Mzee Makamba aibua siri ya Urais 2015

Hivi kwani Mzee Makamba ana umri gani? Kwa mtazamo wangu alifanya kazi nzuri sana kama Katibu Mkuu wa CCM kuliko Mzee wetu Mukama wa sasa hivi. Tena ukisema kwa hoja zinazoenda na wakati, naweza bado nikamtetea Mzee Makamba kuliko Mzee Mukama.

Mimi naona hajaongea kumpinga JK, ametoa mtazamo wake wa siasa zilivyo. ni dhahiri kwamba kichini chini wana-CCM wote nchi nzima wanalalamika na hali ya nchi ilivyo na chama chao, lakini wanalinda nidhamu ya kumhehimu Mwenyekiti wao waliyemchagua wao wenyewe, Mpendwa wetu Jakaya Kikwete. Lakini ni dhahiri kwamba watakapolazimishwa kuchagua mtu, basi nidhamu itapotea. Kwani hata Mkapa hakumbeba Jakaya, kwahiyo siamini Jakaya ana mpango wa kumbeba mgombea yoyote yule.

Naamini ujumbe wa Mzee Makamba ni kwamba yoyote anayefikiria kugombea kupitia ticket ya CCM, assijipange kwa siasa za kutegemea kubebwa na Jk, bali ajenge hoja zake na watu wampime kwa mabaya na mazuri yake.

Kwa kumalizia, hivi kama tunajenga hoja ya Zitto kuwa Rais wa nchi hii mwaka 2015, tena kama private candidate, kwanini isiwe JANUARY MAKAMBA? Nawasilisha.

Kazi gani nzuri alofanya? Kwa kuiua CCM? Labda hiyo.... Wewe ni mmoja wa familia hiyo umejidhihirisha mwishoni eti JM..thee tehh eteh ndio maana mzee ameanza kutabiri ili atakaye teuliwa na CCM aambiwe waende Tanga akaoneshwe nguvu za giza na amuombe ampe kazi JM huyo unayemtaka awe rais.. kazi kweli kweli....teh theheh
 
Makamba kwa nini asiwe kama Masishanga aliyetoka hadharani kumuunga mkono Sumaye,kuliko kujificha kwenye vivuli vya kpiga ramli.?
 
Mbona ni mapema mno kuzungumzia uraisi na mbona haikuwa hivi kwa mtangulizi wake.

Hii inaonesha ni jinsi gani watu wanavyowaza kujinufaisha na si kuwanufaisha wananchi na kama tabia hii haitakomeshwa taifa litaingia vitani kwa faida ya wachache huku waliowengi wasijue kinachogombaniwa.

Kama kanisa litaibuka kama ilivyokuwa 2005 na kusema ni chaguo la mungu je wananchi tutasemaje? Maana Chaguo la Mungu kwa maana yao ndo mwendo huu na wanaridhika nao maana walisema ni chaguo la Mungu.

Ndo maana nasema kwa mtindo huu tutapiganishwa kupitia misaada tunayopewa na hawa wanaokuwa baadae kuwa chaguo la mungu ili kufanikisha matakwa ya nafsi zao na jamaa zao.

Pia ni vizuri kujiuliza kanisa linaajenda gani na utawala? Maana huwa linatoa miongozo,matamko na hata maelekelezo juu ya nini kifanyike au ndo hisani ya kutoka kwa chaguo la mungu?
 
Kwani Mungu anapiga kura?

Mimi sijui kwa nini siku za karibuni nikajaribu kuingia kwenye Post zenye heading ya Mungu sipati access? Good Question Mwanakijiji. sababu the other day tuliambiwa so and so ni chaguo la Mungu? does He Vote? Good Question bother.
 
Mimi sijui kwa nini siku za karibuni nikajaribu kuingia kwenye Post zenye heading ya Mungu sipati access? Good Question Mwanakijiji. sababu the other day tuliambiwa so and so ni chaguo la Mungu? does He Vote? Good Question bother.

Inategemea wewe muhusika mwenyewe kuwa, je una amini Mungu yuko, je una dini? dini yako ni ipi? mimi nina dini na katika dini yangu viongozi wote wananapata mamlaka ya kutawala kwa kibali cha Mungu. Mungu akitaka kuwatia adabu nyie kama taifa kwa dhambi zenu ndio atampa kibali asiyekidhi matarajio yenu vinginevyo mtampata anaye kidhi mliyo ya tarajia. wale waliosema ni chaguo la Mungu hawaja kosea hata kidogo kwa mujibu wa imani yangu mie. ila kwa haya maoni ya mzee makamba sikujua kuwa yeye ana kipaji cha utabiri pia.
 
