PreGE2025 Mwenyekiti UVCCM Iringa Vijijini awataka vijana bodaboda kuwatetea viongozi wa serikali wanaposemwa vibaya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Iringa Vijijini, Elia Juma Kidavile, ametoa wito kwa vijana wa kuwanenea viongozi wao mazuri kutokana na juhudi kubwa wanazozifanya katika kuleta maendeleo kwa wananchi. akiongeza kuwa viongozi hao wamekuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa miradi mbalimbali , ikiwemo katika sekta za elimu, afya, na jamii, ambayo imesaidia kuboresha maisha ya wananchi.

Kidavile ameyasema hayo leo tarehe Aprili 3 , 2025 alipokuwa akizindua shina la bodaboda la UVCCM kata ya Mboliboli, tarafa ya Pawaga, Wilaya ya Iringa. Uzinduzi huo ni sehemu ya ziara ya kamati ya utekelezaji ya UVCCM Wilaya ya Iringa Vijijini.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


Your browser is not able to display this video.
 
Hapo ndo akili za CCM zilipoishia. Alafu tutegemee nchi hii kupata maendeleo ya kweli?

CCM wanailifubaza sana hili Taifa kila kukicha. Creativity yao ndo imeishia hapo kuwafanya vijana kuwa bodaboda.

Pathetic Nation.
 
Hii ni kufundisha watu kukataa uhalisia ili kuwa chawa
 
Ingekua busara huyu mwenyekiti angetafuta sababu za viongozi kusemwa vibaya na kuwaonya viongozi hao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…