Mzee Tryphon Maji Amefariki Dunia

Pole sana wafiwa.

Nakumbuka Mtoto wake mmoja tulikuwa kombania moja naye pale JKT alifariki kwa kuungua kwa moto.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.Nakumbuka majonzi yaliyotupata wakati mtoto wake alipokufa moto JKT.Ni wakati enzi zile anaishi chole road.

rest in peace.
 
operesheni kambarage?

ndiyo ilikuwa operesheni kambarage ruvu jkt kombania f ya kamanda mwambingu. Abuu maji alikufa kwa moto wakati huo baba yake alikuwa tayari kamtafutia chuo marekani na ilibaki siku mbili kuondoka nchini. Kumbuka abuu alikufa siku ya mwisho ya kumaliza jkt
 
Ahhh nani atasahau enzi zile za STESHENI na ile CHAI MAHARAGE ILIYOKUWA IKIENDA masaki IKIITWA kabibiiii?

maana hata akina Alfa na CHICAGO BULLS walikuwa hawaoni ndani na akina NIKAS na ule mbasi wao ndio kabisaaa

KABIBIII ilikuwa inapita traffic za salenda briji kisa? Gari la TRYPHON MAJI!

Bullet train (BOMBASTIC SOUND) enzi hizi tulikuwa bado tunasoma vijisekondari vya Bongo. Namkumbuka Mzee MAJI ambapo kuna mwanae mmoja alikuwa anasoma Jitegemee pale kama sikosei. Alikuwavurugu sana dogo yule.

Mungu awafariji wafiwa.
 

... kuna mwanae mmoja alikuwa anasoma Jitegemee pale kama sikosei. Alikuwavurugu sana dogo yule.

Mungu awafariji wafiwa.

Mnafiki mkubwa!

Hao wafiwa unaosema wafarijiwe ndio huyo huyo unaesema aliwavuruga sana dogo. Familia itafarijika na maneno hayo? Ukishaamua kula nguruwe bana kula aliyenona, usiume na kupuliza.

Wafiwa poleni.
 
Jamani marehemu hata hajazikwa, it is disrespectful to speak the truth about the dead.

Mungu alitoa, Mungu ametwaa. Mungu kwa nini unatuchezea chezea kutoa na kuchukua? Lakini kazi yako haina makosa. Familia, ndugu na marafiki, poleni sana.

Amina.

Unatamka kwa uhakika kabisa kuwa "kazi ya Mungu haina makosa," halafu hapo hapo unahoji kwa nini Mungu anawachezea chezea wanadamu kwa kutoa na kuchukua. Which is which?
 
If he cared about the family your good Allah would not have allowed him to die in the first place, let alone need you to beg him or remind him about the difficulty the family is going thru. He would know, he's God the merciful!
Jiandae your day is there...!
 
Jamani marehemu hata hajazikwa, it is disrespectful to speak the truth about the dead.

Mungu alitoa, Mungu ametwaa. Mungu kwa nini unatuchezea chezea kutoa na kuchukua? Lakini kazi yako haina makosa. Familia, ndugu na marafiki, poleni sana.

Amina.
Duh...!
 
Rest in Peace mzee Maji!

Frank, Mwamba(Moses), Dastan(Tunu), Kaizer na Tiba(Antonia),mwenyezi mungu awape nguvu kipindi hiki kigumu. Sorry for the loss of your pillar...

Jirani yenu Mwembe Tayari-Mbezi
 
Last edited by a moderator:
Poleni wafiwa!Wenye picha ya Marehemu mzee Maji tunaomba muiweke tumwone maana hili lilikuwa jina maarufu miaka ya tisini.

dah ni kweli kabisa ndugu yangu kamuna huyu mzee alikua maaarufu sana miaka ile japokua tulikua wadogo lakini jina lake lilikua maarufu katika viunga vya darisalama. My condolences to the family
 
Ninasikitika kwa habari za kifo cha ndugu maji. Mungu ailaze rohoyake mahali pema peponi.Hata sahaulika milele kwa utumishi wake uliokuwa bora
 
Mungu Ailaze Roho Ya Marehemu Mahala Pema Peponi

Poleni Kaizer, Dastan na ndugu wengine wote.
 
hivi ni yule aliyekuwa mkuu wa fieldforce Ukonga baada ya Tossi au...mwenye details naomba msaada please.Nawapa pole wafiwa
 
Back
Top Bottom