Mwingira amlaani mchungaji Loliondo

semmy samson

Member
Dec 20, 2010
85
0
Jamani huu ni wivu wa kiimani au nini wadau?...huyu Mtu kumuonea wivu Babu anamaana gani. hebu ichekini hii taarifa ilyoandikwa na
Elizabeth Suleyman gazeti la mwnanchi....15 march 2011

Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha amemuombea mabaya Mchungaji Ambikile Mwasapile anayetoa tiba ya magonjwa sugu katika eneo la Samunge, Loliondo kwamba anapaswa kulaaniwa hadi kufa kutokana na kutoa huduma hiyo.

Mwingira alisema hayo katika mahubiri ya ibada ya Jumapili aliyoyatoa katika Makao Makuu ya Kanisa hilo lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam. “Imeandikwa katika Biblia kwamba,ukipewa bure nawe toa bure. Iweje yeye anauza dawa hiyo, ikiwa Mungu amesema aponye watu. Hakuna sababu ya kuwatoza fedha yoyote wagonjwa.

“Hizi ni roho za kishetani zinazotaka kuwaangusha walio wengi ambao hawamjui Yesu Kristo kwani haiwezekani mtu atumiwe na Mungu halafu hata siku moja asimtaje Yesu. Asitumie Biblia hata kuwahubiria watu wamtumaini muumba wao,”alisema Mwingira.

Mwingira alisema huduma hiyo ni uongo na kwamba haina tofauti na Deci iliyokuja kiujanja ujanja na kuteka watu wengi baadaye walijutia maamuzi yao. “Kama mpakwa mafuta wa Bwana niliyeitwa kwa kusudi lake.
Nailaani Loliondo ife pamoja na Mchungaji wake na itoweke kama Deci ilivyotoweka,” alisema Mwingira. Mwingira alisema Mchungaji Mwasapile ni mwongo, anataka kuwadanganya watu na kuwapoteza kiimani.

Alisema kama alivyoilaani Deci na ikafa, anailaani huduma ya Loliondo ili ife kwa kuwa mchungaji huyo ni roho ipotezayo, inayotaka kuwateka watu walioko gizani na kuwaangamiza. Alisema baadhi ya viongozi tayari wamepigwa ngwara na roho hiyo na kunywa dawa, bila wao kujijua.
“Sitakubali kuendelea kuona roho hiyo ikipoteza watu. Nailaani itoweke Loliondo na iangamie kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,”alisisitiza. Mwingira alisema haiwezekani kwa mtu aliyeitwa na Mungu kuwahudumia watu wake, baadhi ya watu hao wafe kwenye huduma yake.

“Ni wagonjwa wangapi wamepelekwa kule na wengine wamefariki nyumbani kwake kabisa na wengine njiani, je mlishawahi kujiuliza? alihoji Mwingira. Mwingira alitoa kauli hiyo siku chache baada Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kulieleza gazeti hili:"Miujiza haiji kwa urahisi hivyo na watu kuponya kiasi hicho, huenda wanaweza kuponywa kwa ‘Illusion’ na baade ikaleta madhara."

Alisema cha msingi watu wanapaswa kuwa makini na serikali pia kwa sababu, wingi wa watu kuponywa huenda baadaye ukaleta vifo vingi zaidi kutokana na dawa yenyewe.

Pengo alisema: “Ninachoamini miujiza haiji kwa urahisi na watu wakaponywa kiasi hicho kwa mara moja, huenda ikawa ni kuponya kwa ‘illusion’ na baadae watu wakapata madhara makubwa.

“Ila sina jibu la kutoa kuhusu uponyaji huo, nabaki tu kushangaa nayayotendeka kwa Mchungaji huyo hadi kufikia watu kuamini kiasi hicho,”alisema. Pengo alisema huenda akawa ameamua kutumia njia hiyo akawavuta hata wa waumini waingie kwenye imani yake na kuacha dini zao.
 
Jamani huu ni wivu wa kiimani au nini wadau?...huyu Mtu kumuonea wivu Babu anamaana gani. hebu ichekini hii taarifa ilyoandikwa na
Elizabeth Suleyman gazeti la mwnanchi....15 march 2011

Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha amemuombea mabaya Mchungaji Ambikile Mwasapile anayetoa tiba ya magonjwa sugu katika eneo la Samunge, Loliondo kwamba anapaswa kulaaniwa hadi kufa kutokana na kutoa huduma hiyo.

