Mwl. Nyerere aliitabiria mema CHADEMA, Ndugai na Bashiru msihuzunike

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,307
12,602
Hizi shangwe sio za bure,


Mkutano Mkuu wa CCM umekwisha, mengi tumeyaona na mengi tumeyasikia. Sasa tunafahamu ni nani kasema nini na nani anataka nini.

Tumejitoa ufahamu watanzania wote kukubali kuogopa kuiadhibu CCM hata kama inafanya makosa tusiyoyataka. CCM imegeuka Mungumtu, hakuna anaeihoji akabaki kuwa na amani yake, atabezwa na kudhihakiwa. Kila mtu na kila kundi linaitumia CCM kama kichaka TU kufanikisha kile anachokikusudia kukitekeleza hata kama kiwe kinaiumiza Tanganyika, Zanzibar au Tanzania yote na watu wake.

Hata wenye akili timamu wanageuka kuwa wendawazimu wakifika kwenye vikao vya CCM, wanazisahau na kuzidharau agenda zao ndani ya vikao vya CCM, wanabaki wanakenua tu wapende wasipende.
Ndani ya vikao vya CCM mashetani wanageuka malaika na malaika wanageuka mashetani kwa kutumia silaha ya kudumisha umoja ndani ya CCM na kutesa kwa zamu na kulamba asali kwa zamu kwa kuwaamina wajumbe wote wa mkutano kuwa adui Yao namba moja ni watanzania wenzao ambao wako kwenye vya upinzani.

Hata kwa maslahi mapana ya taifa hakuna anaekubali kutofautiana na walamba asali wa zamu kwa kuhofia asiyoyajua kumfika. Sisi wote wanaCCM na wasio wanaCCM, wenye elimu na wasiokuwa na elimu wa dini zote na jinsia zote na makabila yote tunabaki kuangalia tu hata kama tunajkiua kile wanachokikosea, kile wanachokiharibu, kile wanachokiiba, na kile wanachogawana kwa maslahi yao binafsi, familia zao, koo zao na kanda zao wanakotoka.

Hata Ndugai pale sio kama yuko shwali, bali anafikiria atafanya nini sasa mbele yao, amuombe nani wafanye nini, aseme nini ambacho ni tofauti na wao na itakuwaje kwake kama akisema nini.

Mwalimu Nyerere aliyajua haya ya kulamba asali kwa zamu kuwa yatakuja kutokea wakati yeye hayupo duniani, na yatamkosa mtu madhubuti wa kuyakemea. Hii ndio sababu ya msingi kabisa ya yeye kuishinikiza CCM kukubali uwepo wa vyama vingi vya siasa nchini hata kama wananchi kwakutumia kura ya maoni walikataa vyama vingi. Nyerere alitaka vyama vingi ili visimame badala yake kuikosoa CCM atakapokuwa hayupo duniani.

Na Nyerere hakutaka kuwepo na utitiri wa vyama vya siasa, bali alitaka CCM ishindane kwa haki na chama kingine kikubwa cha upinzani. Bahati nzuri hicho chama cha upinzani alikitaja kabisa kwa jina kutokana na kuwa na sera safi. Kwakuwa chama hiki cha upinzani kilipata baraka kamili za baba wa Taifa hivyo nawaomba wale wote ambao ni wana CCM kindakindaki wasioridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa ndani ya CCM wahamie CHADEMA ili kukipa nguvu ambayo Mwl Nyerere aliikusudia chadema iwe nayo.

Mwl. Nyerere aliendelea kusema, mpinzani wa kweli wa CCM atatoka CCM, hivyo ni muda wa unabii wa Mwl Nyerere kutimia. Na kila mwanasiasa au mtu yeyoteambae ataihujumu chadema ajue hataishi kwa amani kwakuwa chadema ina mkono, ndoto na wosia wa Mwl Nyerere mwenyewe kwa wanaCCM wenzake na watanzania wote. Aliyasema yote kuhusu chadema hadharani hakuna ambaye hakumsikia akisema juu ya chadema.

