Mwanasiasa mkongwe nchini, John Malecela, amevunja ukimya na kutangaza kuwa atagombea tena katika nafasi ya ubunge kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao na kulitetea jimbo lake.
Alisema hayo jana alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wilayani Chamwino juu ya watu ambao wamekuwa wakisema kuwa hafai kugombea tena kutokana na kuwa na umri mkubwa.
Malecela alisema kuwa wananchi wake bado wanamuhitaji kwa hiyo hawezi kuacha kugombea kutokana na maneno ya watu kuwa yeye hana sifa ya kuwa mgombea tena bila kujali kuwa wananchi wanataka nini.
Alisema hata kama hatagombea bado ataendelea kuheshimika kwani amewafanyia wananchi wake mambo makubwa na kutekeleza ilani ya chama kwa asilimia kubwa lakini hawezi kuacha wakati wakiwa bado wanamuhitaji aendelee kuwafanyia yale yalio salia.
Ninyi wenyewe mashahidi mmewasikia wananchi wanavyosema kuwa bado wananihitaji kwa hiyo siwezi kuacha wakiwa bado wana mapenzi na mimi kiongozi wao, alisema Mwanasiasa huyo mkongwe.
Akijibu swali la waandishi wa habari waliotaka kujua kwa nini haigi mfano wa wazee wenzake walioamua kuacha kugombea kama Paul Kimiti, Malecela alisema, Mimi ni Malecela na kimiti ni Kimiti kwa hiyo siwezi kuiga kitu ambacho hakiko moyoni mwangu mwenyewe wametangaza hivyo na mimi natangaza kuwa nagombea.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Unajua mie siwaelewi hawa viongozi wa Afrika??? Wanataka kufia katika kiti cha uongozi.
Nikimquote jamaa anadai "Ninyi wenyewe mashahidi mmewasikia wananchi wanavyosema kuwa bado wananihitaji kwa hiyo siwezi kuacha wakiwa bado wana mapenzi na mimi kiongozi wao, Hivi unadhani wananchi watasema hawamuhitaji wakati jamaa hawapishi wenzie wakaongoza???
Jamaa anakaa madarakani hadi anakongoroka utafikiri ni ufalme. Mabadiliko hayaletwi na kiongozi aliyekaa muda mrefu kwasababu hana benchmark ya kuibeat but instead anatawala kama vile amezaliwa na cheo hicho. Kiongozi mpya akija huwa anatazama mwenzie amefanya nini ili na yeye aweze kuyapiku malengo ya mwenzie aliyepita. Sasa malecela anapredecessor gani anayejicompare naye.
Jamaa anataka madaraka hadi siku atakapokufa !!!!!
Alisema hayo jana alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wilayani Chamwino juu ya watu ambao wamekuwa wakisema kuwa hafai kugombea tena kutokana na kuwa na umri mkubwa.
Malecela alisema kuwa wananchi wake bado wanamuhitaji kwa hiyo hawezi kuacha kugombea kutokana na maneno ya watu kuwa yeye hana sifa ya kuwa mgombea tena bila kujali kuwa wananchi wanataka nini.
Alisema hata kama hatagombea bado ataendelea kuheshimika kwani amewafanyia wananchi wake mambo makubwa na kutekeleza ilani ya chama kwa asilimia kubwa lakini hawezi kuacha wakati wakiwa bado wanamuhitaji aendelee kuwafanyia yale yalio salia.
Ninyi wenyewe mashahidi mmewasikia wananchi wanavyosema kuwa bado wananihitaji kwa hiyo siwezi kuacha wakiwa bado wana mapenzi na mimi kiongozi wao, alisema Mwanasiasa huyo mkongwe.
Akijibu swali la waandishi wa habari waliotaka kujua kwa nini haigi mfano wa wazee wenzake walioamua kuacha kugombea kama Paul Kimiti, Malecela alisema, Mimi ni Malecela na kimiti ni Kimiti kwa hiyo siwezi kuiga kitu ambacho hakiko moyoni mwangu mwenyewe wametangaza hivyo na mimi natangaza kuwa nagombea.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Unajua mie siwaelewi hawa viongozi wa Afrika??? Wanataka kufia katika kiti cha uongozi.
Nikimquote jamaa anadai "Ninyi wenyewe mashahidi mmewasikia wananchi wanavyosema kuwa bado wananihitaji kwa hiyo siwezi kuacha wakiwa bado wana mapenzi na mimi kiongozi wao, Hivi unadhani wananchi watasema hawamuhitaji wakati jamaa hawapishi wenzie wakaongoza???
Jamaa anakaa madarakani hadi anakongoroka utafikiri ni ufalme. Mabadiliko hayaletwi na kiongozi aliyekaa muda mrefu kwasababu hana benchmark ya kuibeat but instead anatawala kama vile amezaliwa na cheo hicho. Kiongozi mpya akija huwa anatazama mwenzie amefanya nini ili na yeye aweze kuyapiku malengo ya mwenzie aliyepita. Sasa malecela anapredecessor gani anayejicompare naye.
Jamaa anataka madaraka hadi siku atakapokufa !!!!!