Wazungu ni watu wema sana kuliko viongozi wa kiafrika!Wanatusaidia pmj na MiPhd yetu kutoka jalalani kwamba mtoto aliyechini ya miaka 18 hana uhuru wa kutosha katika kufanya maamuzi ni peer thinking hivyo anahitaji kusaidiwa akipata ujauzito lakini pia sio wote wanapata ujauzito kutokana na viherehere vyao lahasha wengine wanabakwa au kushawishiwa kutokana na mazingira duni ya kiuchumi,wengi wamepata ujauzito kwa kupewa msosi tu,hvyo tuwapinge akina Mwigulu na wengine wenye mawazo finyu kuhusu haki ya mtoto wa kike kupata elimu.Ebu tutumie common sense tu hvi mzungu ananufaika ninini katika hili?je mabinti hawa ni makenikia mpaka tuambiwe tunaowasupport sio wazalendo (unpatriotic) kama asemavyo Mwigulu na Phd yake?Sijui miafrika tukoje ndio inferiority complex.
Well actually personal I am not a supporter wa kumnyima mtu yeyote haki ya kupata elimu.
Dunia ya leo msemo wa kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha sio theory tena bali ni fact. Wameenda mbele zaidi elimu ni afya pia, kwa sababu inamsaidia mwanadamu kuweza kuchukua hatua za kujikinga kwa kuelewa wa madhara.
Nakubaliana na mtazamo wako wa ‘poor’ thinking kwa watoto ni sababu ya msingi; mabeberu jambo hilo wameliweka kama vulnerability.
Ya kwamba ni rahisi sana kumlaghai mwanafunzi kwa zege kuliko mtu mzima na ni rahisi sana mtoto kubakwa na kunyamazishwa iwapo familia itaamua kufumbia macho.
Kwa ivyo central to the problem sio mtoto kwa mtazamo wao bali society; ndio maana linapokuja swala la kutembea kimapenzi na mtoto wazazi nao wanafungwa kama walijua hawaku report.
Kama ni mashuleni iwapo walimu walijua kuna mwenzao anatabia hizo si ajabu na wao wakaenda jela au kufukuzwa pamoja kama awakutoa taarifa na mwalimu mkuu nae akaenda.
Ndio maana ulaya mwalimu akijulikana tu ana mahusiano na mwanafunzi wa sekondari chances utasikia kakimbia na nchi, vinginevyo siyo tu jela, ukitoka unakuwa kwenye sex offenders list na kwa wenzetu ukienda kuomba kazi criminal record lazima utaje na zingine upeleke CRB (kama vile uhakiki wa polisi) basically umeshaharibu maisha yako yote.
Kutokana na mziki wenyewe watu wazima ata wakiona mtoto paja, mgongo na chuchu zimenona sio kwamba awatamani lakini wakifikiria jinsi maisha yao yanavyoweza haribiwa wengi hawathubutu.
Sio sisi pamoja na hukumu kali bado ni rahisi kukwepa mikono ya sheria achilia mbali kutembea na watoto bali ata wanapopewa mimba, ukizingatia na shida za zilio wengi it makes it even easier to get away with.
Sasa badala ya serikari kupambana na wanafunzi inabidi iione jamii ndio tatizo zaidi. Na kutaka kuona more accountability kutoka huko kwenye service level.
In short ni vita ambavyo wanasiasa inabidi wapigane kuona more is done in terms of detering those acts, haki inapatikana na watoto wanapewa elimu sio lazima shule za kawaida.
Lakini aina maana kuandika barua ya kuzuia serikari ikose hela kabisa hapo hao hakina Zitto wamekosea lazima uangalie picha kubwa inapokosekana hiyo hela hakina nani nao wanaoathirika na kwanini waadhibiwe kwa maamuzi yasiyo yao.