Binafsi nionavyo mimi, mzalendo ni mtu ambaye ana moyo wa dhati katika jambo fulani ambapo yeye atahakikisha anasimamia na kulinda maslahi ya kila mdau kuhusiana na jambo husikka,mathalani viongozi wetu ambao tumewapa jukumu la kuhakikisha wanatuongoza sisi kama taifa katika mchakato mzima wa kajiletea maendeleo yetu wanatakiwa kutokuwa na chembe ya ubinafsi,hata kidogo.lakini kitendo chao cha kuyatumia madaraka vibaya kama vile kukubali kusaini mikataba mibovu pamoja na ufujaji wa mali za umma, hii inatuonyesha viongozi tulionao hakuna hata mmoja ambaye ni mzalendo wa kweli,
Mzalendo anatakiwa kuwa na msimamo katika maamujzi yake na hata kuhakikisha anawahamasisha watu wengine kuwa misimamo sahihi haswa katika suala ambalo anaona lina manufaa kwa kila raia,mfano ni pale Mwl nyerere alipowakatalia wazungu kuchimba madini, na kuwaambia yatachimbwa na watanzania wenyewe watapokuwa na akili, sasa nyerere alifanya hivi makusudi ili,kila mwananchi aweze kufaidika na madini, lakini embu angalia leo watu wengine wamepewa madaraka wakatuingiza kwenye mikataba feki kabisa,
Mzalendo ni mtu ambaye anatakiwa awe ana mtazamo chanya kuhusiana na mustakabali wa jamii yake inayomzunguka, ni yule ambaye atakuwa yuko radhi kufanya kila jitihada ili aweze kuhakikisha anatafuta ufumbuzi wa busara jamiii yake kuhusiana na matatatizo yanayoikabili na sio kuwa kinara wa kuongeza matatizo katika jamii,mfano embu angalia viongozi wetu wanavyoutuongezea matataizo,wizi wa EPA,MEREMETA,RICHMOND, DOWANS,KIWIRA COAL MINES, nk
Mzalendo ni mtu ambaye yupo tayari kujitoa mhanga kupigania maslahi ya jamii yake pale anapoona jambo fulani au maaamuzi fulani yanaleta au yataleta shida kwa jamiii husika,kwahiyo ni mtu ambaye yupo radhi kuipigania jamiii yake hata kupoteza maisha yake mfano,Che Guavara,
Mzalendo anatakiwa awe mtu ambaye ana maono na mitazamo yenye kuleta tija katika jamii yake,anatakiwa awe mtu mwenye uwezo wa kufanya vitu kwa ubunifu zaidi na kujua vizuri mazingira ya jamiii yake na mabadiliko yanayotoke katika jamii hiyo kadri muda unavyokwenda,
Mzalendo ni mtu anayefanya mambo kwa vitendo na sio kwa maneno, yaani ni mtu ambaye anahakikisha anatekeleza kile anachokisema na kuwahamasisha watu wengine washirikiane nae katika kufankikisha lile ambalo kila mwanajamiii ataona kuwa lina manufaaa na linahitajika kufanywa kwa wakati huo,mfano kipindi cha mapinduzi ya Urusi watu wote wa kada ya chini ambao walikuwa wananyonywa walihamasishwa na walihamasika na kumuunga mkono bwana illyich na kufanikiwa kuleta mapinduzi ya kweli
Mzalendo anatakiwa awe objective yaaani value free hatakiwi kuwa bias, kwahiyo anatakiwa awe mwepesi kukubali kukosolewa na kukubali maoni na mitazamo ya wengine katika jamiii,anatakiwa awe mtu wa kujifunza kila siku mambo mabalimbali yanayoizunguka jamii yake.
lakini kwa hapa Tanzania tuliokuwa nao wengi wazalendo uchwara yaani feki kabisa,waliojitahidi kuonyesha uzalendo ni SOKOINE na NYERERE TU.