Mzee Mwanakijiji, Tafadhali...

hivi unamjua Mwanakijiji kweli mjomba ?
 
Character X CHADEMA wamejipangia mkakati gani wa kuweza kumdhibiti Lowassa ikitokea akashinda uchaguzi October? Watawezaje kumdhibiti ili asifanye yale wanayohofia kwamba yako ndani ya CCM?Ndio sasa hivi wanaweza kujipa moyo kwamba CHADEMA ndio kitakuwa chama tawala, ila ni kwa kiasi gani wao kama chama wataweza kupandikiza yale wanayotaka na kuamini? Bungeni wanaamini watapata majority ya wabunge lakini je, wataweza kuwa-controll wote? Maana wabunge watakaopatikana kwa influence ya Lowassa loyalty yao itakuwa kwa Lowassa na sio kwa CHADEMA. Hivyo wanaweza kuelekezwa popote pale atakapotaka Lowassa iwe ni sahihi kwa chama au la.

Tuwe wakweli kwa nafsi zetu, majuzi tu wengi wetu hapa tulikuwa na fikra za "Lowassa hafai, Lowassa hafai!" kwasababu alitangaza nia akiwa CCM, leo hii badhi mnadai kwamba "he is our only hope". Lowassa hajahamia CHADEMA kwasababu anaamini kwenye wanachofanya, kama asingekatwa CCM sasa hivi angekuwa anawapinga vikali mno. Yeye yuko pale kwasababu kuna opportunity ya yeye kupata anachokitaka SANA, urais, na sio kitu kingine chochote kile. Kila mtu anasema muhimu ni kung'oa mfumo uliopo, je mfumo huo huo mbovu ukipandikizwa CHADEMA instead? Maana mkulima ni yule yule (Lowassa) kilichobadilishwa ni shamba tu, na hata mbegu na majembe anakuja na yake (wafuasi na wagombea).

Wale ambao hawajalainishwa na dhana ya kuiondoa CCM madarakani kwa gharama yoyote ile kama Mzee Mwanakijiji na wengineo nawaelewa, tena sana maana kuna mengine mengi ya kuangalia baada ya Lowassa kuingia ikulu ikitokea ikawa hivyo. Kuiondoa CCM madarakani sio mwisho wa safari, ni mwanzo tu. Na kama hakuna mkakati madhubuti wa kuweza kum-CONTROL dereva(Lowassa) basi huo ushindi wa October utakuwa ni kazi bure kwa wote tunaotaka mabadiliko.

Binafsi sijaona ulazima wa CHADEMA/UKAWA kumsimamisha Lowassa kama mgombea wao wa urais eti kwamba itakuwa rahisi wao kushinda. Atashinda kwa kura gani? Za wafuasi wake na za UKAWA. Sasa kwanini asiwa-support kama mwanachama tu kwa kuwapa UKAWA kura za wafuasi wake ambazo zikiongezwa na zile za UKAWA zinaweza kutupa ushindi na akasimamishwa mtu ambae watu wengi watakuwa na imani nae? Kwanini ni lazima asimame yeye?

Wanachofanya CHADEMA sasa hivi ni kucheza kamari, tena kwa kuwekeza kila walichonacho. That will cost them dearly. Watacheza wakidhani wanashinda kwasababu wana karata nzuri kumbe mchangaji ameficha nyingine kiganjani na mwisho wa siku wanaweza wakashindwa na kupoteza kila kitu.
 
Last edited by a moderator:
GalaxS3 has a point but I do not see his proposed solution....rather he stimulates fear of remaining undecided/ neutral....

Propose a solution? Are you telling me Lowasa has been CDM solution all along? All those efforts and demonstrations and injuries and deaths have been for nothing? Have you been around for the last 5 years and witnessed the kind of accountability that a few opposition MPs were able to bring through the parliament? In this election absent of Lowasa, how many MPs do you think they stood to gain? They have a solution, the problem is they changed their mission to justfy accommodating Lowasa.
 
Mambo uliyoandika ni ya msingi sana ,nadhani wahusika watatafakari hususani kipindi hichi kigumu zaidi. Wanachadema wameuwa huko Arusha na kwingineko wakipigania haki na katika harakati za kuing'oa ccm leo hii tunashindwa kuwa kitu kimoja na kusonga mbele na mapambano!

