Mzee Butiku: Wanasiasa wanaopuuza Katiba mpya kabla ya 2025, hawana utu 🙏

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,161
22,669
Salaam, Shalom,

Mmoja kati ya wazee wazalendo waliobaki nchini, Mzee Joseph Butiku, ameendelea kuwaasa wanasiasa wote Wanaopuuza umuhimu wa KATIBA mpya kuacha ubinafsi na kuthamini UTU.

Ikumbukwe pia, mwezi Octoba, aliyekuwa Waziri mkuu Awamu ya Pili, Mzee Joseph WARIOBA alipokuwa katika mahojiano katika kipindi Cha DAKIKA 45, ITV, Alipendekeza pia kuwa, ni vizuri Katiba mpya ikapatikana kabla ya Uchaguzi 2025. Na muda uliopo unatosha ikiwa tutaanza ilipoishia Tume aliyoisimamia kabla.

Wanasiasa wanatakiwa kuthibitisha kuwa Wana UTU na kuhakikisha wanatoa ushirikiano kuhakikisha tunapata Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.

Wazee ni hazina, Tuwatumie.

Na hiyo ni message Kwa kijana wa chama kuwa kamwe wazee hawawezi kunyamaza na kuacha Kutoa maoni kulisaidia Taifa Kwa kisingizio Cha "KUSTAAFU".

Source: The Chanzo tv

Karibuni🙏
 
Salaam, Shalom,

Mmoja kati ya wazee wazalendo waliobaki nchini, Mzee Joseph Butiku, ameendelea kuwaasa wanasiasa wote Wanaopuuza umuhimu wa KATIBA mpya kuacha ubinafsi na kuthamini utu.

Ikumbukwe pia, mwezi Octoba, aliyekuwa Waziri mkuu Awamu ya kwanza, Mzee Joseph WARIOBA alipokuwa katika mahojiano katika kipindi Cha DAKIKA 45, ITV, Alipendekeza pia kuwa, ni vizuri Katiba mpya ikapatikana kabla ya Uchaguzi 2025.

Wazee ni hazina, Tuwatumie.

Source: The Chanzo tv

Karibuni
MZEE wangu Wanasiasa wa Chama Tawala hawataki KATIBA MPYA ndio maana Pamoja na Ilani ya Chama CCM ya 2015 kuwa Itaendeleza Mchakato wa Katiba Mpya Hayati Magufuli alisema Katiba Mpya sio Kipau mbele bado akasema Hana Bajeti yake.Baada ya Utawala kubadilika Mapya yakaibuka ya Vikosi Kazi na Wananchi Kusomea Elimu ya Katiba zote hizo ni mbinu za Ucheleweshaji.Binafsi natabiri Katiba Mpya mwaka 2035

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
MZEE wangu Wanasiasa wa Chama Tawala hawataki KATIBA MPYA ndio maana Pamoja na Ilani ya Chama CCM ya 2015 kuwa Itaendeleza Mchakato wa Katiba Mpya Hayati Magufuli alisema Katiba Mpya sio Kipau mbele bado akasema Hana Bajeti yake.Baada ya Utawala kubadilika Mapya yakaibuka ya Vikosi Kazi na Wananchi Kusomea Elimu ya Katiba zote hizo ni mbinu za Ucheleweshaji.Binafsi natabiri Katiba Mpya mwaka 2035

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Mzee Warioba na Mzee Butiku, kwenye suala la Katiba mpya, misimamo yao inajulikana.

Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote,ndo mpango mzima.
 
Hili lizee lilikuwa linataka katiba ibadilishwe ili Magufuli aongezewe muda zaidi ya miaka 10, halafu leo linajidai lina busara
Duh! Ebu weka source hapa sisi wengine tujiridhishe zaidi.

However, issue hapa bado siyo solid. Kwasababu obviously hajawataja hao wanasiasa, sidhani kama kuna wana ccm hawa kizazi cha uchawa ambao wanakubaliana na katiba mpya bila kujali nafasi walizonazo. Wawe na madaraka au la.

Ndo maana mleta mada amewataja wawili tu kama sikosei mzee Butiku na mzee Warioba.

Zaidi ya hao unaweza kunitajia mwana ccm mwingine ambaye anakubaliana na katiba mpya?
 
Salaam, Shalom,

Mmoja kati ya wazee wazalendo waliobaki nchini, Mzee Joseph Butiku, ameendelea kuwaasa wanasiasa wote Wanaopuuza umuhimu wa KATIBA mpya kuacha ubinafsi na kuthamini utu.

