Mzee wa upako: Nchi itajengwa na wananchi wenyewe

MIMI BABA YENU

JF-Expert Member
Mar 1, 2019
295
679
Askofu wa Kanisa la Gospel Revival Center – Ubungo Kibangu Mchungaji Anthony Lusekelo, Mzee wa Upako (Chifu Mwantembe) amewataka watanzania kuendelea kuiunga serikali mkono katika ulipaji wa kodi (Tozo) uliotukuka ili kuweza kujenga taifa lenye uchumi imara.


Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari leo Septemba 3, 2022 ofisini kwake Ubungo Kibangu, amesema swala la kulipa Tozo lipo toka zamani na hata katika vitabu vya dini limezungumzwa.

“watu wengi watakuwa wanajua maana ya Zaka na Zabihu, zilichukuliwa kwa wananchi ili kuendesha nchi yao, hivyo mambo ya kuchukua tozo yalianza kutoka mambo ya Torati, hamuwezi kuendesha nchi yenu bila kuchukua nguvu za wananchi wenyewe kwa kuendesha taifa lenu na mambo ya ibada” alisema Mzee wa Upako.

Mzee wa upako ameeleza kuwa, katika vitabu vya dini ulipaji wa kodi ulianza mnamo kipindi cha waisraeli walipokuwa wakihitaji mfalme wao Sauli na kuambiwa wataendesha nchi yao kwa kutozwa kodi ili kuimarisha taifa lao.

Mzee wa Upake alihitimisha mazungumzo yake na wanahabari kwa kusema "Kulipa kodi ni wajibu wakila Mwananchi katika kujenga Taifa, viongozi wetu wana nia ya dhati kabisa katika taifa hili, hivyo ni wajibu wetu sote kulipa Tozo na Kodi ili kujiletea maendeleo"
 
Siku nao wakibana matumizi yao, wakomeshe wizi wa pesa za umma na kupatiwa majawabu report za CAG watu hawawezi kulalamika ila kwa mwenye akili timam umlazimishe tozo huku kila akisoma habari lazima akute upigaji mahali sasa moyo wa kulipa hizo tozo utatoka wap
 
Tatizo no pale maendeleo ya taifa hayaendani na wingi wa tozo tunazolipa.
 
Askofu wa Kanisa la Gospel Revival Center – Ubungo Kibangu Mchungaji Anthony Lusekelo, Mzee wa Upako (Chifu Mwantembe) amewataka watanzania kuendelea kuiunga serikali mkono katika ulipaji wa kodi (Tozo) uliotukuka ili kuweza kujenga taifa lenye uchumi imara.


Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari leo Septemba 3, 2022 ofisini kwake Ubungo Kibangu, amesema swala la kulipa Tozo lipo toka zamani na hata katika vitabu vya dini limezungumzwa.

“watu wengi watakuwa wanajua maana ya Zaka na Zabihu, zilichukuliwa kwa wananchi ili kuendesha nchi yao, hivyo mambo ya kuchukua tozo yalianza kutoka mambo ya Torati, hamuwezi kuendesha nchi yenu bila kuchukua nguvu za wananchi wenyewe kwa kuendesha taifa lenu na mambo ya ibada” alisema Mzee wa Upako.

Mzee wa upako ameeleza kuwa, katika vitabu vya dini ulipaji wa kodi ulianza mnamo kipindi cha waisraeli walipokuwa wakihitaji mfalme wao Sauli na kuambiwa wataendesha nchi yao kwa kutozwa kodi ili kuimarisha taifa lao.

Mzee wa Upake alihitimisha mazungumzo yake na wanahabari kwa kusema "Kulipa kodi ni wajibu wakila Mwananchi katika kujenga Taifa, viongozi wetu wana nia ya dhati kabisa katika taifa hili, hivyo ni wajibu wetu sote kulipa Tozo na Kodi ili kujiletea maendeleo"View attachment 2344610
WEWE UNALIPIWA TOZO ALTARENI
 
Hawa ndio wale waliosetiwa kuanza kuzipamba tozo kwa manufaa ya serikali.

