Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 9,352
- 15,070
- Thread starter
- #41
Hiki ndiyo kilele cha kutokufikiri. Hiyo shule ya Tabora alisoma peke yake? Ulitaka Waingereza wasijjenge shule kwa ajili ya kuwaelimisha Waafrika? Hata leo serikali zote duniani zinaendelea kujenga shule na vyuo ili kusomesha vijana watakaoongoza nchi zao siku za usoni.
Tabora haifanani kwa vyovyote vile na Eton College.
Nyerere alipotoka Tabora Boys alikwenda Makerere ambayo ilikuwa ni College ya University of London na siyo Scotland(Edinburgh).
Inaelekea haujanielewa vizuri, Waingereza walijenga shule nyingi tu, ila hii ya Tabora ilikuwa ni Shule maalumu na ilijengwa kwa kufwata Model ya Eton College ya huko kwao, hilo wala usijaribu kulipinga, unaposema haifanani unamanisha nini?
Unaelewa maana ya "model"? Maana yake ni kwamba lengo la kuanzishwa kwa hiyo Shule (Tabora) ni kama lile lile la Eton College ambalo lilikuwa au kupika au kulea Viongozi wa wajao wa Taifa hilo ndilo lengo haswa.
Na hilo liko kila mahali na kama unabisha nenda Nyaraka za Taifa (National archives) pale Upanga na kasome historia yetu kila kitu kimeorodheshwa na kinatunzwa!
Sasa unataka kubisha Mlm.Nyerere hakusoma Scotland au? Au unataka kubisha kwamba alikutana na mambo ya ujamaa Scotland au? Au unataka kubisha kwamba Waingereza ndio walimpeleka kusoma Scotland? au unafikiri ni wazee wa Mkoa DSM ndio walimchangia kumpeleka Scotland?