Ileile hamahama ya EL na vijana wake imeleta shida kubwa sana CDM.. wakati EL anahama na vijana wake ilikuwa nafasi nzuri pia kwa CCM kupenyeza watu wake..
Vyama vya upinzani vitengeneze mifumo imara yakudhibiti mapandikizi kwenye nafasi nyeti ili kupunguza madhara nyakati za mafuriko..
Mbowe, Mnyika, Lissu, ZZK, Maalim Seif, Jussa, Babu duni mpaka sasa hawa ndio wapinzani pekee wasiowaza maslahi binafsi wala kuwa na tamaa..
Hizi siasa za kibongo zimejaa wasaka fursa, watafuta vyeo, na wanaowaza maslahi binafsi na tusipokuwa makini kila siku upinzani utaanza upya...