Nani mwenye taarifa za huyu mzee Makamba kuhusu ile Pembe iliyokua kwenye paji la uso kama bado inaendelea kuota atuambie!
 
Inategemea wewe muhusika mwenyewe kuwa, je una amini Mungu yuko, je una dini? dini yako ni ipi? mimi nina dini na katika dini yangu viongozi wote wananapata mamlaka ya kutawala kwa kibali cha Mungu. Mungu akitaka kuwatia adabu nyie kama taifa kwa dhambi zenu ndio atampa kibali asiyekidhi matarajio yenu vinginevyo mtampata anaye kidhi mliyo ya tarajia. wale waliosema ni chaguo la Mungu hawaja kosea hata kidogo kwa mujibu wa imani yangu mie. ila kwa haya maoni ya mzee makamba sikujua kuwa yeye ana kipaji cha utabiri pia.

Kama kweli Mungu ndio anavote in, na ni kweli ameshiriki kuvote in yeyote kati ya Marais wote waliopita, na Marais wengine popote pale duniani, basi na He is a failed god. Lakini as much as I know him, hausiki na huu uchafu unaoendelea hapa. we are responsible for it and the other god we have chosen to save.
 
Mungu hachagui Rais ingekuwa ndiye anaechagua asingetupa hili janga!!

kabisaa!! Mungu anaona maisha ya baadae so kama alijua hii nchi ingekua hivi tulivyo sasa angetupa Rais mwingine ambae ni bora na ana uongozi bora mwaka 2010
 
Definition mpya ya KUJIVUA GAMBA....
CCM bana..

Alisema lengo la kujivua gamba halikuwa likiwalenga baadhi ya wanasiasa wachache ndani ya Chama cha Mapinduzi wanaotuhumiwa kwa ufisadi bali ililenga kuwaondoa watu walioonekana kukaa kwa muda mrefu katika safu za uongozi ndani ya chama na kuleta damu changa ili nao waje waongoze wakiwa na mbinu mpya.
 
Kama kweli Mungu ndio anavote in, na ni kweli ameshiriki kuvote in yeyote kati ya Marais wote waliopita, na Marais wengine popote pale duniani, basi na He is a failed god. Lakini as much as I know him, hausiki na huu uchafu unaoendelea hapa. we are responsible for it and the other god we have chosen to save.

Umenifurahisha kwa 1. umeliandika neno Mungu (tofauti na god) kama mimi 2. umekubaliana na mimi bila kunielewa na bila kujua. ni fafanue kidogo labda utanielewa na utaendelea kukubaliana nami. kuwa watu wote tumeumbwa na Mungu kwa mujibu wa imani ya dini yangu. Mungu atampa kibali mtu wa kutuongoza kutokana na majority tunavyo wajibika au tusivyowajibika kwake. kama tunawajibika kwa shetani atampa kibali mtu anayewajibika kwa shetani ili kututia adabu.sasa ni wajibu wa wanaotawaliwa kuomba hekima ya Mungu huyohuyo iliwajue mamlaka inayotawala inamtii shetani au Mungu kwa kuangalia matendo yao wenyewe naya wa watawala wao halafu wachukue hatua. bahati mbaya masuala yanayo husu kumtii na kumuomba Mungu hayana spoon feeding ni juhudi za mtu mmoja mmoja na kwa mambo mengine kama taifa.
 
Mhe Mbopo, salam aleikum. Hivi ni wewe tuliokusoma kwenye gazeti la RAI le?. Najua utasema ni gazeti la MAFISADI, kama ambavyo RAIAMWEMA lilivyo gazeti la WAADILIFU, kama ulivyoelezea makundi yako wewe ya CCM.

Naona unaongea kama MAMLAKA kabisa. Lowassa anautaka sana urais lakini HATAKUWA RAIS .
Hivi wewe ni MUNGU? Maana yake hata Rais Kikwete hana mamlaka ya kusema hivyo, basi na mimi najitwisha mamlaka hayo hayo, nasema BERNARD MEMBE HATAKUWA RAIS NA WALA HATA MKUU WA WILAYA KWENYE SERIKALI INAYOFUATA. Ameeeeen.

Hata ukikasirika, ukweli unabaki pale pale na hata yeye mwenyewe moyoni mwake anajua hivyo. The good news ni kwamba Membe anastaafu siasa in 2015 na hahitaji uteuzi wa yeyote yule.
 
