Mzee Makamba aibua siri ya Urais 2015

Uyu Mzee ameiua ccm na sasa anatamani kuzikwa nayo....rais ataletwa na wapiga kura bwana Mungu tokalini akapiga kura? Ila bora yeye kasema Mungu waliotangulia wanasema wameoteshwa Tehe Tehe Tehe yeye apumzike Kama hakuiba za kumtosha nafasi Yake imepita
 
Hivi jamani muambiwe mara ngapi msikie? Lowassa anautaka sana urais lakini HATAKUWA RAIS hata kama atakusanya vikongwe wote hawa i.e. Makamba, Kingunge, Bomani, Kisumo n.k. Yeye hana uwezo wa uchambuzi na ni lazima aelewe kwamba mazingira ya Kanu, Moi na Kenyatta ni toafuti na mazingira ya CCM, Kikwete na wagombea waliopo. Mbona chama hakikushindwa pale Mkapa alipomridhia Kikwete? Moi aliharibu pale alipozima jaribio la kidemokrasia la kupata mgombea wakati katika issue hii kanuni za Chama na mchakato wa uteuzi utazingatiwa. Hii mbinu ya Mzee Makamba, ambaye anajua kwamba mgombea wake hachaguliki na kudhani watamtisha Rais asitekeleze majukumu yake wakati wa uteuzi hazitafua dafu.

Makamba hana hata aibu, mwezi huu wa Ramadhan, kukanusha kwamba hakuna makundi wakati tulio nje tunajua kwamba kuna makundi mawili ndani ya chama. Kuna wale ambao ni walafi, wabinafsi, wahujumu rasilimali za nchi na wadumaza maendeleo kwa upande mmoja, na wale watetea haki za wanyonge, wapinga ufisadi na wapigania haki na walinzi wa rasilimali zetu kwa upande mmoja. Yeye ni mnufaika wa kundi la kwanza na ndiye gamba namba moja. Sasa anaibuka na kujifanya ni nabii, aende zake akaendeshe hotel yake aliyoijenga kwa fedha za ufisadi na hata kuhamishia fenicha za CCM huko!

Mafanikio au Matatizo ya nchi hii sio hao watu mano wataja kuwa wanaaa au hawafai kuwa marais wa nchi hii, Mtu ambaye mpaka sasa hajui kwamba matatizo tuliyonayo chanzo chake ni CCM basi ana tatizo kwenye ubongo ambalo hakuna wa kumsaidia... mi ninachojua wazee ndio huwa waoga wa mabadiliko sio vijana... tafakari chukua hatua...
 
ukitaka kupata cheo cha ukatibu mkuu ccm sifa ya kwanza unatakiwa UWE MROPOKAJI ANGALIA MAKAMBA, MUKAMA
 
Kwani Mungu anapiga kura?

wavivu wa kufikiri au watu wenye kupenda kuficha jambo haraka sana husingizia Mungu.Katika kuishi tunapanga kisha ndani yake Mungu huwapo. maana imeandikwa wakusanyikapo wawili kwa ajili yang mimi nipo kati yao.
 
Makamba mtu wake ni EL.asitudanganye, Wakati JK Mtu wake ni MEMBE, Lakini wote ni mafisadi Tutakomaa hatutaki Raisi wenye harufu ya ufisadi au chama chenye harufu ya ufisadi!

umelenga sawa ndio maana anatetea watu kujivua gamba!mzee anazeeka vibaya!
 
Umenifurahisha kwa 1. umeliandika neno Mungu (tofauti na god) kama mimi 2. umekubaliana na mimi bila kunielewa na bila kujua. ni fafanue kidogo labda utanielewa na utaendelea kukubaliana nami. kuwa watu wote tumeumbwa na Mungu kwa mujibu wa imani ya dini yangu. Mungu atampa kibali mtu wa kutuongoza kutokana na majority tunavyo wajibika au tusivyowajibika kwake. kama tunawajibika kwa shetani atampa kibali mtu anayewajibika kwa shetani ili kututia adabu.sasa ni wajibu wa wanaotawaliwa kuomba hekima ya Mungu huyohuyo iliwajue mamlaka inayotawala inamtii shetani au Mungu kwa kuangalia matendo yao wenyewe naya wa watawala wao halafu wachukue hatua. bahati mbaya masuala yanayo husu kumtii na kumuomba Mungu hayana spoon feeding ni juhudi za mtu mmoja mmoja na kwa mambo mengine kama taifa.

Nilichojifunza hapa ni kwamba Imani yako na Yangu ni Tofauti.
 
Hapana, siri iliyoibuliwa na Mzee Makamba ni kuwa Rais Kikwete hatokuwa na nguvu ya ushawishi ndani ya CCM katika kukichagulia Chama cha Mapinduzi Mgombea wa Urais..!:eek2:
 
*Aonya mgombea atakayebebwa na Kikwete

Na Mwandishi Wetu

Kuhusu dhana ya ‘kujivua gamba’ ndani ya CCM, Makamba alisema kauli hiyo imetafsiriwa vibaya na wale wanaoitekeleza.

Alisema lengo la kujivua gamba halikuwa likiwalenga baadhi ya wanasiasa wachache ndani ya Chama cha Mapinduzi wanaotuhumiwa kwa ufisadi bali ililenga kuwaondoa watu walioonekana kukaa kwa muda mrefu katika safu za uongozi ndani ya chama na kuleta damu changa ili nao waje waongoze wakiwa na mbinu mpya.
Source: Gazeti la Fahamu

Well Said mzee Makamba...
 
Hapana, siri iliyoibuliwa na Mzee Makamba ni kuwa Rais Kikwete hatokuwa na nguvu ya ushawishi ndani ya CCM katika kukichagulia Chama cha Mapinduzi Mgombea wa Urais..!:eek2:

ukiangalia kwa makini hamna Rais anayemalizia muda wake aliyefanikiwa kuweka mtu wake katika historia yetu. Nyerere alimtaka Salim 85' hakamkosa, Mwinyi alikua na mtu wake na siyo Mkapa, Mkapa alitaka Kigoda 2005, Jk hawezi kutuwekea mtu wake, hawezi hii iko obvious huyu makamba anaongea mambo ya wazi na watu wananukuu...
 
Back
Top Bottom