Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mzee Exavery Mgavilwa (71) maarufu kwa jina la Boy Safi ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ninga halmashauri ya Wilaya ya Njombe ameiangukia serikali akiomba kufikishiwa nishati ya umeme nyumbani kwake akidai kuwa hataki kufa bila kuona umeme ukiwaka kwenye nyumba yake.
Mzee Mgavilwa ameeleza hayo wakati akitoa kero zake kwa Mbunge wa Jimbo la Lupembe Wakili Edwirn Swalle alipokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji hicho ambapo amesema mpaka sasa watoto wake wamekuwa wakihangaika bila mafanikio.
"Hatuna umeme kabisa, vijana wangu wamekuwa wakijaribu kupiga kelele na diwani lakini na yeye anajitetea anasema sio mimi, mnataka nife bila kupata umeme? Swalle nilikuchagua mwenyewe", amesema mzee Mgavilwa
Mzee Mgavilwa ameeleza hayo wakati akitoa kero zake kwa Mbunge wa Jimbo la Lupembe Wakili Edwirn Swalle alipokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji hicho ambapo amesema mpaka sasa watoto wake wamekuwa wakihangaika bila mafanikio.
"Hatuna umeme kabisa, vijana wangu wamekuwa wakijaribu kupiga kelele na diwani lakini na yeye anajitetea anasema sio mimi, mnataka nife bila kupata umeme? Swalle nilikuchagua mwenyewe", amesema mzee Mgavilwa