Saa ya ukombozi ni sasa,tutumie nafasi hii kumwangamiza adai .
 

Ujinga ni mzingo! Asingekatwa Lowasa kwenye CCM, lengo lenu halikuwa limekamilika? Lazima mkubali kwamba nyie ni walafi wa fedha na ukanda! Bilioni kumi wamekunja viongozi wa chama na kuuza chama chenu. Hii ndo inampa Lowasa ujasiri wa kutokuvaa magwanga yenu na kusema anachojisikia
 

Rate ya 25 kwa 23 afu jua sample tu walichukuwa
 
Kama ni shimoni tumetumbukia wote mkuu, huu ni mtazamo wangu pia.
 
Last edited by a moderator:
Rate ya 25 kwa 23 afu jua sample tu walichukuwa

Mkuu bado hata huo utafiti wanaousema wao humu humu walidai jamaaa kahonga ili apambwe,kiukweli ni htar na bahati mbaya watu neutral hapa tunatukanwa tu,ila huu ndo ukweli,majibu ya mepesi yameendelea kutolewa kwa maswali magumu
 

Hate Never changes anybody for the better.. Love on the other hand is the power that transforms nations..

Time like this our motive is being tested.. On whether a motive towards national liberation or national segregation, and self righteousness?

If our motive in this movement is to instill hate and segregation and draw lines of who we think can be called "a patriot" and who should never be allowed to join the movement for change because we think "He was not there when we were building our party " our motive is perverted and we may need to reconsider that position.

Kama nilivyosema hakuna mwenye hati miliki yakuongoza Tanzania. Tanzania ni ya wa Tanzania na si ya familia flani .
Lakini kama hiyo nisawa, basi hakuna pia mwenye hati miliki ya Movement hiii... Hayupo!!!

Wala tusijizungumzie kama vile wale ni wao wachafu na sisi ni sisi wasafi hatuwezi kuungana hatakama indeed we have a common goal.

Mimi nadhani there is a big picture.. And you can see it if you wanna


Lakini all in all, point ya msingi kabisa kwa mzee mwaka Kijiji. Iwapo yote niliyoandika hapa yatasahaulika, ningetamani akumbuke ujumbe wangu kuwa ni huu

Wewe ni kiongozi. Watu wanakusikiliza, achakuwaongoza kugawanyika!!!!! Haitusaidii katika hatua yoyote ya movement hii.. And certainly not katika hatua kama hii..

Waweke watu pamoja, waongoze kufikia lengo kuu..

Comrade,
 

Why support/be a follower of Dr. Slaa while he has neither complained nor dissociated from the new corrupt leadership?
 

Hoja zako nzuri lakini ukweli ni kuwa CHADEMA baada ya mgogoro wa Zitto walikuwa wamedhoofika sana na sio ajabu wangepata kipigo kikubwa sana 2015.

Hata hivyo, kumkaribisha Lowassa ni sawa na mgonjwa mahututi mwenye maumivu makali kunywa dawa kusaidia kupunguza maumivu akijua wazi kuwa hiyo dawa pia ina madhara ya pembeni (side effects).

Cha kupima hapa ni kuangalia, je madhara ya pembeni ya hiyo dawa
(yaani rushwa) ni mapungufu kuliko maumivu ya kutokutumia hiyo dawa (kudhoofika kwa CDM).

Kwa maoni yangu ni kuwa, CHADEMA itabidi wamvumilie Lowassa na madhambi yake ili angalau awapitishe kwenye uchaguzi huu wakiwa katika afya njema (umaarufu), halafu baada ya hapo waangalie maisha baada ya uchaguzi 2015, aidha wakiwa wameshinda au wameshindwa uraisi.
 

Wakati nakubaliana na yote hayo, ila umesahau hulka ya binadamu. Siyo CCM wote wanapenda yanayoendelea wala siyo kuwa wote hawana uchungu na Tanzania. Ndiyo maana Lowassa ni muhimu sana, na inawauma. Sifa hizo ulizozitaja ilikuwa nazo KANU.
Kweli. Ni vizuri upinzani ujaribu kugeuza baadhi ya haya badala ya kuendelea kupeleka kesi ya ugomvi wa ndizi kwa nyani yule yule.
 

