Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Akiongea na kituo cha runinga cha Azam, leo asubuhi mjini Dodoma, mzee John Malecela amemshukuru aliekuwa raisi marehemu John Magufuli kwa kazi nzito ya kujenga upya mji wa Dodoma.
Mzee John Malecela ambae aliwahi kuwa waziri mkuu wa Tanzania na balozi nchini Uingereza amemtakia kheri Raisi Samia Suluhu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aliulizwa kuhusu maono ya marehemu JPM kama CCM itaweza kuyabeba na kuyandeleza yale yote ambayo ameyaacha.
Mzee Malecela akajibu kwamba marehemu John Magufuli alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa CCM aliahidi kukiimarisha chama cha mapinduzi na kukifanya kuwa chama chenye nguvu nchini.
Akaendelea kwa kusema nguvu ya CCM ilijidhihirisha kwenye uchaguzi wa mwaka 2020.
Mwisho akatoa onyo kwamba ikiwa kuna mafisadi ambao wana mpango wa kuja kukivuruga chama cha mapinduzi basi anaahidi kuwa watashughulikiwa ipasavyo.
Hayo ni maoni makini ya mmoja wa wazee na waasisi wa taifa hili yaani kwa kiingereza twasema "part of establishement".
Lakini tuchukulie kuwa hilo ni onyo kwa kila mtanzania ambae ana mawazo mengine mbadala ya mawazo ya CCM na dira ya maendeleo 2015-2025.
Wakati huohuo CCM mchana huu wapo kwenye kikao kizito kinachokaliwa na mzee Phillip Mangula.
Katibu mwenezi Humphrey Polepole anatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu yalojiri kwenye kikao hicho.
Mzee John Malecela ambae aliwahi kuwa waziri mkuu wa Tanzania na balozi nchini Uingereza amemtakia kheri Raisi Samia Suluhu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aliulizwa kuhusu maono ya marehemu JPM kama CCM itaweza kuyabeba na kuyandeleza yale yote ambayo ameyaacha.
Mzee Malecela akajibu kwamba marehemu John Magufuli alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa CCM aliahidi kukiimarisha chama cha mapinduzi na kukifanya kuwa chama chenye nguvu nchini.
Akaendelea kwa kusema nguvu ya CCM ilijidhihirisha kwenye uchaguzi wa mwaka 2020.
Mwisho akatoa onyo kwamba ikiwa kuna mafisadi ambao wana mpango wa kuja kukivuruga chama cha mapinduzi basi anaahidi kuwa watashughulikiwa ipasavyo.
Hayo ni maoni makini ya mmoja wa wazee na waasisi wa taifa hili yaani kwa kiingereza twasema "part of establishement".
Lakini tuchukulie kuwa hilo ni onyo kwa kila mtanzania ambae ana mawazo mengine mbadala ya mawazo ya CCM na dira ya maendeleo 2015-2025.
Wakati huohuo CCM mchana huu wapo kwenye kikao kizito kinachokaliwa na mzee Phillip Mangula.
Katibu mwenezi Humphrey Polepole anatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu yalojiri kwenye kikao hicho.