Ngoja hao waumini wenu wakose sadaka za kuwatolea kwenye vijiwe vyenu ndio mtapata akili.
 
tuwaulize waumini wake, wamemwelewaje mchungaji wao???. Na sidhani kama ameelewa wananchi wanachokilalamikia?? angeelewa angezungumza vizuri na angesaidia kumshauri rais namna njema ya kuishi na wananchi masikini kama waumini wa huyu Mchungaji. Waumini wakija kanisani kwake wanakua wanajitahidi kufua nguo zao na kujiweka vizuri ili waonekane wana maisha mazuri ila uhalisia ni tofauti. Waumini wanapitia wakati mgumu sana sema hakuna mahali pa kuelezea maumivu yao.
 
Askofu wa Kanisa la Gospel Revival Center – Ubungo Kibangu Mchungaji Anthony Lusekelo, Mzee wa Upako (Chifu Mwantembe) amewataka watanzania kuendelea kuiunga serikali mkono katika ulipaji wa kodi (Tozo) uliotukuka ili kuweza kujenga taifa lenye uchumi imara.


Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari leo Septemba 3, 2022 ofisini kwake Ubungo Kibangu, amesema swala la kulipa Tozo lipo toka zamani na hata katika vitabu vya dini limezungumzwa.

“watu wengi watakuwa wanajua maana ya Zaka na Zabihu, zilichukuliwa kwa wananchi ili kuendesha nchi yao, hivyo mambo ya kuchukua tozo yalianza kutoka mambo ya Torati, hamuwezi kuendesha nchi yenu bila kuchukua nguvu za wananchi wenyewe kwa kuendesha taifa lenu na mambo ya ibada” alisema Mzee wa Upako.

Mzee wa upako ameeleza kuwa, katika vitabu vya dini ulipaji wa kodi ulianza mnamo kipindi cha waisraeli walipokuwa wakihitaji mfalme wao Sauli na kuambiwa wataendesha nchi yao kwa kutozwa kodi ili kuimarisha taifa lao.

Mzee wa Upake alihitimisha mazungumzo yake na wanahabari kwa kusema "Kulipa kodi ni wajibu wakila Mwananchi katika kujenga Taifa, viongozi wetu wana nia ya dhati kabisa katika taifa hili, hivyo ni wajibu wetu sote kulipa Tozo na Kodi ili kujiletea maendeleo"View attachment 2344610
Sahihi kabisa. Asante mzee wa Upako.🙏🙏🙏
 
Haiwezekani Mafao nayo yakatwe Tozo.
Hili sio haki kabisa nilipunguzwa kazi 2020 mpaka hii leo sijapata kazi nyingine.
Na mafao yangu nilifuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote ila kuna njia yangu niliitumia nashukuru nilifakiwa kulipwa na cha kushangaza ninachoambulia ni Tozo zinaning'inia ktk statement yangu ya kibenki.
 
Huyo mchungaji alichozungumza ni kinyume na matakwa ya waumini wake, ngoja aone kanisa tupu ndipo atatengea kauli yake hiyo.. au kwa sababu yeye anapata vya bure? Hapo hajatumia akili kabisa
 
Mwigulu atangaze kesho kodi makanisani usikie moto wa mzee wa bapa. Kodi ya wazi kabisa hiyo halafu mwigulu anakimbizana na tozo tozo.
 
Kiwango siyo tatizo, shida ni tozo inatumikaje? Makusanyo ya mwezi moja tuu kupitia tozo inatosha kuonesha tofauti ya maendeleo ktk nchi lakini hatuoni kitu.

Ni kweli matumwizi yamekuwa hovyo.mara ujenzi wa Ikulu Zanzibar mara manunuzi ya maV8.
 
Chapombe huyu apuuzwe tu
😂 😂 😂 😂 😂😂
'Zakayo' mtoza Ushuru alirudisha alichowadhulumu wananchi baada ya kutembelewa na Yesu. Hivi huyu mla sadaka anaongozwa na nani ? Roho mtakavitu?

1662286497449.png
 
Back
Top Bottom