Mwisho wa Daudi Ballali

Mwisho wa Daudi Ballali

Upuuzi mtupu tutafanyana wajinga hadi lini?
Kwani kuwepo kwa kaburi lililoandikwa Ballali haimaanishi aliyezikwa humo ni yeye, kwa hili mnatufanya tuhisi kuna uchafu mwingi alifanya ambao serikari imeukalia . imeendelea
 
Muda ukiwadia ykweli utajizithiirisha tu.
Kwani kwa teknolojia iliyopo sasa ni jambo dogo sana kuweza kuthibitisha kama ndiye yeye balali au la aliyezikwa kwa kuchukua na kupima sampuli ya mabaki ya mwili wa marehemu hata kama ni mifupa tu ndio iliyosalia.
 
Waishio nje wakifia huko huwa miili yao inasafirishwa kuja kuzikwa nyumbani, au hata kama watazikwa huko, basi huwa hakunaga usiri kwenye mazishi na taratibu zake, toka mwanzo hadi mwisho... SEMBUSE GAVANA WA BoT.... Pelekeni hukooo uwongo wenu..

Mficheni tu, ila mjuwe huko aliko atazeeka na SIKU MOJA NAFSI ITAMSUTA NA ATAYASEMA YOTE.... time will tell

Some people think that the truth can be hidden with a little cover-up and decoration. But as time goes by, what is true is revealed, and what is fake fades away.
By Ismail Haniyeh
 
Yaani uwepo wa kaburi ndiyo uthibitisho wa kifo? Bado mimi siamini. Yawezekana kabisa kaeneo kalinunuliwa na kujengwa kinachoonekana hapo.Na mambo mengine yanaendelea.Kiukweli,suala la Balali lina maswali mengi kuliko majibu.

Hivi watanzania lini tutaacha kuwa watu wa ajabu .... mmeambiwa mtu kafa maana yake amekufa. Marekani hakuna shortcuts za kijinga na usanii kama Tanzania ... eti ooh kumejengewa jina tu, tutajuaje aliyezikwa hapo ni yeye, kwa nini azikwa marekani, etc ..... Kwa kifupi waulizeni ndugu au marafiki zenu walioko marekani ni nini kinatokea mtu akifa, hata kifo cha kawaida hampati mwili mpaka uchunguzi ufanyike. Maziko yenyewe si bei rahisi ndio maana kuna watu wanachomwa moto kwa kushindwa kupata gharama za maziko. Wageni wengi tu huzikwa marekani kwa hiyo Balali hakuwa wa kwanza na wala hatakua wa mwisho kuzikwa marekani! labda ndio yalikua maamuzi yake na mke wake. kwenye maamuzi kama hayo ya maziko Marekani anasikilizwa mtu mwenye power of attorney, kwa hiyo hata mje jumuia nzima tunataka kwenda mzika Tanzania lakini mke wake akaamua azikwe marekani maana yake ni atazikwa marekani...mke wake angesema achomwe moto, angechomwa moto. MAREKANI HUENDESHWA KWA SHERIA HAKUNA SHORTCUTS ZISIZO NA CONSEQUENCES!
 
Muda ukiwadia ykweli utajizithiirisha tu.
Kwani kwa teknolojia iliyopo sasa ni jambo dogo sana kuweza kuthibitisha kama ndiye yeye balali au la aliyezikwa kwa kuchukua na kupima sampuli ya mabaki ya mwili wa marehemu hata kama ni mifupa tu ndio iliyosalia.

Unywele tu unatosha kuthibitisha
 
Mkazi wa Kijiji la Luganga, Wilaya ya Mufindi, Iringa, alikozaliwa Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali analazimika kutumia saa 32 kufika katika kaburi la kiongozi huyo lililopo eneo la Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

Ndugu wa Ballali (pichani) wanaweza kutaka kwenda kuona kaburi la ndugu yao, kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawakuwahi kupata fursa ya kumzika Gavana huyo ambaye alikuwa kiongozi wa juu kabisa wa taasisi kubwa inayosimamia masuala ya fedha na uchumi wa nchi.