Mwingira alisema hayo katika mahubiri ya ibada ya Jumapili aliyoyatoa katika Makao Makuu ya Kanisa hilo lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam. “Imeandikwa katika Biblia kwamba,ukipewa bure nawe toa bure. Iweje yeye anauza dawa hiyo, ikiwa Mungu amesema aponye watu. Hakuna sababu ya kuwatoza fedha yoyote wagonjwa.

“Hizi ni roho za kishetani zinazotaka kuwaangusha walio wengi ambao hawamjui Yesu Kristo kwani haiwezekani mtu atumiwe na Mungu halafu hata siku moja asimtaje Yesu. Asitumie Biblia hata kuwahubiria watu wamtumaini muumba wao,”alisema Mwingira.

Mwingira alisema huduma hiyo ni uongo na kwamba haina tofauti na Deci iliyokuja kiujanja ujanja na kuteka watu wengi baadaye walijutia maamuzi yao. “Kama mpakwa mafuta wa Bwana niliyeitwa kwa kusudi lake.
Nailaani Loliondo ife pamoja na Mchungaji wake na itoweke kama Deci ilivyotoweka,” alisema Mwingira. Mwingira alisema Mchungaji Mwasapile ni mwongo, anataka kuwadanganya watu na kuwapoteza kiimani.

Alisema kama alivyoilaani Deci na ikafa, anailaani huduma ya Loliondo ili ife kwa kuwa mchungaji huyo ni roho ipotezayo, inayotaka kuwateka watu walioko gizani na kuwaangamiza. Alisema baadhi ya viongozi tayari wamepigwa ngwara na roho hiyo na kunywa dawa, bila wao kujijua.
“Sitakubali kuendelea kuona roho hiyo ikipoteza watu. Nailaani itoweke Loliondo na iangamie kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,”alisisitiza. Mwingira alisema haiwezekani kwa mtu aliyeitwa na Mungu kuwahudumia watu wake, baadhi ya watu hao wafe kwenye huduma yake.

“Ni wagonjwa wangapi wamepelekwa kule na wengine wamefariki nyumbani kwake kabisa na wengine njiani, je mlishawahi kujiuliza? alihoji Mwingira. Mwingira alitoa kauli hiyo siku chache baada Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kulieleza gazeti hili:"Miujiza haiji kwa urahisi hivyo na watu kuponya kiasi hicho, huenda wanaweza kuponywa kwa ‘Illusion’ na baade ikaleta madhara."

Alisema cha msingi watu wanapaswa kuwa makini na serikali pia kwa sababu, wingi wa watu kuponywa huenda baadaye ukaleta vifo vingi zaidi kutokana na dawa yenyewe.

Pengo alisema: “Ninachoamini miujiza haiji kwa urahisi na watu wakaponywa kiasi hicho kwa mara moja, huenda ikawa ni kuponya kwa ‘illusion’ na baadae watu wakapata madhara makubwa.

“Ila sina jibu la kutoa kuhusu uponyaji huo, nabaki tu kushangaa nayayotendeka kwa Mchungaji huyo hadi kufikia watu kuamini kiasi hicho,”alisema. Pengo alisema huenda akawa ameamua kutumia njia hiyo akawavuta hata wa waumini waingie kwenye imani yake na kuacha dini zao.

wamepoteza waumini wao maana wamekwenda kuponya kwa babu baada ya wao kushindwa kuwaponya. "Maslahi binafsi" wala si ujumbe wa mungu. Mbona mwingira na kakobe hulazimisha waumini wao kutoa fedha na vito vya thamani-sasa tuseme nao wanafanya baishara??? Mungu humbariki yeye ajishushaye kama babu-shs 500 tu (200 kanisa, 200 wasaidizi kushughulikia madawa; na 100 babu). Mungu bariki hudumu hii ya maajabu uliyotushushia kupitia kwa babu ili watu wote ulimwenguni wenye magonjwa sugu waponywe.
 
wamepoteza waumini wao maana wamekwenda kuponya kwa babu baada ya wao kushindwa kuwaponya. "Maslahi binafsi" wala si ujumbe wa mungu. Mbona mwingira na kakobe hulazimisha waumini wao kutoa fedha na vito vya thamani-sasa tuseme nao wanafanya baishara??? Mungu humbariki yeye ajishushaye kama babu-shs 500 tu (200 kanisa, 200 wasaidizi kushughulikia madawa; na 100 babu). Mungu bariki hudumu hii ya maajabu uliyotushushia kupitia kwa babu ili watu wote ulimwenguni wenye magonjwa sugu waponywe.

Ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeen
 
Jamani huu ni wivu wa kiimani au nini wadau?...huyu Mtu kumuonea wivu Babu anamaana gani. hebu ichekini hii taarifa ilyoandikwa na
Elizabeth Suleyman gazeti la mwnanchi....15 march 2011

Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha amemuombea mabaya Mchungaji Ambikile Mwasapile anayetoa tiba ya magonjwa sugu katika eneo la Samunge, Loliondo kwamba anapaswa kulaaniwa hadi kufa kutokana na kutoa huduma hiyo.

Mwingira alisema hayo katika mahubiri ya ibada ya Jumapili aliyoyatoa katika Makao Makuu ya Kanisa hilo lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam. "Imeandikwa katika Biblia kwamba,ukipewa bure nawe toa bure. Iweje yeye anauza dawa hiyo, ikiwa Mungu amesema aponye watu. Hakuna sababu ya kuwatoza fedha yoyote wagonjwa.

"Hizi ni roho za kishetani zinazotaka kuwaangusha walio wengi ambao hawamjui Yesu Kristo kwani haiwezekani mtu atumiwe na Mungu halafu hata siku moja asimtaje Yesu. Asitumie Biblia hata kuwahubiria watu wamtumaini muumba wao,"alisema Mwingira.

Mwingira alisema huduma hiyo ni uongo na kwamba haina tofauti na Deci iliyokuja kiujanja ujanja na kuteka watu wengi baadaye walijutia maamuzi yao. "Kama mpakwa mafuta wa Bwana niliyeitwa kwa kusudi lake.
Nailaani Loliondo ife pamoja na Mchungaji wake na itoweke kama Deci ilivyotoweka," alisema Mwingira. Mwingira alisema Mchungaji Mwasapile ni mwongo, anataka kuwadanganya watu na kuwapoteza kiimani.

Alisema kama alivyoilaani Deci na ikafa, anailaani huduma ya Loliondo ili ife kwa kuwa mchungaji huyo ni roho ipotezayo, inayotaka kuwateka watu walioko gizani na kuwaangamiza. Alisema baadhi ya viongozi tayari wamepigwa ngwara na roho hiyo na kunywa dawa, bila wao kujijua.
"Sitakubali kuendelea kuona roho hiyo ikipoteza watu. Nailaani itoweke Loliondo na iangamie kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,"alisisitiza. Mwingira alisema haiwezekani kwa mtu aliyeitwa na Mungu kuwahudumia watu wake, baadhi ya watu hao wafe kwenye huduma yake.

"Ni wagonjwa wangapi wamepelekwa kule na wengine wamefariki nyumbani kwake kabisa na wengine njiani, je mlishawahi kujiuliza? alihoji Mwingira. Mwingira alitoa kauli hiyo siku chache baada Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kulieleza gazeti hili:"Miujiza haiji kwa urahisi hivyo na watu kuponya kiasi hicho, huenda wanaweza kuponywa kwa ‘Illusion' na baade ikaleta madhara."

Alisema cha msingi watu wanapaswa kuwa makini na serikali pia kwa sababu, wingi wa watu kuponywa huenda baadaye ukaleta vifo vingi zaidi kutokana na dawa yenyewe.

Pengo alisema: "Ninachoamini miujiza haiji kwa urahisi na watu wakaponywa kiasi hicho kwa mara moja, huenda ikawa ni kuponya kwa ‘illusion' na baadae watu wakapata madhara makubwa.

"Ila sina jibu la kutoa kuhusu uponyaji huo, nabaki tu kushangaa nayayotendeka kwa Mchungaji huyo hadi kufikia watu kuamini kiasi hicho,"alisema. Pengo alisema huenda akawa ameamua kutumia njia hiyo akawavuta hata wa waumini waingie kwenye imani yake na kuacha dini zao.

Sikuhizi hadi viongozi wa dini wasanii... ! inamaana DECI ilikufa kutokana na Laana Zake!! ??? nampongeza Pengo at last ameongea kitu maneno ya maana yanayofaa kuongelewa na mtu kama yeye! aendelee hivohivo , siasa hazimfai zinamshushia hadhi kwa kuongea pumba
 
Bac yeye ndio balaa anamilki hadi benki kavuna kutoka huduma ya mungu.
Conflict of interest wanashindwa kuvumilia
 
