GPA ni kigezo safi..lakini waangalie mtu kaaccomplish kitu gani ndo wampe ajira.

6. Wafanye collaboration na UD..they cant dispense UD. Wajifunze kula na adui yao..and in the process they can learn alot. Infact sasa Iam happy naona wameanza kuwa creative kuwa na course mbali mbali ambazo hata UD hawana. They should concretize this by hiring smart dons.

7. UD is still the best University in our country (whatever that means). Ila improvement is always needed. Na haina maana kwamba vyuo vingine haviwezi kuwa bora kuliko UD..only right strategy.

8. By the way hata internationals wanapita humu......hivi unafikiri watu wakiona kashfa kama hizi..VC wa chuo anatuhumiwa kupata "diploma mill" unafikiri watu wata bother hata kuomba exchange ya semister? wanajua kabisa hapa hakuna kipya...na I can assure you hawa watoto wanaokuja mfano kama Africa kwenye exchange wanakuwa wameshafanya thorough research kuhusu hivi vyuo. Kuliko wewe na mimi tunavyofikiria. Credibility ni muhimu sana. Hata University of Dodoma....hii kashfa ya wakenya itawasumbua sana...maana watu wanakuwa na walakini tayari. So MU bado..pull up your sleeve!

Hivi unafikiri Harvard wanafundisha nini? Au Oxford wanafundisha nini? hakuna kitu extra ordinary, kuna vyuo wanafundisha na wanatoa elimu nzuri sana perhaps kuliko wao....lakini ile reputation yao iko solid, kiasi kwamba by mere having that name on your certificate..will make a difference and certainly it will pull your applications ontop of the heap!
 
MU wawa-encourage waalimu wao kuomba admission kwenye vyuo makini. Maana walimu ni kioo...kama ulisoma Pacific western University..usitegemee mwanafunzi wako unayemfundisha ataomba shule Yale au Cambridge (just an example). Ni vyema walimu wakasoma shule makini..siyo hizi shortcut, za ilmradi kuwa na PhD.

Well done Masanja, from your contribution one notes that your sort of people is what academic exellence is reffered to!
 
Duh:

Naona mjadala mzima umegeuka kuwa Mzumbe vs UDSM. Ukweli wa mambo unabakia kuwa wanaosoma Mzumbe au vyuo vingine ni watanzania kama wale wanaosoma UDSM. Na wajibu wao kwa taifa ni hulehule.

Vilevile mtu mwenye advance diploma anaweza kwenda kuchukua Masters period.

Nchi nyingi zinatumia credit system. Mtu mwenye Bachelor anaweza kuchukua Masters kwa credit 30 (masomo 10). Na mtu wa Advance diploma credit 36 (masomo 12). Hivyo hakuna tofauti yoyote hile.

Tukirudi kwenye mada. Vyuo vinavyotoa advance diploma ni lazima vifanye transformations za program zao na kutoa Bachelor hili kuwafanya watanzania wawe competitive katika masuala ya kazi na masomo.

Transformation inayofanyika Mzumbe ni ya kuungwa mkono na mtanzania yoyote. Na vitendo vilivyofanywa wa waalimu hawa vinarudisha maendeleo ya nchi na vinaweza kufanyika mahali popote. Hivyo ni lazima transparency iwepo. Hivyo lawama zisiwepo katika kwa Taasisi yenyewe bali kwa individuals wanaotaka kujinufaisha bila kuwa na shahada zinazotakiwa.
 
Kwa hiyo hapa anayedanganywa ni nani? mimi naona huyu anayefojifoji, au kusaidiwa mitihani ndiye anajidanganya, what makes some one to decide to study something?? nadhani lengo ni kufahamu, saa kama umejiandikisha online studies ya finance au whatever, lengo ili ujue then unadanganya! mimi naona tatizo ni mtu mwenyewe lakini si kuwa distance learning in matatizo.

So kutaka kuwa na cheti kizuri, titles, zimefanya (may be this online degree si nzuri kwa waafrika?? especially TZ,) kwa nini other races wanasoma vizuri na wanaendelea nazo, ??? ni kwa sababu hatuko honest?? what if then someone is honest?

So this way has go no problem at all, sipokuwa individual wasiotaka kuelewa mambo basi ndio hufanya ionekane sio nzuri. Tofauti ni kuwa wenzetu they meant kuelewa kitu fulani, sisi tunataka watu waviogope vyeti vyetu!!!

Hapo linakuja swali kwa Nkunya kuwa, this was SAHIHI KWA HAWA LECTURERS KUWA NA DEGREE ZA AINA HIZO, KWANI WATANZANIA WASOMI WENGI WALIPOPATA PhD, they have nothing more to add!

nadhani kungekuwa na products kutokana na walio na PhD, basi nature ingewaondoa. sijaona tofauti ya masters, Phd in TZ, la kama wapo wachache sana.

maadamu tunataka vyeti tu, basi no problem wako tayari hata kufoji kwenye hivyo vyuo ambavyo vinatambuliwa!

KWA NINI WATU WANAFOJI VYETI TZ?? kuna tatizo sehemu jamani

Watu wanafoji vyeti Tanzania kwa sababu HAKUNA THE RULE OF LAW... Kama kweli tungekuwa na utawala wa sheria wenye kuheshimika then watu wasingethubutu kufanya vitu hivi.

At one time, Rais alimteua waziri wa sheria ambaye alikua ana hiyo fake degree. Kungekuwa na parliamentary scrutiny kama iliyopo US kwa watu wanaoshika nyadhifa kubwa then majamboz kama haya ya kufoji vyeti yangeweza gundulika mumo kamatini, kama tu wajumbe wa hiyo kamati ya ku-scrutinize wateuliwa wangekuwa wawazi na wakweli na kama hiyo kamati ingejumuisha wajumbe kutoka katika vyama vyote vya siasa na pia sisi akina yakhe wa mitaani (lay person).
 
Mzumbe University is one of the weak University na hata ukiangalia wanafunzi weng ambao wamesoma Mzumbe wengi wao huwa incompetent.They have good Grades ila in terms of delivering is an Issue!

Kama Waziri Maghemebe anataka apwe Heshima aanze kuzinyoa hizi Ph.D feki na watu warudi Shule,Na naomba asiishie hapo aende mbele zaidi na kuangalia Ph.D za wabunge na viongzoi mbali mbali.

To mention but a few

1.Dr. Makongoro Mahanga
2.Dr. Nchimbi
3.Dr. Mary Nagu

the list goes on..Hivi hapa Jf kwanini tusianze kutoa Honary degree?Naamini tutakuwa na watu kama hawa

Dr. M.M Mwanakijiji
Dr. Gembe
Dr.FMES
Dr. Kichuguu


The list goes on

Naongezea: Dr. D. Kamala; Dr. Z. Gama; (Msc) Lukuvi, (MA) Lyatonga Mrema n.k.
 
Back
Top Bottom