kipindi kile Tanzania ina chuo kikuu kimoja tu (UDSM) kikiwa na campus tatu mlimani(main),morogoro (kilimo,siku hizi SUA) na muhimbili(udaktari,siku hizi Muhas).Kote huko mzee Punch alikuwa anatamba though main campus ndo yalikuwa makazi yake zaidi.IFM ,cbe vilikuwa vinaandaa watu wa kuja kuchukua Bcomm baadae mlimani au kufanya CPA,mzee Punch alikuwa harushi makombora huko.Kipindi hicho mlimani chumba tunalala watu wawili wawili tu,imagine Hall six mchumba ule ulivyokuwa mkubwa.Kuna kitu kilikuwa kinaitwa kupigwa exile,yaani mate wako analeta mwanamke(au mwanamke analeta mwanaume hall three) na wewe unakwenda kulala
hukooooo!!!!
naamini humu jf kutakuwa na mamemba ambao washawahi kuwa ma Punch.Waje hapa watujuze kwa nini walikuwa wanadhalilisha wenzao.