under_score
Senior Member
- Nov 2, 2011
- 190
- 45
Habari za jumapili Wakuu?
Nakumbuka ingekuwa nimalize masomo yangu ya shahada ya kwanza (B.com) pale chuo kikuu cha Darisalama mnamo miaka ya late 90's hivi, yaani almost 15 years back, lakini sasa ilinibidi nikache zangu "UD" tu nrudi kijijini kwetu ibiri nikalime tumbaku!
Sasa mnajua ilikuwaje wana ? Leo hii, yaani usiku wa jana kuamkia leo, nimeota marudio ya picha moja flani hivi la ukweli, ambalo imebidi nkutupieni hapa jamvini tu ili nipate ku'share na ma'experiences yenu kama vipi!
Ilikua namna hii: Nakumbuka siku moja niko na mshkaji wangu wa kitambo iyo (R.I.P my friend) tunakatiza zetu Academic Bridge (sijui lile daraja linaitwaje siku hizi) kitu ngoma 9 hivi za usiku ka kawaida tunatoka zetu kupiga "msuli" kuelekea mabwenini kulala, enzi hizo nakumbuka mi nlikua nalala Hall-5 ghorofa ya 11 (siku hizi naskia Hall-5 ni la wanawake tupu, sa sjui ni kweli?) afu mshkaji wangu ye alikuwa Hall 2 ghorofa ya 8 hivi kama sikosei!
Sasa wana picha lilianza kunoga tulipofika pale maeneo ya Rev. Square (siku hizi sijui patakua panaitwaje), kwa pembeni yake hivi kulia palikuwa na Cafeteria enzi hizo (sa sijui kama pashageuzwa ni darasa labda siku hizi) tukakuta ma "black-ninjas", mtu kama 7 hivi zimetengeneza kitu kama pyramid kuelekea juu kwenye roof ya hilo jengo la Cafeteria, ambapo kimsingi ndo ilikuwaga "Billboard" ya machapisho ya Mzee Punch wa enzi hizo!
Mwanangu asikwambie mtu, kwa ile namna jamaa walivosambaratika kwa kasi ya ajabu kutoka pale mahali spati picha lake, manake mi nliona chenga tu, na kilichofuatia ni kwamba na sisi tuligawana njia tukala zetu kona mbaya kabisa kila mtu na njia yake kachala nlijikuta niko Mabibo hostel, na msela wangu akaibukia from Mwenge hostel iyo asubuhi yake, make duh!! enzi hizo hata simu za mikononi ilikuwa hakunaga mwana!
Sasa niulize mwisho picha lilikuwaje, ile kufika tu Mabibo hostel kwenye room ya mshkaji wangu mngine ili nimgongee nipate japo hifadhi kwa masaa yale machache ya usiku yaliyobakia nakutana na ile "chata" ya danger (fuvu la kichwa cha mtu + ile mifupa miwili iliyopigwa cross kwa nyuma yake) imebandikwa mlangoni kwa jamaa, with words in RED: Mzee Punch is every where; Mzee Punch is incognito; when you see Mzee Punch you see Death, etc etc etc!
Na sasa kitu ilonchanganya zaidi ni kwamba picha lilikuwa ni hilo hilo na kwa yule mchizi wangu alokimbilia Mwenge hostel alipofika kutaka kugonga mlango wa room ya jamaa, sasa swali huwa najiuliza mpaka kesho, who was that "Mzee" for real, ni kundi la wale maninja tulowaona, ama wale ni manyoka tu wa "Mzee", ama huyo Mzee alikuwa ni jini, ni Shetani ama li kitu'kitu gani haswa!! Kwanza alijuaje in-advance kwamba ni wapi tunakimbilia for us to find the warning remarks waiting for us, kila mmoja kwa wakati wake na kwa mahali alipokimbilia katika ile hali ya kuchanganyikiwa ....
Nakumbuka ingekuwa nimalize masomo yangu ya shahada ya kwanza (B.com) pale chuo kikuu cha Darisalama mnamo miaka ya late 90's hivi, yaani almost 15 years back, lakini sasa ilinibidi nikache zangu "UD" tu nrudi kijijini kwetu ibiri nikalime tumbaku!
Sasa mnajua ilikuwaje wana ? Leo hii, yaani usiku wa jana kuamkia leo, nimeota marudio ya picha moja flani hivi la ukweli, ambalo imebidi nkutupieni hapa jamvini tu ili nipate ku'share na ma'experiences yenu kama vipi!
Ilikua namna hii: Nakumbuka siku moja niko na mshkaji wangu wa kitambo iyo (R.I.P my friend) tunakatiza zetu Academic Bridge (sijui lile daraja linaitwaje siku hizi) kitu ngoma 9 hivi za usiku ka kawaida tunatoka zetu kupiga "msuli" kuelekea mabwenini kulala, enzi hizo nakumbuka mi nlikua nalala Hall-5 ghorofa ya 11 (siku hizi naskia Hall-5 ni la wanawake tupu, sa sjui ni kweli?) afu mshkaji wangu ye alikuwa Hall 2 ghorofa ya 8 hivi kama sikosei!
Sasa wana picha lilianza kunoga tulipofika pale maeneo ya Rev. Square (siku hizi sijui patakua panaitwaje), kwa pembeni yake hivi kulia palikuwa na Cafeteria enzi hizo (sa sijui kama pashageuzwa ni darasa labda siku hizi) tukakuta ma "black-ninjas", mtu kama 7 hivi zimetengeneza kitu kama pyramid kuelekea juu kwenye roof ya hilo jengo la Cafeteria, ambapo kimsingi ndo ilikuwaga "Billboard" ya machapisho ya Mzee Punch wa enzi hizo!
Mwanangu asikwambie mtu, kwa ile namna jamaa walivosambaratika kwa kasi ya ajabu kutoka pale mahali spati picha lake, manake mi nliona chenga tu, na kilichofuatia ni kwamba na sisi tuligawana njia tukala zetu kona mbaya kabisa kila mtu na njia yake kachala nlijikuta niko Mabibo hostel, na msela wangu akaibukia from Mwenge hostel iyo asubuhi yake, make duh!! enzi hizo hata simu za mikononi ilikuwa hakunaga mwana!
Sasa niulize mwisho picha lilikuwaje, ile kufika tu Mabibo hostel kwenye room ya mshkaji wangu mngine ili nimgongee nipate japo hifadhi kwa masaa yale machache ya usiku yaliyobakia nakutana na ile "chata" ya danger (fuvu la kichwa cha mtu + ile mifupa miwili iliyopigwa cross kwa nyuma yake) imebandikwa mlangoni kwa jamaa, with words in RED: Mzee Punch is every where; Mzee Punch is incognito; when you see Mzee Punch you see Death, etc etc etc!
Na sasa kitu ilonchanganya zaidi ni kwamba picha lilikuwa ni hilo hilo na kwa yule mchizi wangu alokimbilia Mwenge hostel alipofika kutaka kugonga mlango wa room ya jamaa, sasa swali huwa najiuliza mpaka kesho, who was that "Mzee" for real, ni kundi la wale maninja tulowaona, ama wale ni manyoka tu wa "Mzee", ama huyo Mzee alikuwa ni jini, ni Shetani ama li kitu'kitu gani haswa!! Kwanza alijuaje in-advance kwamba ni wapi tunakimbilia for us to find the warning remarks waiting for us, kila mmoja kwa wakati wake na kwa mahali alipokimbilia katika ile hali ya kuchanganyikiwa ....