kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,307
- 12,602
Hizi shangwe sio za bure,
Mkutano Mkuu wa CCM umekwisha, mengi tumeyaona na mengi tumeyasikia. Sasa tunafahamu ni nani kasema nini na nani anataka nini.
Tumejitoa ufahamu watanzania wote kukubali kuogopa kuiadhibu CCM hata kama inafanya makosa tusiyoyataka. CCM imegeuka Mungumtu, hakuna anaeihoji akabaki kuwa na amani yake, atabezwa na kudhihakiwa. Kila mtu na kila kundi linaitumia CCM kama kichaka TU kufanikisha kile anachokikusudia kukitekeleza hata kama kiwe kinaiumiza Tanganyika, Zanzibar au Tanzania yote na watu wake.
Hata wenye akili timamu wanageuka kuwa wendawazimu wakifika kwenye vikao vya CCM, wanazisahau na kuzidharau agenda zao ndani ya vikao vya CCM, wanabaki wanakenua tu wapende wasipende.
Ndani ya vikao vya CCM mashetani wanageuka malaika na malaika wanageuka mashetani kwa kutumia silaha ya kudumisha umoja ndani ya CCM na kutesa kwa zamu na kulamba asali kwa zamu kwa kuwaamina wajumbe wote wa mkutano kuwa adui Yao namba moja ni watanzania wenzao ambao wako kwenye vya upinzani.
Hata kwa maslahi mapana ya taifa hakuna anaekubali kutofautiana na walamba asali wa zamu kwa kuhofia asiyoyajua kumfika. Sisi wote wanaCCM na wasio wanaCCM, wenye elimu na wasiokuwa na elimu wa dini zote na jinsia zote na makabila yote tunabaki kuangalia tu hata kama tunajkiua kile wanachokikosea, kile wanachokiharibu, kile wanachokiiba, na kile wanachogawana kwa maslahi yao binafsi, familia zao, koo zao na kanda zao wanakotoka.
Hata Ndugai pale sio kama yuko shwali, bali anafikiria atafanya nini sasa mbele yao, amuombe nani wafanye nini, aseme nini ambacho ni tofauti na wao na itakuwaje kwake kama akisema nini.
Mwalimu Nyerere aliyajua haya ya kulamba asali kwa zamu kuwa yatakuja kutokea wakati yeye hayupo duniani, na yatamkosa mtu madhubuti wa kuyakemea. Hii ndio sababu ya msingi kabisa ya yeye kuishinikiza CCM kukubali uwepo wa vyama vingi vya siasa nchini hata kama wananchi kwakutumia kura ya maoni walikataa vyama vingi. Nyerere alitaka vyama vingi ili visimame badala yake kuikosoa CCM atakapokuwa hayupo duniani.
Na Nyerere hakutaka kuwepo na utitiri wa vyama vya siasa, bali alitaka CCM ishindane kwa haki na chama kingine kikubwa cha upinzani. Bahati nzuri hicho chama cha upinzani alikitaja kabisa kwa jina kutokana na kuwa na sera safi. Kwakuwa chama hiki cha upinzani kilipata baraka kamili za baba wa Taifa hivyo nawaomba wale wote ambao ni wana CCM kindakindaki wasioridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa ndani ya CCM wahamie CHADEMA ili kukipa nguvu ambayo Mwl Nyerere aliikusudia chadema iwe nayo.
Mwl. Nyerere aliendelea kusema, mpinzani wa kweli wa CCM atatoka CCM, hivyo ni muda wa unabii wa Mwl Nyerere kutimia. Na kila mwanasiasa au mtu yeyoteambae ataihujumu chadema ajue hataishi kwa amani kwakuwa chadema ina mkono, ndoto na wosia wa Mwl Nyerere mwenyewe kwa wanaCCM wenzake na watanzania wote. Aliyasema yote kuhusu chadema hadharani hakuna ambaye hakumsikia akisema juu ya chadema.
Ni bahati mbaya tu chadema ya sasa nayo ina viongozi ambao wanaochumia tumbo zao ingawa ina sera safi ambazo mwl Nyerere alizikubali na kuzisifia hadharani mchana kweupe. Ni muda wa wanaCCM kuhamia chadema ili unabii wa baba wa Taifa utimie.