Alisema lengo la kujivua gamba halikuwa likiwalenga baadhi ya wanasiasa wachache ndani ya Chama cha Mapinduzi wanaotuhumiwa kwa ufisadi bali ililenga kuwaondoa watu walioonekana kukaa kwa muda mrefu katika safu za uongozi ndani ya chama na kuleta damu changa ili nao waje waongoze wakiwa na mbinu mpya.

Alisema dhana hiyo imepotoshwa na wale wanaoitekeleza wanaitekeleza kwa malengo tofauti.


hiyo kauli hapo juu ndo anapochekesha kwelikweli!!!!

ha ha haaaa!!!muongo utamjua tu. huyu mzee ndo walewale tu wenye dhambi ya kula nyama ya mtu. hana jipya, angepumzika tu anazidi kujidhalilisha bure.

hata Nyerere tuliyemwamini sana aliishia kutuchagulia FISADI Mkapa.
Rais tutaamua sisi wenyewe watanzania na sio huyu mzee anayeweweseka!!!!

Aggggggggrrrrrrrrrhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!
 
Makamba, JK,Nape, na baadhi wanaofanana nao kitabia ndo walioifikisha CCM hapo ilipo na kusaidia kuifikisha CDM hapa ilipo sitegemei leo hii Makamba awe na point za maana za kuongea kuhusu na Mstakari wa Chama chake na Taifa hili cha muhimu akae kimya ili angalau asahaulike asije ingizwa kwenye kashfa za ufisadi bure maana ndani ya CCM hakuna msafi
 
*Aonya mgombea atakayebebwa na Kikwete

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba amejitokeza hadharani kwa mara ya kwanza na kuzungumzia mustakabali wa taifa kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Makamba amekuwa kimya kwenye ulingo wa siasa, tangu alipoondolewa kwenye nafasi ya Ukatibu Mkuu ndani ya CCM alisema Watanzania waamini kuwa Mgombea urais 2015 atatoka kwa Mungu.

Makamba alisema amesikia kelele nyingi kuhusu nani akayemrithi Rais Jakaya Kikwete lakini pamoja na hayo yote atakayeamua hatma ya mgombea urais ni Mungu peke yake.

Mwanasiasa huyo machachari, anayesifika kwa kwa kutolea mifano maandiko ya kwenye vitabu vya biblia na quran, alikwenda mbali zaidi na kunukuu maandiko ya biblia akisema; “ Si kila mtu aniitae bwana bwana atakayeurithi ufalme wa mbinguni’ akiwa na maana kuwa si wote wanaoutaka urais watakuwa marais.

Akitolea mfano, Makamba alisema hata wakati Kanisa la Kiinjili ya Kiluteri Tanzania (KKT) wanamchagua Askofu Mkuu wao Maaskofu wawili waliokuwa wakigombea nafasi hiyo, Steven Munga wa Dayosisi ya Lushoto na Askofu Owdenberg Mdegella wa Dayosisi ya Iringa baada ya kupigiwa kura kwa takribani mara tatu walishindwa kumpata mgombea.

“Lakini aliibuka askofu mmoja akasema tuongeze jina la Alex Malasusa, jina la Malasusa lilipoongezwa tu walipopiga kura mara moja, Malasusa akapita, hivyo nataka kuwaambia kuwa mgombea urais 2015 atatoka kwa Mungu na atapatikana kwa staili kama aliyopatikana Malasusa…hivyo watu wasiwe na mashaka” alisema Makamba.

Baadhi ya wanasiasa wanaotajwa kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Waziri wa Afrika Mashariki, Bernad Membe.

Wengine ni Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani, John Nchimbi.

Alipoulizwa kati ya wanaotajwa kuwania kiti cha urais 2015 ni yupi ambaye anamuunga mkono, Makamba alisema ni mapema mno kuweka msimamo wake wazi.

Hata hivyo alisema muda ukifika na mchakato wa kuchukua fomu za kuwania urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi utakapoanza na baada ya wagombea kuchukua fomu ndipo atakapotangaza mgombea anayemuunga mkono.

Katika hilo, alisema mgombea atakayemuunga mkono yeye ana uhakika atapita na ndiye atakayeshinda urais 2015.

Makamba ambaye ni mwanasiasa machachari mwenye maneno mengi, akizungumzia hilo alikwenda mbali zaidi na kutahadharisha kuwa mgombea atakayeungwa mkono na Rais Jakaya Kikwete kugombea urais 2015 ataanguka.

