Mzee David Wakati Katutoka Leo

David alikuwa na kipindi chake maalum cha dakika 30 kizuri sana kielimu nimekisahau jina. Magwiji wa habari nchi hii hauwezi kumkosa David. Mungu ailaze mahala pema peponi roho yake. Amen.
TBC Taifa watamuenzi kwa stahili yake nadhani.
 
RIP Mzee David Wakati.Nakumbuku kipindi chake maarufu alikuwa kikimalizika anaaga na wimbo "Mungu akipenda tutaonana tena"
 
Nadhani Muheshimiwa Sana Amepata sehemu ya Kwenda Kuzuga Kwa lengo la Kujifanya Yupo Karibu na Wananchi!! Naona Huu Msiba ni wa Hadhi Yake

RIP DAVID

Mizaha mingine ya siasa za majitaka haifai kuwekwa kwenye suala kama hili la msiba.
 
alikuwa anasoma taarifa ya habari vizuri sana ..
 
nilitegemea katika kuhazimisha miaka hamsini ya utanganyika tungesikia kitu kutoka kwake. lakini haikuwa hivyo!
mungu amsamehe kwa mapungufu aliyonayo na amlaze salama.

RIP D Wakati
wale walio soma minaki au pugu moja kati ya shule hizi sikumbuki vizuri ni siku nyingi alishawahi kuzungumzia alisoma moja ya shule hizo wamempoteza mzee wao.
 
Mola muweke pahala anapo stahikhi David Wakati.
 
David Wakati wakati wako umewadia wa kurejea kwa muumba RIP
 
Mchango wako kwa Taifa letu hauwezi kusahahulika, Rest In Peace.

Kwa Familia, Mungu awape nguvu.
 
mungu akulaze mahali pema peponi nakumbuka sauti ya mvuto ya mzee huyu kwenye taarifa ya habari pamoja na jacob tesha sijui yuko wapi kwa sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…