Ni bahati mbaya tu chadema ya sasa nayo ina viongozi ambao wanaochumia tumbo zao ingawa ina sera safi ambazo mwl Nyerere alizikubali na kuzisifia hadharani mchana kweupe. Ni muda wa wanaCCM kuhamia chadema ili unabii wa baba wa Taifa utimie.
 
Ndugai na Bashiru ,Polepole wanakubalika ile mbaya huku mtaani

Wanakubalika kwa lipi?. Kwa kutoa kauli moja tu na kukimbia. Ndugai aliomba msamaha na kufuta kauli yake Hana msimamo. Bashiru naye juzi alikuwa anapigia makofi kila kinachsemwa hata kama ni matusi. Msitengeze watu ambao sio.
 
nawaomba wale wote ambao ni wana CCM kindakindaki wasioridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa ndani ya CCM wahamie CHADEMA ili kukipa nguvu ambayo Mwl Nyerere aliikusudia chadema kuwa nayo. Mwl. Nyerere aliendelea kusema, mpinzani wa kweli wa CCM atatoka CCM, hivyo ni muda wa unabii wa Mwl Nyerere kutimia.
Chadema iliwahi kufanya makosa kwa kuitumia nadharia hii na kudhani itatisaidia, lkn haikufua dafu.
Chadema ilipokea viongozi waandamizi wastaafu toka ccm na serikalini (sitaki kuwataja majina yao maana wanajulikana). Lkn mpk hivi tunavyozungumza hakuna hata mmoja aliyesalia chadema.

Siyo kwamba walirejea kwa kupenda. Hapana. Walilazimika kufanya hivyo kitokana na mbinyo walioupata toka kwa watawala.

Nyerere ni kweli alikubali vyama vingi kuingia nchini lkn bila shaka alifanya hivi siyo kwasabb alisukumwa na utashi wake. Bali alilzimishwa na wenye dunia (nchi za magharibi). Ndiyo maana hakubadilisha katiba ili iendane na matakwa ya uwepo wa vyama vingi.

Kwa kuhitimisha. Nyerere hastahili sifa zote hizo ulizomwagia. Matatizo ya kidemokrasia na mfumo mbovu wa utawala tunaokabiliana nao leo vimerithiwa kutoka kwake. Hakupenda vyama vingi.

Yasemekana uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995 Nyerere alikaa mstari wa mbele kumpinga marehemu Augustine Lyatonga Mrema. Kama baba wa taifa kwann aliamua kuegemea ccm?
 
Chadema iliwahi kufanya makosa kwa kuitumia nadharia hii na kudhani itatisaidia, lkn haikufua dafu.
Chadema ilipokea viongozi waandamizi wastaafu toka ccm na serikalini (sitaki kuwataja majina yao maana wanajulikana). Lkn mpk hivi tunavyozungumza hakuna hata mmoja aliyesalia chadema.

Siyo kwamba walirejea kwa kupenda. Hapana. Walilazimika kufanya hivyo kitokana na mbinyo walioupata toka kwa watawala.

Nyerere ni kweli alikubali vyama vingi kuingia nchini lkn bila shaka alifanya hivi siyo kwasabb alisukumwa na utashi wake. Bali alilzimishwa na wenye dunia (nchi za magharibi). Ndiyo maana hakubadilisha katiba ili iendane na matakwa ya uwepo wa vyama vingi.

Kwa kuhitimisha. Nyerere hastahili sifa zote hizo ulizomwagia. Matatizo ya kidemokrasia na mfumo mbovu wa utawala tunaokabiliana nao leo vimerithiwa kutoka kwake. Hakupenda vyama vingi.

Yasemekana uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995 Nyerere alikaa mstari wa mbele kumpinga marehemu Augustine Lyatonga Mrema. Kama baba wa taifa kwann aliamua kuegemea ccm?
Mwalimu aliwahi kujibu katika mkutano na waandishi wa habari mwaka 1995 kwamba, asingeweza kuwa neutral eti kwa sababu ni Baba wa Taifa wakati CCM ilikuwa na mgombea Urais mzuri, na kusisitiza, "Niwe neutral...nimelewa?"

