Mwigulu: Tunataka kero ikifika ofisi ya serikali ipatiwe ufumbuzi, wanaopuuza watatolewa kazini

Mwigulu: Tunataka kero ikifika ofisi ya serikali ipatiwe ufumbuzi, wanaopuuza watatolewa kazini

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza katika mkutano na madereva pikipiki, bajaji na machinga wote leo Januari 8, 2026 katika ukumbi wa Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, amesema serikali inataka wananchi wanapofikisha kero zao katika Ofisi za serikali zipatiwe ufumbuzi akisisitiza kuwa itafika hatua watumishi wanaopuza kero za wananchi watafukuzwa kazi wakiunganishwa na wanyanganyi akiwataka maafisa wa serikali kutambua kuwa wapo katika nafasi hizo kwa ajili ya wananchi

Amesema hayo katika mkutano na madereva pikipiki, bajaji na machinga wote Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa kimataifa Julius Nyerere leo Januari 8, 2026


 
JPM tu ndo aliweza hilo sidhani kama atatokea mwingine tena.
 
Serikali haramu iliyoshindwa kuwajibika inawaajibisha wengine. Nonsense.
 
KAZA BUTI DR MWIGULU UNAKAZI NGUMU MFUPA ULIOMSHINDA FISI HUO...HAKIKISHA HUCHEKI NA KIMA AU NYANI..LAKIN NAWEWE UJITIZAME...KILA LA HERI...PITIA POTE UMEME HAPA MIKOA YA PENDEZONI UMEME NI SHIDA, MAJI, AFYA, AJIRA ZA MCHONGO, ELIMU, MIUNDOMBINU,MIRADI, KILIMO, BIASHARA, MAZINGIRA, ARDHI, MIFUGO..NA UPANDISHAJI WA BEI KIHOLELA KUANZIA CHAKULA MPAKA VITU VINGINE..MAMBO NI MENGI, MENGI MENGI KAZI UNAYO.
 
Huu ndio unafiki na utapeli katika siasa.

Kabla ya uchaguzi, kuna watu binafsi, wazee wa hekima, taasisi za dini, vyama vya siasa, vilolalamikia uwepo wa tume fake ya kusimamia uchaguzi, walilalamikia ushetani wa kuteka na kuua watu, walilalamikia sheria na kanuni mbaya za uchaguzi, baada ya watu wengi kuuawa na UVCCM, kmkm na polisi, watu mbalimbali wameomba na kushauri ndugu wa marehemu warudishiwe miili ya marehemu; kuna lipi liliwahi kushughulikiwa?? Halafu leo huyu shetani anakuja na kauli eti serikali itasikiliza na kushughulikia kero za wananchi!!

Kwa hiyo amewaona bodaboda na waendesha bajaji ndiyo kundi la wasio na akili, analoweza kulifanyia utapeli wa kisiasa!

Wananchi, akija kiongozi tapeli mwenye kuongea upuuzi, anngalao mzomeeni.
 
Back
Top Bottom