Bac yeye ndio balaa anamilki hadi benki kavuna kutoka huduma ya mungu.
Conflict of interest wanashindwa kuvumilia

nakubaliana na wewe mkuu! This is typical conflict of interest. Huyo jamaa aliipinga Dec sababu ana benk na waumini walianza kuikacha na kukimbilia huko. Sasa amemrudia Babu. Watu tumechoka na usanii wa makanisa yao. Watu wamepeleka ndugu zao loliondo wakapona, wamerudi tuwewaona kwa macho yetu waliokuwa na kisukari wanakunywa chai, soda nk. Kwann tusimwamini babu. Hata Tomaso aliamini baada ya kuona! Kama ni nabii awaponye ndugu zetu tutamfuata! Aache usanii wa kuchukua mtu chanika anakuja kujifanya kapona wakati mwenge yenyewe hakuna aliyepona!!?.
 
huyu Mwingira kwa mamlaka gani anajiita Mtume na Nabii?Japo i dont support 'mizizi' ya babu,but for this ill side with him.Hawa Manabii na maaskofu uchwara wamezidi sasa,duuh..bora miye sina dini
 
sio wivu hayo yanayosemwa yana ukweli kabisa.
watu wengi kwa sasa wamekuwa vipofu hawasikii hawaelezwi,il nakwambia madhala yake yatajulikana baadaye kama sio kazi ya Mungu.
Kama ni Mungu basi itadumu.
Mwingira na Kakobe wana wivu wa KIJINGA. Atalaaniwa yeye, maalun mkubwa
 
That who Jah blessed,no one curse,hakuna cha babu kulaaniwa wala loliondo kuanguka,hawa wachungaji wanawivu wa kijinga,na amin nawaambieni wanaweza kwenda kutafuta uchawi ili wamuondoshe huyu babu yetu,lakini hawatafanikiwa na loliondo itasimama imara,mbona waoa kwenye huduma zao sadaka wanaitilia kipaumbele,na hizo ndizo zinazo wanunulia magari na majumba ya kifahari,angalia hali zao za kimaisha kabla ya kuanzisha makanisa na hivi sasa,ni tofauti kubwa sana,wameshafanya vichwa vya watu mitaji,na huyu babu ni mtoa huduma na anafamilia,kibinadamu haiwezekani awahudumie watu bure na wakati anawasaidizi na familia inayomzunguka,tumchangie babu yetu na tuzidi kumuombea kwa Mungu!!
 
wamepoteza waumini wao maana wamekwenda kuponya kwa babu baada ya wao kushindwa kuwaponya. "Maslahi binafsi" wala si ujumbe wa mungu. Mbona mwingira na kakobe hulazimisha waumini wao kutoa fedha na vito vya thamani-sasa tuseme nao wanafanya baishara??? Mungu humbariki yeye ajishushaye kama babu-shs 500 tu (200 kanisa, 200 wasaidizi kushughulikia madawa; na 100 babu). Mungu bariki hudumu hii ya maajabu uliyotushushia kupitia kwa babu ili watu wote ulimwenguni wenye magonjwa sugu waponywe.

Taratibu mkuu, je anayeposnya ni Mungu au Babu??
hapo ndio kuna kuwa na tatizo na hiyo imani, huyo babau kama angetumia Jina la Yesu katika huo uponyaji wake nadhani kusingekuwa na mtu yeyote kuwa na shaka na huduma yake.Yeye anatumia mitishamba kama mganga wa kienyeji anavyofanya bila ya maombi wala kumtaja aliyemwezesha, je huyo ni Mungu kweli??
Alisema kila mlifanyalo basi fanayeni kwa kumtanguliza yeye,muombe kwa jina langu nami nitawafanyia.
 
sio wivu hayo yanayosemwa yana ukweli kabisa.
watu wengi kwa sasa wamekuwa vipofu hawasikii hawaelezwi,il nakwambia madhala yake yatajulikana baadaye kama sio kazi ya Mungu.
Kama ni Mungu basi itadumu.
Unajua tatizo ni kwamba hata huduma za hao wachungaji wengine tunazitilia mashaka,kwani siku hizi zipo dini zinazomtaja Mungu lakini zinaongozwa na mashetani,katika mengi ya haya makanisa ya siku hizi uponyaji hupatikana kwa yule ambaye atakuwa tayari kujiunga na kanisa husika,yaani hata ukipata uponyaji ,watakubembeleza ujiunge na kanisa hilo,lakini kwa babu ni Drink and Go!!!
 
Wote wanaompinga mchungaji walaaniwe wafe wao. Sitaki mtu ampinge ili yeye ndo abaki maarufu! Babu wa ukweli,mi sina imani/yan dini yake lakini kutokea ktk imani yangu namuombea babu aendeleze utabibu huo. Enzi za mitume miujiza hii ilikuwepo,si ajabu ikirudi!
 
Back
Top Bottom