Pili, Mwalimu katujengea Taifa moja, alistaafu mwaka 1985 na kufariki dunia mwaka 1999, ni uhovyo uliopitiliza kuendelea kumlaumu#Wewe umeifanyia nini Tanzania?🙏🙏🙏
 
Chadema iliwahi kufanya makosa kwa kuitumia nadharia hii na kudhani itatisaidia, lkn haikufua dafu.
Chadema ilipokea viongozi waandamizi wastaafu toka ccm na serikalini (sitaki kuwataja majina yao maana wanajulikana). Lkn mpk hivi tunavyozungumza hakuna hata mmoja aliyesalia chadema.

Siyo kwamba walirejea kwa kupenda. Hapana. Walilazimika kufanya hivyo kitokana na mbinyo walioupata toka kwa watawala.

Nyerere ni kweli alikubali vyama vingi kuingia nchini lkn bila shaka alifanya hivi siyo kwasabb alisukumwa na utashi wake. Bali alilzimishwa na wenye dunia (nchi za magharibi). Ndiyo maana hakubadilisha katiba ili iendane na matakwa ya uwepo wa vyama vingi.

Kwa kuhitimisha. Nyerere hastahili sifa zote hizo ulizomwagia. Matatizo ya kidemokrasia na mfumo mbovu wa utawala tunaokabiliana nao leo vimerithiwa kutoka kwake. Hakupenda vyama vingi.

Yasemekana uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995 Nyerere alikaa mstari wa mbele kumpinga marehemu Augustine Lyatonga Mrema. Kama baba wa taifa kwann aliamua kuegemea ccm?
Kosa walilofanya chadema wakati ule ilikuwa kupokea watu wasiokuwa wasafi kutoka CCM, wengi wao walikuwa na tuhuma na mali ambazo walikuwa hawezi kueleza walizipata wapi ambazo kwa vyovyote vile zinawalazimu kubaki CCM ili kuepuka kunyang'anywa, na wengine walikataliwa na mwl Nyerere mwenyewe mchana kweupe kuwa sio wasafi na hawafai kuwa viongozi lakini chadema walipuuza wakawapokea. Hivyo chadema ililaaniwa kwa kwenda kinyume na Mwl Nyerere.

Chadema lazima lazima na lazima ipokee watu safi kutoka CCM kama Mwl Nyerere alivyoagiza ili kukipa hadhi ambayo Mwl Nyerere alikusudia iwe nayo. Kama viongozi wa chadema waliusahau huu usia wa mwl basi mm ninawakumbusha sasa, waache kuhangaika na akina Halima mdee wajenge chama na kupokea wanachama wapya safi kutoka vyama vingine.
 
Hizi shangwe sio za bure,


Mkutano Mkuu wa CCM umekwisha, mengi tumeyaona na mengi tumeyasikia. Sasa tunafahani ni nani kasema nini na nani anataka nini.

Tumejitoa ufahamu watanzania wote kukubali kuogopa kuiadhibu CCM hata kama inafanya makosa tusiyoyataka. CCM imegeuka Mungumtu, hakuna anaeihoji akabaki kuwa na amani yake, atabezwa na kudhihakiwa. Kila mtu na kila kundi linaitumia CCM kufanikisha kile anachokikusudia kukitekeleza hata kama kiwe kinaiumiza Tanganyika, Zanzibar au Tanzania yote na watu wake. Hata wenye akili timamu wanageuka kuwa wendawazimu wakifika kwenye vikao vya CCM, wanasahau na kuzidharau agenda zao ndani ya vikao vya CCM, wanabaki wanakenua tu wapende wasipende. Ndani ya vikao vya CCM mashetani wanageuka malaika na malaika wanageuka mashetani kwa kutumia silaha ya kudumisha umoja ndani ya CCM na kutesa kwa zamu na kulamba asali kwa zamu.

Hata kwa maslahi mapana ya taifa hakuna anaekubali kutofautiana na walamba asali wa zamu kwa kuhofia asiyoyajua kumfika. Sisi wote wanaCCM na wasio wanaCCM, wenye elimu na wasiokuwa na elimu wa dini zote na jinsia zote na makabila yote tunabaki kuangalia tu hata kama tunajkiua kile wanachokikosea, kile wanachokiharibu, kile wanachokiiba, na kile wanachogawana kwa maslahi yao binafsi, familia zao, koo zao na kanda zao wanakotoka.

