Mkya
JF-Expert Member
- Dec 15, 2013
- 667
- 94
Wana bodi mwezi Wa nane tarehe nane naibu Katibu mkuu ccm bara ambaye ameonyesha nia ya kutaka uraisi mwigulu atazichapa na Mbunge Wa nzega Dk Kigwangala ambaye naye ameonyesha nia ya kuutaka uraisi baada ya raisi Kikwete
Tukutane uwanja Wa taifa name nane tuone nani atatoka bingwa
Tukutane uwanja Wa taifa name nane tuone nani atatoka bingwa
AGOSTI 8, mwaka huu Uwanja wa Taifa patakuwa hapatoshi kwani Watanzania watashuhudia matukio makubwa ya burudani kupitia Tamasha la Usiku wa Matumaini.
Miongoni mwa matukio hayo ni ndondi za waheshimiwa wabunge ambapo mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kigwangala atakazichapa ‘kavukavu' na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba.
Akizungumza na Mikito Nusunusu, Mratibu wa tamasha hilo lenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya sekondari nchini, Luqman Maloto alitaja burudani kibao zitakazolipamba tamasha hilo ikiwemo mechi ya wabunge mashabiki wa Simba na wenzao wa Yanga, Bongo Fleva dhidi ya Bongo Movie.
"Wabunge wa Yanga sasa hivi wanatamba na usajili mpya wa Ridhiwani Kikwete wakati wenzao wa Simba wakiwa na Geodfrey Mgimwa sasa sijui mwaka huu nani ataibuka bingwa kwani mwaka jana Yanga walishinda kwa ushindi mdogo wa 1-0," alisema Maloto.
Chanzo: Global Publishers