Mkutano Mkuu wa CCM umekwisha, mengi tumeyaona na mengi tumeyasikia. Sasa tunafahamu ni nani kasema nini na nani anataka nini.
Tumejitoa ufahamu watanzania wote kukubali kuogopa kuiadhibu CCM hata kama inafanya makosa tusiyoyataka. CCM imegeuka Mungumtu, hakuna anaeihoji akabaki kuwa na amani yake, atabezwa na kudhihakiwa. Kila mtu na kila kundi linaitumia CCM kama kichaka TU kufanikisha kile anachokikusudia kukitekeleza hata kama kiwe kinaiumiza Tanganyika, Zanzibar au Tanzania yote na watu wake.
Hata wenye akili timamu wanageuka kuwa wendawazimu wakifika kwenye vikao vya CCM, wanazisahau na kuzidharau agenda zao ndani ya vikao vya CCM, wanabaki wanakenua tu wapende wasipende.
Ndani ya vikao vya CCM mashetani wanageuka malaika na malaika wanageuka mashetani kwa kutumia silaha ya kudumisha umoja ndani ya CCM na kutesa kwa zamu na kulamba asali kwa zamu kwa kuwaamina wajumbe wote wa mkutano kuwa adui Yao namba moja ni watanzania wenzao ambao wako kwenye vya upinzani.
Hata kwa maslahi mapana ya taifa hakuna anaekubali kutofautiana na walamba asali wa zamu kwa kuhofia asiyoyajua kumfika. Sisi wote wanaCCM na wasio wanaCCM, wenye elimu na wasiokuwa na elimu wa dini zote na jinsia zote na makabila yote tunabaki kuangalia tu hata kama tunajkiua kile wanachokikosea, kile wanachokiharibu, kile wanachokiiba, na kile wanachogawana kwa maslahi yao binafsi, familia zao, koo zao na kanda zao wanakotoka.
Hata Ndugai pale sio kama yuko shwali, bali anafikiria atafanya nini sasa mbele yao, amuombe nani wafanye nini, aseme nini ambacho ni tofauti na wao na itakuwaje kwake kama akisema nini.
Mwalimu Nyerere aliyajua haya ya kulamba asali kwa zamu kuwa yatakuja kutokea wakati yeye hayupo duniani, na yatamkosa mtu madhubuti wa kuyakemea. Hii ndio sababu ya msingi kabisa ya yeye kuishinikiza CCM kukubali uwepo wa vyama vingi vya siasa nchini hata kama wananchi kwakutumia kura ya maoni walikataa vyama vingi. Nyerere alitaka vyama vingi ili visimame badala yake kuikosoa CCM atakapokuwa hayupo duniani.
Na Nyerere hakutaka kuwepo na utitiri wa vyama vya siasa, bali alitaka CCM ishindane kwa haki na chama kingine kikubwa cha upinzani. Bahati nzuri hicho chama cha upinzani alikitaja kabisa kwa jina kutokana na kuwa na sera safi. Kwakuwa chama hiki cha upinzani kilipata baraka kamili za baba wa Taifa hivyo nawaomba wale wote ambao ni wana CCM kindakindaki wasioridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa ndani ya CCM wahamie CHADEMA ili kukipa nguvu ambayo Mwl Nyerere aliikusudia chadema iwe nayo.
Mwl. Nyerere aliendelea kusema, mpinzani wa kweli wa CCM atatoka CCM, hivyo ni muda wa unabii wa Mwl Nyerere kutimia. Na kila mwanasiasa au mtu yeyoteambae ataihujumu chadema ajue hataishi kwa amani kwakuwa chadema ina mkono, ndoto na wosia wa Mwl Nyerere mwenyewe kwa wanaCCM wenzake na watanzania wote. Aliyasema yote kuhusu chadema hadharani hakuna ambaye hakumsikia akisema juu ya chadema.
Ni bahati mbaya tu chadema ya sasa nayo ina viongozi ambao wanaochumia tumbo zao ingawa ina sera safi ambazo mwl Nyerere alizikubali na kuzisifia hadharani mchana kweupe. Ni muda wa wanaCCM kuhamia chadema ili unabii wa baba wa Taifa utimie.