Hata Ndugai pale sio kama yuko shwali, bali anafikiria atafanya nini sasa mbele yao, amuombe nani wafanye nini, aseme nini ambacho ni tofauti na wao na itakuwaje kwake kama akisema nini.

Mwalimu Nyerere aliyajua haya ya kulamba asali kwa zamu kuwa yatakuja kutokea wakati yeye hayupo duniani, na yatamkosa mtu madhubuti wa kuyakemea. Hii ndio sababu ya msingi kabisa ya yeye kuishinikiza CCM kukubali uwepo wa vyama vingi vya siasa nchini hata kama wananchi kwakutumia kura ya maoni walikataa vyama vingi. Nyerere alitaka vyama vingi ili visimame badala yake kuikosoa CCM atakapokuwa hayupo duniani. Na Nyerere hakutaka kuwepo na utitiri wa vyama vya siasa, bali alitaka CCM ishindane kwa haki na chama kingine kikubwa cha upinzani. Bahati nzuri hicho chama cha upinzani alikitaja kabisa kwa jina kutokana na kuwa na sera safi. Kwakuwa chama hiki cha upinzani kilipata baraka kamili za baba wa Taifa hivyo nawaomba wale wote ambao ni wana CCM kindakindaki wasioridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa ndani ya CCM wahamie CHADEMA ili kukipa nguvu ambayo Mwl Nyerere aliikusudia chadema iwe nayo. Mwl. Nyerere aliendelea kusema, mpinzani wa kweli wa CCM atatoka CCM, hivyo ni muda wa unabii wa Mwl Nyerere kutimia. Na kila mwanasiasa au mtu yeyoteambae ataihujumu chadema ajue hataishi kwa amani kwakuwa chadema ina mkono, ndoto na wosia wa Mwl Nyerere mwenyewe kwa wanaCCM wenzake na watanzania wote. Aliyasema yote kuhusu chadema hadharani hakuna ambaye hakumsikia akisema juu ya chadema.

Ni bahati mbaya tu chadema ya sasa nayo ina viongozi ambao wanaochumia tumbo zao ingawa ina sera safi ambazo mwl Nyerere alizikubali na kuzisifia hadharani mchana kweupe. Ni muda wa wanaCCM kuhamia chadema ili unabii wa baba wa Taifa utimie.

Katika kupitia pitia hili la sera nikweli nilisoma sehemu. Lakini, hakuna sehemu ( labda u- cite hapa kwa rejea ya kisomi), Mwalimu aliposema Chadema inafaa kuongoza. Wakati anang'atuka Uenyekiti wa Chama, aliusia, kiongozi safi (Rais) atatoka ndani ya CCM na, "Bila CCM madhubuti, nchi yetu itayumba".

Katika hotuba hiyo, pia Mwalimu alisema angetamani kiwepo Chama kingine kikubwa lakini cha Kijamaa. #Mwalimu hakuwa mliberali.🙏🙏🙏
 
Mwalimu aliwahi kujibu katika mkutano na waandishi wa habari mwaka 1995 kwamba, asingeweza kuwa neutral eti kwa sababu ni Baba wa Taifa wakati CCM ilikuwa na mgombea Urais mzuri, na kusisitiza, "Niwe neutral...nimelewa?"
Majibu ya hovyo haya na yasiyoendana na hadhi yake ya ubaba wa taifa.


Pili, Mwalimu katujengea Taifa moja, alistaafu mwaka 1985 na kufariki dunia mwaka 1999, ni uhovyo uliopitiliza kuendelea kumlaumu#Wewe umeifanyia nini Tanzania?🙏🙏🙏
Ktk hili nakuunga mkono kwa 100%
 
Majibu ya hovyo haya na yasiyoendana na hadhi yake ya ubaba wa taifa.



