Kama ningekuwa mimi ningemfukuza uwanachama wa CCM mzee Sinde Warioba kwa kulitoboa jahazi lizame na waliomo ndani yake waliwe na papa.
Sera ya CCM ni serikali mbili, yeye anataka serikali 3. Hii haitoshi kumvua uanachama wake?
Mzee Warioba haoni zuri hata moja CCM na serikali yake wanafanya nchini, yeye ni kukosoa, kukosoa, kukosoa, kubeza, kubeza, kubeza tu huku akisubiri kulipwa mafao yake ya kustaafu hadi kufa. Sijui anadhani hayo mafao anayolipwa kila siku yanapatikanaje bila yeye kuchangia kuyaweka mazingira bora ya uzalishaji na ukusanyaji kodi.
Mzee Warioba hajalaani matukio na wale wote waliochoma moto mali ya umma na miundombinu ya uzalishaji na ukusanyaji kodi kama barabara, vituo vya mafuta, malori ya biashara, ATM, TRA vinavyozalisha fedha inayotumika kupata fedha ya kulipa mafao yake ya kustaafu.
Mzee Warioba sasa hivi yuko karibu sana na chadema kuliko CCM, yuko karibu sana na mwenyekiti wa chadema kuliko mwenyekiti wa CCM.
Kwanini chama cha mapinduzi hakimjadili mwanachama kama huyu? Hii double standard inatokana na nini?. Kama Nchimbi kakosea kwanini Warioba hakosei?
Ni heri kuwa na pengo kuliko kuwa na jino bovu linalokuuma muda wote.