Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo (Abdul Nondo) atema cheche muda huu

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo (Abdul Nondo) atema cheche muda huu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975

------------

"Waziri wa Vijana anapewa fedha anakuja kutuambia sisi vijana kwamba fedha hizo zimepelekwa wizara za kisekta, sisi tulitarajia Waziri Joel Nanauka baada ya kupokea ile hundi aje awaeleze vijana kwamba bilioni 200 zipo utaratibu wake ni huu, vigezo vyake ni hivi, muongozo wake wa utolewaji ni huu, udhibiti wake ni huu, vijana njooni mukope utaratibu wake ni huu hapa. Yeye akisimama anaishia kusema kwamba fedha zikwenda Wizara za Kisekta."- Amesema Abudl Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT-Wazalendo


 
Huyu dogo ana akili nzuri mno ila chama alichokikumbatia hakimpeleki popote .

Zaidi namuona akija kuharibika kama rafiki yake wa enzi hizo bwana Emijidius Cornel walipokuwa kwenye harakati keko ya magurumbasi juu ya habari za walimu wa kujitolea
 
Huyu dogo ana akili nzuri mno ila chama alichokikumbatia hakimpeleki popote .

Zaidi namuona akija kuharibika kama rafiki yake wa enzi hizo bwana Emijidius Cornel walipokuwa kwenye harakati keko ya magurumbasi juu ya habari za walimu wa kujitolea
Kuna wakati fulani act walikua wanatembea mikoani huko wanaorodhesha changamoto na kutoa mapendekezo , lilikua jambo la maana sana
 
Kuna wakati fulani act walikua wanatembea mikoani huko wanaorodhesha changamoto na kutoa mapendekezo , lilikua jambo la maana sana
Ni jambo la maana lakini bado tunao muda mrefu sana wa kusubiria ACT kuwa chama cha upinzani sababu ni nyingi zinazokinyima credibility hiko chama .

Huyo dogo ni pure activist ila njia anayopita ina makando kando mengi na pia alikosea kutanguliza uhome boy kwenye harakati maana Godfather wake haeleweki yeye ni nani toka alipokimbizwa CDM .

Anyway kila jambo lipe muda ,wacha tusiyoyajua tuyape muda ipo siku tutayajua tu .

Ila ukimuona mwambie Elina bado hajaamini kama huyo dogo angemuacha kisa hiko cheo cha ngome sijui ya vijana ,bado anamkubali sana ,mueleze awe anapokea na simu zake ,kuachana sio vita sababu maisha yana vituo vingi huwezi jua kuna kituo wanaweza kutana tena kama walivyokutana UD
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Hizo pesa wanapewa uvcccm tu, kikubwa uwe na kadi ya chama!.
Pesa za serikali wanagawana maccm...sawa, tutaelewana tu huko mbele!!!.
 
Kuna wakati fulani act walikua wanatembea mikoani huko wanaorodhesha changamoto na kutoa mapendekezo , lilikua jambo la maana sana
Hiyo ilikuwa na maana kama ushindani ni wa sera. Sasa unakusanya taarifa na kuziwekea mikakati ya kuzitatua, ikifika wakati wa uchaguzi mshindi anatangazwa nje ya kura za wananchi.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Ni jambo la maana lakini bado tunao muda mrefu sana wa kusubiria ACT kuwa chama cha upinzani sababu ni nyingi zinazokinyima credibility hiko chama .

Huyo dogo ni pure activist ila njia anayopita ina makando kando mengi na pia alikosea kutanguliza uhome boy kwenye harakati maana Godfather wake haeleweki yeye ni nani toka alipokimbizwa CDM .

Anyway kila jambo lipe muda ,wacha tusiyoyajua tuyape muda ipo siku tutayajua tu .

Ila ukimuona mwambie Elina bado hajaamini kama huyo dogo angemuacha kisa hiko cheo cha ngome sijui ya vijana ,bado anamkubali sana ,mueleze awe anapokea na simu zake ,kuachana sio vita sababu maisha yana vituo vingi huwezi jua kuna kituo wanaweza kutana tena kama walivyokutana UD
Naam mkuu, sema hapo kwa Elina tumtakie kila la kheri ampate nondo,

Mimi siwafahamu kama unavowafahamu wewe, ila unaweza mshauri "Elina" akavizia vikao vya act, au press kama hili la leo
 
Hiyo ilikuwa na maana kama ushindani ni wa sera. Sasa unakusanya taarifa na kuziwekea mikakati ya kuzitatua, ikifika wakati wa uchaguzi mshindi anatangazwa nje ya kura za wananchi.
Naam na changamoto kuu kabisa ya ccm, kutika hawataki na kuchapa kazi hawawezi
 
Naam na changamoto kuu kabisa ya ccm, kutika hawataki na kuchapa kazi hawawezi
Kwasasa hivi ccm hawafanyi siasa bali wanapora madaraka baada ya kufikia mwisho. Siku za nyuma kulikuwa na midahalo, lakini kwa sasa hakuna, ama ipo kwa uchache. Na iliyopo ni ya kusufia serekali, ama inayochujwa sana.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Kwasasa hivi ccm hawafanyi siasa bali wanapora madaraka baada ya kufikia mwisho. Siku za nyuma kulikuwa na midahalo, lakini kwa sasa hakuna, ama ipo kwa uchache. Na iliyopo ni ya kusufia serekali, ama inayochujwa sana.

Ndani ya hii miaka mitano tunachomoka vipi hata katika kutatua matatizo madogomadogo yanayoweza kutolewa amri tu?
 
Haijalishi una mawazo mazuri kiasi gani, kwa sasa hatuitaji utaalama na matamko
 
Back
Top Bottom