Alisema mgombea atakayebebwa na Rais Kikwete yatampata kama yaliyompata Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002 alibebwa na Rais Daniel arap Moi awe mgombea wa KANU lakini matokeo yake chama kikamegeka na kusambaratika na Mwai Kibaki aliyekuwa akigombea kupitia chama cha Upinzani akaibuka mshindi kwa kura nyingi.

Uhuru ambaye ni mtoto wa Rais wa kwanza wa Kenya alichaguliwa kuingia bungeni mwaka 2001, na kuteuliwa kuwa Waziri wa Serikali za Mitaa chini ya utawala wa Rais Moi na pamoja na kwamba hakuwa na uzoefu mkubwa wa kisiasa Rais Moi alikuwa akitaka awe mrithi wake.

Mbali na hilo Kuhusu CCM na harakati zake za siasa kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2015, Makamba ambaye amepata kuwa kiongozi ndani ya CCM akianzia nafasi ya chini na kupanda hadi kushika nyadhifa za juu kabisa alisema ana uhakika chama hicho kitashinda.

Alipinga akisema kuwa chama hicho hakina makundi kama ambavyo baadhi ya watu wanatafsiri.

“Nimekaa CCM kwa muda mrefu sana…sijaona makundi yanayosemwa, ila kama ukisema pale ambapo wagombea wanachukua fomu za kuwania urais, hapo sawa makundi lazima yaibuke kwa sababu kila mmoja kuna mtu wake ambaye anaona anafaa kuwa rais” alisema Makamba.

Kuhusu dhana ya ‘kujivua gamba’ ndani ya CCM, Makamba alisema kauli hiyo imetafsiriwa vibaya na wale wanaoitekeleza.

Alisema lengo la kujivua gamba halikuwa likiwalenga baadhi ya wanasiasa wachache ndani ya Chama cha Mapinduzi wanaotuhumiwa kwa ufisadi bali ililenga kuwaondoa watu walioonekana kukaa kwa muda mrefu katika safu za uongozi ndani ya chama na kuleta damu changa ili nao waje waongoze wakiwa na mbinu mpya.

Alisema dhana hiyo imepotoshwa na wale wanaoitekeleza wanaitekeleza kwa malengo tofauti.


Source: Gazeti la Fahamu

Mukama, Chiligati na Msekwa nao ni damu changa...ccm kwa sarakasi wameshindikana ..wanasema wasiyoamini na kufanya wasiyosema.....kaburi li karibu msihangaike sana Mwenyezi Mungu atawapumzisha kwa amani
 
Huyu mzee makamba ni mnafiki kupita maelezo hapo anasema atamtaja atakayeshinda muda ukifika iliajipendekeze kwaa atakayeona ana nguvu ya kushinda si ataje sasa kama anaweza kubhashiri kwa unajimu wake, hana lolote anawaleta anapotosha mind tuu ili watu wajue JK ana mtu wake kati ya wanaotaka kuomba urais CCM wakati si kweli karibia wote ni wale walewale tuu,mwakyembe,sita,membe,lowasaa,nchimbi na yeye makamba wote walikuwa wanamtandao wa Jk sasa utofauti unatoka wapi usanii tuu hapo.

Rais bora wagombee kina magufuli ,mwandosya au kigoda watafanya kazi sio usanii tuu. na kina mzee makamba wanalijua hilo ndio maana hawawapi promo hawa...hao wanaotajwa kugombanani promo tuu hiyo wadanganyika fungukeni ukaelewa unavyosaniiwa

mwakyembe alikua timu mwandosya 2005
 
Hata ukikasirika, ukweli unabaki pale pale na hata yeye mwenyewe moyoni mwake anajua hivyo. The good news ni kwamba Membe anastaafu siasa in 2015 na hahitaji uteuzi wa yeyote yule.

membe atafanya nini akistaafu? phd ilki awe mwalimu au?
 
Tunahitaji hii axis of power ichukue nchi 2015...Mwandosya (Rais) Sitta, (Pm), Magufuli (ujenzi na uchukuzi hamna kutenganisha hivi vitu) Mwakyembe (ardhi na maendeleo mijini aweke sawa wizara ngumu hii) Sospeter aendelee na nishati, fedha ateuliwe utouh(hamna tena misamaha ya kodi kijinga jinga) Kilimo na elimu ni wizara muhimu Prof anajua vichwa vyake ataviweka hapo.... hii ni timu ya ushindi
 
Back
Top Bottom