Ikumbukwe pia, mwezi Octoba, aliyekuwa Waziri mkuu Awamu ya kwanza, Mzee Joseph WARIOBA alipokuwa katika mahojiano katika kipindi Cha DAKIKA 45, ITV, Alipendekeza pia kuwa, ni vizuri Katiba mpya ikapatikana kabla ya Uchaguzi 2025.

Wanasiasa wanatakiwa kuthibitisha kuwa Wana UTU na kuhakikisha wanatoa ushirikiano kuhakikisha tunapata Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.

Wazee ni hazina, Tuwatumie.

Source: The Chanzo tv

Karibuni

Warioba hajawahi kuwa waziri mkuu awamu ya kwanza. Amekuwa waziri mkuu awamu ya pili ya Mzee Mwinyi toka 1985-1990 mwisho!
Awamu ya kwanza aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali.
 
Salaam, Shalom,

Mmoja kati ya wazee wazalendo waliobaki nchini, Mzee Joseph Butiku, ameendelea kuwaasa wanasiasa wote Wanaopuuza umuhimu wa KATIBA mpya kuacha ubinafsi na kuthamini utu.

Ikumbukwe pia, mwezi Octoba, aliyekuwa Waziri mkuu Awamu ya kwanza, Mzee Joseph WARIOBA alipokuwa katika mahojiano katika kipindi Cha DAKIKA 45, ITV, Alipendekeza pia kuwa, ni vizuri Katiba mpya ikapatikana kabla ya Uchaguzi 2025.

Wanasiasa wanatakiwa kuthibitisha kuwa Wana UTU na kuhakikisha wanatoa ushirikiano kuhakikisha tunapata Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.

Wazee ni hazina, Tuwatumie.

Source: The Chanzo tv

Karibuni

Pesa ipo ya kufanya hayo mambo ya zimamoto?
 
Warioba hajawahi kuwa waziri mkuu awamu ya kwanza. Amekuwa waziri mkuu awamu ya pili ya Mzee Mwinyi toka 1985-1990 mwisho!
Awamu ya kwanza aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali.
Ahsante Kwa marekebisho.

Maoni Yako tafadhali.
 
Hawa wazee wanajali na kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko binafsi, maslahi CCM, vyeo, pesa. Wazalendo wa ukweli.
Nimekuwa nikisisitiza kuwa CCM Bado Ina watu wazalendo.
 
Salaam, Shalom,

Mmoja kati ya wazee wazalendo waliobaki nchini, Mzee Joseph Butiku, ameendelea kuwaasa wanasiasa wote Wanaopuuza umuhimu wa KATIBA mpya kuacha ubinafsi na kuthamini UTU.

Ikumbukwe pia, mwezi Octoba, aliyekuwa Waziri mkuu Awamu ya Pili, Mzee Joseph WARIOBA alipokuwa katika mahojiano katika kipindi Cha DAKIKA 45, ITV, Alipendekeza pia kuwa, ni vizuri Katiba mpya ikapatikana kabla ya Uchaguzi 2025. Na muda uliopo unatosha ikiwa tutaanza ilipoishia Tume aliyoisimamia kabla.

Wanasiasa wanatakiwa kuthibitisha kuwa Wana UTU na kuhakikisha wanatoa ushirikiano kuhakikisha tunapata Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.

Wazee ni hazina, Tuwatumie.

Na hiyo ni message Kwa kijana wa chama kuwa kamwe hawawezi kunyamaza na kuacha Kutoa maoni kulisaidia Taifa Kwa kisingizio Cha "KUSTAAFU".

Source: The Chanzo tv

Karibuni🙏
Kwa uzoefu wangu na kutokana na tafiti mbalimbali ktk nchi mbalimbali hapa duniani, hakuna nchi hata moja ambayo ina Katiba nzuri iliyotokana na mawazo, fikra na maoni ya Wananchi wengi zaidi ktk nchi husika bila ya Wananchi hao kupigana mapigano ya umwagaji wa damu, hakuna nchi ya namna hiyo, haipo. Fanya utafiti wako binafsi utagundua ukweli huu mchungu.
 
Kwa uzoefu wangu na kutokana na tafiti mbalimbali ktk nchi mbalimbali hapa duniani, hakuna nchi hata moja ambayo ina Katiba nzuri iliyotokana na mawazo, fikra na maoni ya Wananchi wengi zaidi ktk nchi husika bila ya Wananchi hao kupigana mapigano ya umwagaji wa damu, hakuna nchi ya namna hiyo, haipo.
Hiyo Nchi IPO, ni Moja tu ,Tanzania.
 
Back
Top Bottom