nakumbuka wakati fulani nilipo kuwa nimeajiriwa kwa majirani akina
MK254 pale jijini nairobi.nilikuwa nina tabia ya kujifanya workaholic,wenzangu wanatoka saa 11/12 jioni ,wananiachia funguo nami nakomaa mpaka saa 5/6 usiku.nilikuwa sina sababu ya kuwahi maskani kwangu buruburu since familia yangu (wife and kids) ipo tanzania.niwahi nini nyumbani wakati naishi peke yangu katika nchi ya watu,ni kupiga kazi kwa kwenda mbele.
sasa basi,siku moja ilipo fika saa 6 usiku,nikafunga ofisi na kuelekea geti kuu la jengo ili nitoke niende stendi kuchukua matatu(dala dala) nielekee zangu nyumbani.nilipo fika getini,mlinzi akanizuia.akaniambia mtized siwezi nikakuruhusu uendee nyumbani mida hii,nikapigwa na butwaa!!.nikamuuluza kwanini hutaki kunifungulia mlango niende?,akaniambia sikiliza mtized this is nairobi na hii ni mida ya wakora(wahalifu),kwa maana hiyo sitataka niwajibike kwa lolote litakalo kutokea.
nikawa mkali,nikaanza kumfokea mlinzi kwa kutotaka kunifungulia geti.basi baada ya majibizano ya kama dakika 15 hivi,mlinzi yule akawa mpole na akakubali kunifungulia geti kwa sharti kwamba chochote kitakacho nitokea nje ya geti,yeye hatawajibika.
nikatoka na nikawa natembea kuelekea kituo cha daladala hatua chache toka ofisini.baada ya dakika kama 5 hivi nikasikia milio ya risasi ikitoa upande niliokuwa naelekea.wakora walikuwa kazini,kuna tukio walikuwa wanapiga katika duka moja jirani na jengo ilipo ofisi yetu.
nilichanganyikiwa maana nilikuwa peke yangu pale njiani,walinzi wote wamejifungia ndani ya mageti yao,ifahamike kwamba walinzi wa majengo jijini nairobi huwa wanajifungia ndani ya majengo wanayolinda na kuacha kijishimo kidogo ktk geti ili kuchungulia kinacho endelea nje,hii ni tofauti na dsm ambapo baadhi ya makampuni au majengo,walinzi hujifungia nje.
milio ya risasi ilikuwa inaendelea kurindima,uamuzi wa haraka ulionijia ni kukimbilia katika geti la lile jengo la ofisi yetu.nilifika pale nikiwa nahema kwa hofu na uoga,nikwamwita yule mlinzi na kumuomba anifungulie geti nirudi ndani,mwanzo alisita lakini baadaye alinifungulia kwa tendo la haraka na kufunga geti mda huo huo.
baada ya hali ile kutulia,sharti alilonipa ni kwamba hatofungua geti tena mda ule,hivyo basi itabidi nilale ofisi.nilikubaliana na uamuzi wake bila ubishi.nililala ofisini mpaka asubuhi.tangu siku ile,niliachana kabisa na tabia ya kujifanya workaholic kwa kazi za kuajiliwa na kuchelewa kutoka ofisini until midnight
ninachotaka kukwambia dada yangu
badiebey ni kwamba usikubali shemeji atoke kazini night hours,kwani kwa kufanya hivyo ipo siku atakukumbana na majanga asiyo yatarajia,haijalishi anatumia private transport au public transport.
kwa mfano mvutie picha pale siku moja atakapo zimikiwa na umeme ktk jengo la ghorofa 5/6 mda wa usiku,halafu jengo zima amebaki peke yake ofisini ghorofa ya 4.noma sana.