ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 610
- 1,540
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad kesho Oktoba 20, 2020 atazungumza na vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.
Wapi: Ukumbi wa Ramada Hotel, jirani na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Posta Mpya, Dar es Salaam.
Muda: Mkutano huo utafanyika saa 4:00 asubuhi
Baada ya mkutano huo, Maalim Seif ambaye pia ni mgombea Urais wa ACT-Wazalendo Zanzibar atahutubia mkutano wa hadhara Jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Barafu Mburahati, Ubungo.
Aidha Maalim Seif atatumia mkutano huo kuwanadi wagombea ubunge na udiwani wote wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam.
Waandishi wa habari kama wadau muhimu mnakaribishwa katika matukio hayo.
Imetolewa na:
Janeth Joel Rithe
Naibu/Katibu wa Uenezi, Habari na Mahusiano ya Umma
Leo Oktoba 19/10/2020