idoyo
JF-Expert Member
- Jan 13, 2013
- 3,051
- 1,423
Kwanza nikupongeze kwa hotuba nzuri uloitoa kizalendo kabisa pale Dodoma, makao makuu ya serikali na chama (kama ulivyojipambanua). Ukasema pia utakapokuwa rais serikali itakuwa tayari imehamia Dodoma, wimbo ulioimbwa miaka zaidi ya 40. Mabadiliko ni Vitendo, Wakati ni Sasa!
Tuyaache hayo, turudi kwenye wasifu wako ulokuwa unasomwa kabla ya wewe kufika kwenye ukumbi wa Mwl. Nyerere. Katika moja ya sifa zako ni utashi na kipaji ulivyokuwa navyo tangu utotoni; kati ya watoto sita kwenye familia yenu, wewe ulikuwa mdogo lakini uliweza kuongoza ndugu zako kwa ustadi kabisa (kwa mujibu wa wazazi wako). Ni kipaji cha kujivunia sana, Masha'Allah! Kiongozi wa hivyo ni hazina kubwa katika taifa.
Kisha, katika wasifu huo, ikaelezwa ulipokuwa sekondari (kidato cha tatu) ulikuwa kiongozi mkuu (tuseme kaka mkuu, au rais wa serikali ya wanafunzi). Bila shaka shule inayosemwa hapa ni Iliboru (kwa mujibu wa wasifu-kazi wako). Ulipata nafasi hiyo baada ya aliyekuwa kaka mkuu kuachia ngazi miezi miwili tu baada ya kuchaguliwa na kupelekea waalimu kukuchagua wewe kuongoza shule. Uliongoza kwa ustadi wa juu sana, ukapendwa pia na wakubwa zako hasa wa kidato cha tano na sita, na baadaye ukatunukiwa cheti cha uongozi bora. Hongera sana!
Ikaelezwa pia ulipohitimu shahada ya kwanza ya Uchumi (BA Economics) ya chuo kikuu cha Dar es Salaam uliongoza kwa kupata alama ya juu kabisa (highest GPA) na kupelekea kupata udhamini wa masomo ya shahada ya uzamili (masters) kutoka BoT. Inafaamika kwamba unapofaulu kwa kiwango cha juu kabisa pale UDSM utapatiwa udhamini wa kuendelea na masomo kutoka BoT, Chuo, au mashirika mengine (nina uzoefu na Idara ya Uchumi). Na ukimaliza 'masters' uhakika wa kazi ni 300%; eidha BoT wakuchukue, kwa kuwa wamekusomesha (hawawezi wakapoteza pesa kukudhamini, halafu umalize ukose ajira), au Wizara ya Fedha, au Chuo (kupitia idara husika) kikuajiri kuwa mkufunzi na baadaye mhadhiri kabisa.
Sasa ndugu yangu Mwigulu Nchemba, kwenye hotuba yako ukasema unajua tatizo la ajira kwa kuwa una uzoefu nalo, eti ulipomaliza 'degree' ya pili ulienda kubeba zege! kheeee, were you serious? au ndiyo kufanya mzaha na vijana wasio na ajira? Eti mkeo akawa mama lishe na wewe ukawa mbeba zege! BoT walikusomesha ya nini? Kwenye wasifu-kazi wako inaonesha mwaka 2006 ulipomaliza 'masters' ulienda BoT na kuwa Mchumi I mpaka 2010 ulipoamua kugombea ubunge. Sasa, hilo suala la kubeba zege limetoka wapi? umewadanganya watazania? Kama ndivyo, uombe radhi basi! Au ufafanue!
Tuyaache hayo, turudi kwenye wasifu wako ulokuwa unasomwa kabla ya wewe kufika kwenye ukumbi wa Mwl. Nyerere. Katika moja ya sifa zako ni utashi na kipaji ulivyokuwa navyo tangu utotoni; kati ya watoto sita kwenye familia yenu, wewe ulikuwa mdogo lakini uliweza kuongoza ndugu zako kwa ustadi kabisa (kwa mujibu wa wazazi wako). Ni kipaji cha kujivunia sana, Masha'Allah! Kiongozi wa hivyo ni hazina kubwa katika taifa.
Kisha, katika wasifu huo, ikaelezwa ulipokuwa sekondari (kidato cha tatu) ulikuwa kiongozi mkuu (tuseme kaka mkuu, au rais wa serikali ya wanafunzi). Bila shaka shule inayosemwa hapa ni Iliboru (kwa mujibu wa wasifu-kazi wako). Ulipata nafasi hiyo baada ya aliyekuwa kaka mkuu kuachia ngazi miezi miwili tu baada ya kuchaguliwa na kupelekea waalimu kukuchagua wewe kuongoza shule. Uliongoza kwa ustadi wa juu sana, ukapendwa pia na wakubwa zako hasa wa kidato cha tano na sita, na baadaye ukatunukiwa cheti cha uongozi bora. Hongera sana!
Ikaelezwa pia ulipohitimu shahada ya kwanza ya Uchumi (BA Economics) ya chuo kikuu cha Dar es Salaam uliongoza kwa kupata alama ya juu kabisa (highest GPA) na kupelekea kupata udhamini wa masomo ya shahada ya uzamili (masters) kutoka BoT. Inafaamika kwamba unapofaulu kwa kiwango cha juu kabisa pale UDSM utapatiwa udhamini wa kuendelea na masomo kutoka BoT, Chuo, au mashirika mengine (nina uzoefu na Idara ya Uchumi). Na ukimaliza 'masters' uhakika wa kazi ni 300%; eidha BoT wakuchukue, kwa kuwa wamekusomesha (hawawezi wakapoteza pesa kukudhamini, halafu umalize ukose ajira), au Wizara ya Fedha, au Chuo (kupitia idara husika) kikuajiri kuwa mkufunzi na baadaye mhadhiri kabisa.
Sasa ndugu yangu Mwigulu Nchemba, kwenye hotuba yako ukasema unajua tatizo la ajira kwa kuwa una uzoefu nalo, eti ulipomaliza 'degree' ya pili ulienda kubeba zege! kheeee, were you serious? au ndiyo kufanya mzaha na vijana wasio na ajira? Eti mkeo akawa mama lishe na wewe ukawa mbeba zege! BoT walikusomesha ya nini? Kwenye wasifu-kazi wako inaonesha mwaka 2006 ulipomaliza 'masters' ulienda BoT na kuwa Mchumi I mpaka 2010 ulipoamua kugombea ubunge. Sasa, hilo suala la kubeba zege limetoka wapi? umewadanganya watazania? Kama ndivyo, uombe radhi basi! Au ufafanue!