Mwandishi wa gazeti hili alisafiri kwa saa 24 kutoka Dar es Salaam hadi Washington, Marekani ambako alithibitisha pasi na shaka kwamba Ballali alizikwa Mei 21, 2008 katika makaburi ya Gate of Heaven, baada ya kufariki dunia akiwa nyumbani kwake Maryland, Mei 16, mwaka huo.

Safari hiyo ya siku kumi, ilianza Alhamisi Juni 26, 2014 hadi Jumapili, Julai 6. Mwandishi wa habari hizi aliligundua kaburi hilo baada ya kwenda makaburi ya Gate of Heaven kwa siku tatu mfululizo.

Siku ya kwanza, mwenyeji wa mwandishi ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa alimfikisha katika makaburi hayo, lakini kaburi la Ballali halikuonekana na hata mwandishi alipokwenda siku ya pili peke yake, kaburi hilo pia halikuonekana kwa kutokana na ukubwa wa eneo hilo.

Siku ya tatu, Mwandishi wa Mwananchi alilazimika kuomba msaada wa Ofisi ya Makaburi ya Gate of Heaven, ambayo ilimsadia kuonyesha eneo lilipo kaburi hilo, hivyo kuwezesha kupata picha zake.

Kaburi lake liko katika msitari wa mwisho kabisa na Ukanda wa Kijani wa miti iliyozunguka makaburi ya Gate of Heaven, likiwa limeandikwa jina la kiongozi huyo, pamoja na maneno ya Kiingereza yanayosomeka “When the heart weep for what it has lost, the soul rejoices for what it has found”.

Maana ya maneno hayo ni kwamba “wakati moyo ukiomboleza kwa kile kilichopotea, roho hufurahi kwa kile kilichopatikana”. Kaburi hili limezungukwa na makaburi mengine kadhaa ambayo si ya Watanzania, kwani kwa haraka kutokana na mazingira yalivyokuwa, Mwandishi wa Mwananchi hakuweza kuona kaburi jingine lenye majina yenye asili au kuwa na mwelekeo wa asili ya Tanzania.

Uthibitisho huu ni tofauti na hekaya za miaka nenda rudi zilizogubika kifo cha kiongozi huyo, ambaye tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani Agosti 2007, hakuwahi kurejea na badala yake zilisikika taarifa za kuugua kwake, kifo chake na baadaye mazishi yake yaliyokuwa ya siri kubwa yakiwahusisha ndugu wa karibu pekee.

Kutokana na mazingira hayo, kumekuwapo na uvumi kwamba Ballali hakufa na pengine amefichwa kusikojulikana, madai yanayochagizwa na mtu aliyejitokeza katika mitandao wa kijamii ya Twitter na facebook, akidai kwamba yeye ni Ballali na kwamba hajafa, huku akisisitiza kuwa wakati ukiwadia ukweli utafahamika.

Mtu huyo asiyefahamika hadi sasa alianza kujitokeza Twitter, Oktoba Mosi, 2012 pale aliposema “Nitakutana na Rais Kikwete (Jakaya) na ujumbe wake wiki hii hapa Marekani”. Mtu huyo alidai kwamba alikuja nchini Tanzania na kukaa karibu na Hoteli ya Hyatt Kempinski Kilimanjaro na baadaye kuondoka ghafla kwa kile alichokiita sababu za kiusalama.

Novemba 13 mwaka huo alituma ujumbe akisema:“In Dar es Salaam, Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kempinski Kilimanjaro Hotel. Feels good to be close to my former office, BoT,” akimaanisha kwamba niko Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, najisikia vizuri kuwa karibu na ofisi yangu ya zamani BoT.

Mtu huyo ambaye sasa tunaweza kuthibitisha kuwa ni feki amekuwa akiendelea kutuma ujumbe akijitambulisha kwa jina hilo la Ballali.