The thing about your Martin Luther Kinq's quote, they are so out of context and completely against you in this situation. Saying that Lowasa move to CDM is purely on his personal interest and ambitions [to become president]is not being self righteous or incite hate and segregation, is simply making a very open observation. Personally i have nothing against his ambition, but the point being made here is that lets call a spade a spade and this is one giant SPADE. There is no point denying it. Let me ask you this, the power that Lowasa exert is it proportional to his achievements as a government official throughout his 30+ years career? Just thing about it, i will wait.

So if its not from his achievements, then where does this massive fellowship and power come from? Are we allowed to at least question that before we jump onto the bus of praise and expectations? You keep bringing up that the bigger picture should be our focus, so let me ask which is this bigger picture you are talking about? Is the bigger picture to get rid of CCM or is it the bigger picture to have a prosperous Tanzania where everyone enjoy the fruits of this great nation? Which one is it? I think you are standing too close to a wall my friend, this struggle and hate on CCM [which is justified] is taking its toll. Take a step back, see which exactly is the bigger picture. Getting rid of CCM is just a stepping stone to an even harder job to realize the really bigger picture. A solid foundation needs to be in place otherwise you are just looking for trouble, and that foundation certainly can not come from this LowasaAndTeam union. The point here is, Lowasa is not coming alone, is coming with everything that makes him who he is. And he is not being helped here, he is the one offering help..that is in business is called negotiating from a position of power. POSITION OF POWER!

May you not be led astray after all the effort spent.
 


Asante Mzee Mwanakijiji kwa kuanda majibu ya hoja za wadau, labda niseme kabisa kuwa napenda sana CCM itoke madarakani kwa njia yoyote ile,
Mzee Mwanakijiji, katika majibu yako ningependa pia urudi nyuma kidogo na uuangalie huo umoja wa Katiba ya wananchi (Ukawa), nikiwa na maana kuwa CUF kama mshiriki wa Ukawa lakini pia yupo ndani ya Serikali inayopingwa na Ukawa (Serikali ya Umoja wa Kitaifa), sasa Chadema walikubali vipi kuwa pamoja na CUF ambao wako serikalini pamoja na CCM, kwa minajili ya kuwa la CUF ndio la CCM, na la CCM ndio la CUF, SIJAWAHI KUKUSIKIA/KUKUSOMA UKIPINGA MUUNGANO HUO WA CHADEMA NA CUF ndani ya Ukawa,
Nadhani kupinga kwako kwa Lowassa kuja Ukawa/Chadema kungeanzia na kupinga kwa CUF kuwa Ukawa,

pili, ningependa pia ujaribu kuelezea kwa kifupi tu, malengo hasa ya Vyama vya upinzani ni nini kwa hapa Tanzania?, ni kuikaripia na kuikosoa CCM au kuna mkakati wa kuitoa CCM kwenye Madaraka?, na kama malengo hasa ni kuitoa CCM madarakani ni njia gani hasa sahihi ya kufata?,

tatu, unaweza kuziainisha limitations zozote za vyama vya upinzani kuchukua watu kutoka CCM?, kwamba huyu achukuliwe na huyu aachwe?
 
Last edited by a moderator:
.
Hayo ni maoni yako na una haki ya kuyatoa. Ila siamini kama uko sahihi, sisi tunaona ni turufu mujarabu kushinda uchaguzi huu. CCM wanahaha kama haina madhara kwanini wanatapatapa. Big up kamanda Mbowe chadema tupo pamoja na wewe
Shetani ana tabia moja. Huwa ni muongo muongo. Yaani CCM wanahaha nini? Mbona ccm imetulia kabisa? Mi ni moja ya watu ninaokataa ujinga wa kuuza demokrasia kwa bil 10 leo wewe unatete. Mshenziii wewe na ujingaa wako. Unajua kabisa Lowassaa ni mwizi hata CCM alikataliwa tena mapema leo hii kwenu siyo mwizi. Tena mbowe kuna siku alihimiza Lowassa achomwe moto leo hii unatetea? We taahiraa. Ujua kuwa mi ni mpenda mageuzi sipendi kuona upinzani unakufa! Mbowe kaingia kingi ya marando na apson bila kujua. Time will tell wewe subiri na ujinga wako,
 


It is his power that you fear... I see.,

Well then.. Don't take it to the people, don't divide them. It doesn't help!!! That's my point..


Comrade,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…