Bado unachemka tuu! Tabora school ilijengwa na Waingereza kwa ajili ya kuelimisha Watawala au Viongozi wajao, na wala SIO Machifu tu, ilikuwa ni kwa yoyote yule ambaye alitimiza masharti ambayo wao (Waingereza) waliyaweka ya kupata nafasi ya kusoma pale, hivyo kama Ulikuwa mtoto wa Chifu na ukatimiza masharti walikuchukua Na Mlm.Nyerere ilitokea tu akawa Mtoto wa Chifu!
Wakoloni waliona kitu kwake na ndio maana walimpenda (labda) na kuamua kumuendeleza zaidi, kwa mategemeo kwamba wangemuhitaji baadae, na SI zaidi ya Hapo!
Kumbuka kwamba Waingereza tangu mwaka 1920 walikuwa wanajua kwamba mwisho wa siku ni lazima Waichie Nchi yetu, swala tu lilikuwa ni lini, waiache vipi na wamuacchie nani?
Hivyo kazi ya kutafuta mrithi ilianza muda tu na yeye Mlm.Nyerere, kutokana na juhudi zake yeye mwenyewe wakamuona, wakampenda, wakaanza kazi ya kumkuza na kumuandaa ili aje aendeleze ukoloni ila kwa namna nyingine, kitu ambacho leo hii tunakiona na hata tumekibatiza jina ukoloni mweusi!