Hivi jamani muambiwe mara ngapi msikie? Lowassa anautaka sana urais lakini HATAKUWA RAIS hata kama atakusanya vikongwe wote hawa i.e. Makamba, Kingunge, Bomani, Kisumo n.k. Yeye hana uwezo wa uchambuzi na ni lazima aelewe kwamba mazingira ya Kanu, Moi na Kenyatta ni toafuti na mazingira ya CCM, Kikwete na wagombea waliopo. Mbona chama hakikushindwa pale Mkapa alipomridhia Kikwete? Moi aliharibu pale alipozima jaribio la kidemokrasia la kupata mgombea wakati katika issue hii kanuni za Chama na mchakato wa uteuzi utazingatiwa. Hii mbinu ya Mzee Makamba, ambaye anajua kwamba mgombea wake hachaguliki na kudhani watamtisha Rais asitekeleze majukumu yake wakati wa uteuzi hazitafua dafu.
Makamba hana hata aibu, mwezi huu wa Ramadhan, kukanusha kwamba hakuna makundi wakati tulio nje tunajua kwamba kuna makundi mawili ndani ya chama. Kuna wale ambao ni walafi, wabinafsi, wahujumu rasilimali za nchi na wadumaza maendeleo kwa upande mmoja, na wale watetea haki za wanyonge, wapinga ufisadi na wapigania haki na walinzi wa rasilimali zetu kwa upande mmoja. Yeye ni mnufaika wa kundi la kwanza na ndiye gamba namba moja. Sasa anaibuka na kujifanya ni nabii, aende zake akaendeshe hotel yake aliyoijenga kwa fedha za ufisadi na hata kuhamishia fenicha za CCM huko!