Mwisho wa mapenzi

Mwisho wa mapenzi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
365,933
Reaction score
845,887
Ni majuto ni huzuni ni msiba inauma na kuumiza roho wengi imewatokea wengi inawatokea na wengi itawatokea ni wachache mno mno ambao hawajaumizwa kimapenzi. Wengi wamechukua maamuzi ya hovyo na ya kudhuru mwili kama kujiua na kuwa mlevi au malaya wa kupindukia
TAFAKARI HAYA
huyo anayekuumiza hukuzaliwa naye na hutakufa naye
wewe si wa kwanza kuumizwa na hutakuwa wa mwisho
Ichukulie hiyo hali kama ajali nyingine zozote
kwamba ni muda tu ndio utaponya majeraha ya mapenzi
Kwamba mwisho wa yote ni lazima maisha yaendelee
BASI FANYA HAYA
Usiwaze kupita kiasi kwakuwa huyo umuwazaye wala hana habari tena nawe
Jifunze kutambua kuwa maisha yamejaa maumivu ya kila aina
Mshukuru Mungu kwa kila jema
wakumbuke webgine wote wakupendae usiwahuzunishe kwa ajili ya mtu mmoja tu
kumbuka yote ya furaha
msiachane kwa visa kashfa na matusi italeta maumivu zaidi ya nafuu


ZIJAPOPITA NYAKATI ZA FURAHA USIHUZUNIKE BALI UFURAHI KWAKUWA ZILIKUWAKO...!
 
Hakuna apandaye hii moment ...!
 
TEMBEA NA SPEAR TYRE YA AKIBA ikipasuka tumia ile hata kama ni mchina or imezeeka ....
Lzima uwe na option b jman
 
Kazi ipo.
Kuna dogo mmoja alikuwa na mpenzi na walidumu kwa muda wa miaka 3

Siku ya siku yule binti akamuambia yule dogo kuwa anataka kwenda Dodoma kwa dada yake kupumzika [HAWAKUWA WANAISHI PAMOJA LAKINI NYUMBANI KWA DOGO NA BINTI PALIKUWA KARIBU KIASI KWAMBA WALIKUWA WANAONANA KILA SIKU] Dogo alimruhusu na binti alikwenda

Zikapita siku 5 na kijana akapata habari kuwa mpenziwe alikuwa hajaenda Dodoma bali alikuwa Igunga kwa jamaa mwingine na kijana aliamua kumpigia simu mpenziwe kumuuliza na binti alikubali na alimuambia kuwa amsahau

Kijana alitaharuki na kuanza kuchanganyikiwa na alikaa siku mbili bila kula na siku ya tatu alikunywa sumu,bahati nzuri siku anakunywa kaka yake alikuwa amekwenda kumtenbelea na kwa muda aliofika ilikuwa ni kama dakika 5 tu tangu dogo anywe sumu

Kaka mtu alipofika akamkuta dogo yupo kwenye harakati za mwanzo za kuhangaika huku akitoa maneno ya kujilaumu ni kwanini amekunywa sumu,kaka yake bila kupoteza muda aliomba maziwa kwa jirani na bahati nzuri yakapatikana na alimnywesha na wakamkimbiza hospital na alipatiwa huduma

Baada ya siku 5 kijana aliruhusiwa kutoka hospital na maisha yakaendelea

Baada ya miezi 6 dogo alipata Dem mkali kuliko yule wa mwanzo na dogo akawa anafurahia sana maisha yake ya kimapenzi kuliko mwanzo kwani haya alikuwa akiyasema mwenyewe

Lakini siku moja alisema wazi kuwa kitendo cha kunywa sumu anakiona kama kilikuwa ni kitendo cha kijinga kuliko vyote alivyowahi kuvifanya kwenye maisha yake na anajilaumu sana kwani anayafurahia maisha kuliko alivyokuwa na mpenzi wa mwanzo!
 
Back
Top Bottom