Mwijaku alishindwa nini kununua kiwanja kinachoendana na mipango yake ya ujenzi? Kampuni ya ujenzi ilishindwa kumshauri?

Naungana na wewe na kusisitiza yafuatayo. Vijana wa sasa hata waze tunatakiwa kubadilika. Kujenga majumba makubwa sio ufahari. Mwisho wake huwa hayatumiki. Nenda mbezi beach kuna mijengo inaota nyasi na kupangishwa kwa hela ndogo ili walao kuwe na watu ndani.
Kama kweli katumia 1.2bn (ingawa siamini). Angeweka fedha hizo benki angepata 120m kila mwaka. Angewaambia benki kwa miaka 3. Badala ya kumpa 360m wampe 300m tu. Angejenga nyumba nzuri sana kwa 300m. Tena kwa kununua kiwanja kizuri sana kwa 100m. Nyumba ingekamilika. 1.2bn ingebaki palepale benki na yumba angepata.

Si hivyo tu. Angejenga hoteli imzalishie. Vijana wa sasa tubadilike. Kufukia 1.2bn kwa nyumba ya kuishi ni ufahari wa muda tu.
Kwa nyumba hiyo umeme ni 300,000 kwa mwezi. Mengine je.
Mkuu bado unaamini ile nyumba ya Mwijaku ni 1.3 B?

Ile nyumba hata 200 milioni haifiki..
Usibabaishwe na marangi pamoja na swimming pool juu ya paa.
 
Watanzania tunapaswa kubadili mawazo na fikra zetu hasa katika kufukia fedha kwenye ujenzi. Tuna watu wengi wanakosea kujenga kwa kukosa mawazo sahihi au exposure. Tafsi ya nyumba siyo mpangilio wa tofali bali ni muunganiko wa ramani na mazingira ya nje.

Viwanja vya masaki na osterbay vinaweza kuwa kielelezo cha fikra za ujenzi zinavyotakiwa kuwa. Alichofanya mwijaku na kampuni aliyowapa kazi ni aibu kwa karne hii.

Unapoweka malengo yakujenga nyumba hasa ghorofa unapaswa kuanza kuwaza kiwanja, eneo kiwanja kilipo na majirani wanaokuzunguka.

Unapotenga bilion moja ya ujenzi tunategemea kiwanja kitengeewe si chini ya milioni mia na hamsini endapo unataka kupata kiwanja mjini. Jengo la bilioni moja kibongo bongo linapaswa kujengwa kwenye eneo la heka moja endapo utajenga kigamboni ambapo maeneo ni makubwa.

Waliomshauri na kumjengea Mwijaku ndio washauri wa NHC, ambao wanajenga nyumba Tanzania kwenye kiwanja cha Sqmt 200 au 400 kwenye jiji kama Dodoma ambalo linakuwa . Poverty mentality ya wataalam wa ardhi wa nchi imepelekea watu kujenga kwa gharama kubwa lakini hawana uwezo wakupaki magari ishirini au kuwaalika marafiki nyumbani. Unakuwa na nyumba kama ya mwijaku lakini ukialika marafiki mia kuja kwako unalazimika ukatafute ukumbi. Leo Mwijaku akitazama chini akiwa ghorofani anawachungulia majirani.

Nyumba kama ile ingejengwa kwenye eneo sahihi hata wafanyakazi wenzake wangetuonyesha garden ya nje na wangepiga picha hata mandhari ya kwenda kwa huyu mjuba.

Nakubali kwamba tunanunua viwanja tukiwa hatujui tunajenga nini ila tunapochora ramani ya nyumba kama ile tutafute kiwanja. Alishindwa nini kwenda kujenga mbweni huko au bagamoyo ?

Nampongeza na niwapongeze wote wenye maono kama yake ila tubadili fikra tuje na maeneo ya uzunguni ambapo tukitaka kutembelea tunakuta miundombinu hata ya usalama ipo sawa.

Povu lazima
Nyie wanawake mna kazi sana. Wivu husuda na kijicho. Halafu unaandika kama sisi wote tunamfahamu huyo mwidaku. Hapo utakuta mmechukuliana mabwana sasa ndo manaanza leta habari hizo JF
 
Kwani higo 1.2b unadhani alikuwa nayo bank au ni hesabu baada ya kumaliza ujenzi
Alikuwa anadunduliza na kuitupa kwenye ujenzi. Hata msukuma mkojoteni anaweza kujenga nyumba ya milioni 30 kwa kudunduliza halafu mtanzania ataanza kumkosoa kwamba aah hiyo hela ungefungua hardware. Hivi wanafahamu maana ya kudunduliza hawa watu??
 
Webongo wengi ukiwashauri utasikia we unayo, mchawi, wivu nk. Hawawezi kupokea ushauri au challenge kama watu wazima. Bado wabongo wengi wana akili za kitoto. Namaanisha wabongo wengi wamekomaa miili ila akili zao wengi za kitoto.
 
Mkuu bado unaamini ile nyumba ya Mwijaku ni 1.3 B?

Ile nyumba hata 200 milioni haifiki..
Usibabaishwe na marangi pamoja na swimming pool juu ya paa.
Mkuu Ila na wewe umeshusha sana, haifiki 200M???. Hivi gharama ya nyumba huwa hihusishi na thamani ya kiwanja?

Mtu akisema katumika bil.1 siyo kwamba anajumlisha gharama ya ujenzi wa jengo na ununuzi wa kiwanja?
 
Mnapojadili hii mada wekeni kwenye mbongo then maneno Great thinkers ; jukwaa limeandaliwa kwa ajili ya kujadili hoja siyo kusifu na kupeana moyo.

Kama huna uwezo wakufahamu nafasi ya bilioni moja kwenye ujenzi usijitutumue kujadili kwa sababu tu unataka kusema; katika ujenzi Ile nyumba ya Mwijaku haina thamani ya bilioni moja na milioni mia tatu.

Lakini kwa upande wa pili hoja hapa siyo thamani ya nyumba, ni kiwanja na eneo alipojenga. Tukubali kwamba huyu kakosea kujenga, alipaswa kujenga nyumba kwenye eneo ambalo limepimwa na lina nafasi ya kupata oxygen.

Lakini pia ifahamike hapa hatupo kumshauri Mwijaku, tupo kuwashauri wengine wanaotamani kujenga.....tunawafumbua macho.

Jambo jingine ambalo wasanii wanapaswa kulizingatia kwa huko tuendako ni utajiri unaoendana na uwezo wa kulipa kodi. Mwijaku angetamka 1.3 bilioni kwenye nchi zilizoendelea hoja ingekuwa anapata wapi hizi fedha? Analipa kodi kutokana na faida ya mapato yake? Kibongo bongo hakuna mtu anayejali analysis ya kodi za nchi na ndiyo maana hatuna tatizo na kutaja figure kubwa.

Kwa wale tunaopanga kujenga lazima tujione kwenye nafasi hiyo. Wapo wanasiasa wengi na watumishi wa umma wamekimbia majumba yao na makazi yao baada ya kuteuliwa kwa sababu walishindwa kujipanga wajenge wapi kabla yakupewa madaraka.

Tununue maviwanja siyo viwanja
 
Kama amejenga ni jambo jema sana wacha life liendelee maana hata asingejenga still angeendelea kulala ndani na si nje...
 
Back
Top Bottom