Ballali alifariki dunia kama ilivyotagazwa, lakini ilikuwaje akaenda safarini Washington, ugonjwa wake na hata kifo chake kilikuwaje? Je ndugu zake wanasemaje, safari ya kwenda Marekani ilikuwaje? Fuatilia mfululizo wa habari hii itakapoendelea kesho.

Source: Mwananchi

No comment
 
Alikimbia moto wa Dr.Slaa na Tundu Lissu.
 
Mmenikumbusha maigizo ambayo Mtuanakufa kesho unamwona mitaani uku kukiwa na maandishi alizaliwa lini na alikufa lini.
Hawa maigizo yamefadhiliwa na serikali na kuigizwa na Gazeti Mwananchi.
Wahusika CCM na Matajiri wa EPA
 
Maswali ni mengi....

balali.jpg


balali.jpg


Siku ya tatu, Mwandishi wa Mwananchi alilazimika kuomba msaada wa Ofisi ya Makaburi ya Gate of Heaven, ambayo ilimsadia kuonyesha eneo lilipo kaburi hilo, hivyo kuwezesha kupata picha zake.

Kaburi lake liko katika msitari wa mwisho kabisa na Ukanda wa Kijani wa miti iliyozunguka
makaburi ya Gate of Heaven,"

mbona kwenye picha kwenye kaburi moja tu, au ballali ndio mtu wa mwisho kuzikwa hapo.
nmepata mashaka sana na uhandishi wako unaobase upande mmoja ,halafu unauita wa kichunguzi.

yaani hata ndugu wa ballali hawajui kaburi la ndugu wao lilipo.
sorry hivi nauli ya kwenda huko alikulipia nani .?
 
Seriously?
Yan umeenda USA kutazama kaburi?
Halafu umeridhika kwamba aliyemo ndan ni Balal?
 
Nafurahi hii 'issue' kuibuliwa tena tunapoelekea 2015. Kama ilikuwa imesahaurika vile wakati halikuwa tukio la kawaida nchini. Mtatujibu vizuri ni kwa nini kifo chake mlikifanya usiri mkubwa....
 
Siku moja Serikali Makini itafukua mwili wa huyo anayehisiwa kuwa ni Ballali na kuufanyia DNA test, ili kutendea haki waTanzania na kuridhisha umma wa walipa kodi, as part of good governance. Huyu jamaa "alikufa" akiwa alleged kuwa criminal, kama wataruhusu fununu na bla bla hizi ziendelee, they are setting a very bad precedence!
 
Kwamba mtu aliyekuwa na hadhi ya Gavana wa Benki Kuu anafariki Marekani halafu hata maofisa wa Ubalozi wetu,wawakilishi wetu katika mashirika makubwa ya kifedha yaliyoko US wote wanashindwa kuhudhuria hata kwa uchache wao?
Hata mchawi hakosi mtu wa kumzika na kuwadhibitishia watu kuwa huyo mtu kafa na kuzikwa.
Mwandishi kutueleza kaona kaburi limeandikwa jina eti ndio anakuja kutuambia ni habari za uchunguzi? Basi angeanzia uchunguzi wake katika historia ya matibabu,daktari aliye saini hati ya kifo na mengineyo angeonyesha kweli kafanya kazi.
Watu wangapi wanaokotwa wamekufa na majina yao hayafahamiki? Akizikwa na mkaamua kulipa jina hilo kaburi mfano MSALANI bin so and so hivyo itakuwa yule aliyepo humo ni huyo mwenye jina wakati MSALANI yupo Lumumba anaendelea kutupia post JF na anavuta mpango wake wa buk7 bila wasiwasi?


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mie nasubiri Mzee Mamvi wamnyime kuwakilisha Ccm ktk nafasi ya urais ili amlete Ballali make anajua aliko!!
 
Upuuzi mtupu tutafanyana wajinga hadi lini?
Kwani kuwepo kwa kaburi lililoandikwa Ballali haimaanishi aliyezikwa humo ni yeye, kwa hili mnatufanya tuhisi kuna uchafu mwingi alifanya ambao serikari imeukalia . imeendelea

Kama unajua alipo toa taarifa mkuu.
 
Back
Top Bottom