Ktk hili nakuunga mkono kwa 100%
Nakuelewa. Ila hata hiyo point juu,Mwalimu alisema pia kama upinzani ungekuwa na mgombea mzuri wa Urais kuliko CCM; angempigia kampeni yeye. Baba wa Taifa aliwajua vijana wake, nani ni nani sawa na baba ndani ya nyumba, hivyo alitaka Rais mzuri wa nchi.🙏🙏🙏
 
Nyerere ni kweli alikubali vyama vingi kuingia nchini lkn bila shaka alifanya hivi siyo kwasabb alisukumwa na utashi wake. Bali alilzimishwa na wenye dunia (nchi za magharibi). Ndiyo maana hakubadilisha katiba ili iendane na matakwa ya uwepo wa vyama vingi.
Hapa sio kweli, kumbuka kuwa wakati akiyafanya haya mwl alikuwa sio Rais, hivyo hakuna mtu ambae alimlazimisha aishinikize CCM kukubali mageuzi ya vyama vingi vya siasa, hakuwa kwenye shinikizo la aina yoyoye. Ila kumbuka kipindi hiki alikuwa pia kwenye mapambano dhidi ya serikali ya CCM kuhusu ubadhilifu, rushwa na ukabila mpaka ikamlazimu kuandika kitabu cha tujisahihishe. Lakini, Baada ya kugundua kuwa kazi ya kuikosoa serikali na CCM ni kubwa sana na ya hatari na hataweza kuifanya peke yake, na pia baada ya kugundua kuwa iko siku atakufa pia, na baada ya kugundua pia ndani ya CCM hakuna mtu mwenye nguvu kama zake za kuikosoa CCM na serikali zake baada ya yeye kuondoka, ndipo akaja na wazo la kuruhusu vyama vingi vya upinzani kuwepo ili viwe watch dogs kwa CCM na serikali. Wote tunaona wenyewe kuwa ndani ya CCM sasa hivi hakuna mwenye nguvu zile za Mwl, badala yake wanatumia ubabe, vitisho, na dola kunyamazishana wenyewe kwa wenyewe na kunyamazisha vyama vya upinzani. hakuna nguvu za hoja bali kuna hoja za nguvu.
 
Hapa sio kweli, kumbuka kuwa wakati akiyafanya haya mwl alikuwa sio Rais, hivyo hakuna mtu ambae alimlazimisha aishinikize CCM kukubali mageuzi ya vyama vingi vya siasa, hakuwa kwenye shinikizo la aina yoyoye. Ila kumbuka kipindi hiki alikuwa pia kwenye mapambano dhidi ya serikali ya CCM kuhusu ubadhilifu, rushwa na ukabila mpaka ikamlazimu kuandika kitabu cha tujisahihishe. Lakini, Baada ya kugundua kuwa kazi ya kuikosoa serikali na CCM ni kubwa sana na ya hatari na hataweza kuifanya peke yake, na pia baada ya kugundua kuwa iko siku atakufa pia, na baada ya kugundua pia ndani ya CCM hakuna mtu mwenye nguvu kama zake za kuikosoa CCM na serikali zake baada ya yeye kuondoka, ndipo akaja na wazo la kuruhusu vyama vingi vya upinzani kuwepo ili viwe watch dogs kwa CCM na serikali. Wote tunaona wenyewe kuwa ndani ya CCM sasa hivi hakuna mwenye nguvu zile za Mwl, badala yake wanatumia ubabe, vitisho, na dola kunyamazishana wenyewe kwa wenyewe na kunyamazisha vyama vya upinzani. hakuna nguvu za hoja bali kuna hoja za nguvu.
Acha nile Burger kwanza
 
Katika kupitia pitia hili la sera nikweli nilisoma sehemu. Lakini, hakuna sehemu ( labda u- cite hapa kwa rejea ya kisomi), Mwalimu aliposema Chadema inafaa kuongoza. Wakati anang'atuka Uenyekiti wa Chama, aliusia, kiongozi safi (Rais) atatoka ndani ya CCM na, "Bila CCM madhubuti, nchi yetu itayumba".

Katika hotuba hiyo, pia Mwalimu alisema angetamani kiwepo Chama kingine kikubwa lakini cha Kijamaa. #Mwalimu hakuwa mliberali.🙏🙏🙏
Vyama vya upinzani vya sasa shida yake ni hii hapa ambayo Nyerere aliiona.
 
Back
Top Bottom