Kwa kifupi maneno yako ni ya mtu mvivu wa kufikiri, mtegemezi anayedhani mambo mzuri huja km zawadi..Mh. Rais mstaafu Jakaya Kikwette tunayo matumaini makubwa kwenu kuwa ule muda ambao taifa hili limeusubiri mno hatimaye umewadia.
Ni wazi kuwa kila mtu katika nchi hii angalipendelea tuishi sote kwa usawa na haki. Utashi wa viongozi wa juu katika kufanikisha hayo ni jambo la muhimu sana.
Kufanya maamuzi magumu yatakayorejesha imani ya wananchi kwa nchi yao itakuwa jambo la msingi mno kwa sasa labda kuliko jambo lolote lile.
Pana watu wakiwamo watia nia wengi waliojaribu kuutaka urais na kura kuwa hazikutosha hali nafasi ni moja wakiwamo akina:
1. Asha Rose Migiro
2. Mzee Mwandosya
3. Bernard Membe
4. Mizengo Pinda
5. Frederick Sumaye
6. Edward Lowassa
7. Abdulhaman Kinana
8. Philip Mangula
9. Anna Mghwira
10. Dkt. Slaa
11. Dkt. Nchimbi
12. Nk nk
Watu ambao hawakuwamo ndani ya establishment ya sasa au wale waliokuwa na maoni tofauti kuhusiana na establishment ya sasa kwa hakika wangetufaa sana.
JK tupeni raha kwa kuandaa mustakabala mwema utakaotuletea mwanzo mpya.
Who s JK now? Watanzania tujifunze kujitegemea, hizi siyo zama za kurudia rudia watu kwenye uongozi, mtu akifanya sehemu yake akamaliza au akastaafu basi imetosha..Tanzania ina watu million 60 sasa kwa hivyo wapo wenye uwezo pengine kupita hata hao waliohudumu nafasi mbali mbali..kurecyle viongozi ni kuonyesha kiwango cha juu sana kwamba nchi haina watu wapya wnaoweza kuwa viongozi! HAPANA..nadhani tumeshatoka huko tuangalie mbele, wastaafu wapumzike zamu yao ilishapita.