Mwenyekiti NEC ni Shemeji wa Lowassa - Janga kubwa sana

Mie nadhani hoja siyo aliyeteuliwa anatoka kabila gani, shemeji, mkwe, mume, kaka, mjomba au ndugu wa nani. Hoja ni je, pamoja na sifa anao uwezo kifikra, kimaadili na nguvu kimwili wa kutekeleza majukumu yake katika kipindi hiki cha www.com.

Huu ndio mjadala tunaotakiwa kuwa nao. Mwanzoni mwa mwaka huu niliwahi kuandika makala katika gazeti moja magazeti ya kila siku ya Kiswahili nchini nikielezea baadhi ya matatizo yanayolikabili Taifa letu changa (tumeadhimisha miaka 50 juzi, kwa Tanganyika), kuwa ni nafasi nyingi za uteuzi kutawaliwa na siasa yetu kushikiliwa na wastaafu ambao huchukulia vyeo na nyadhifa wanazokabidhiwa kama sehemu ya kujipumzisha baada ya kazi ngumu serikalini au kwenye ashirika na taasisi za umma.


Viongozi na wanasiasa wastaafu hawajishughulishi kuchangamsha bongo zao wala hawana rekodi (Legacy) wanayolenga kuacha nyuma yao katika majukumu mapya wanayokabidhiwa baada ya kustaafu. Hawa mara nyingi hawataki matatizo na watu wala hawapendi mijadala mikali yenye changamoto. HIVI KAMA JAJI MAKAME KACHOKA, JE, LUBUVA NDIYE MBADALA YAKE MWENYE NGUVU YA KUHIMILI CHANGAMOTO ZILIZO MBELE YA NEC ? Tujadili....
 
Mie nadhani hoja hapa siyo mteule huyo kuwa shemeji, kaka, mjomba, binamu, baba wala ndugu wa nani. Hoja ni kwamba licha ya sifa zote alizonazo zinazomwezesha kushikilia nafasi hiyo, Je, anao uwezi kifirka, kimaadili na nguvu ya kimwili kuhimili mikiki na changamoto za kizazi hiki cha www.com?

Mwanzoni mwa mwaka huu niliwah kuandika makala katika moja ya magazeti ya Kiswahili yanayochapishwa kila siku nchini kuwa moja ya matatizo sugu yanayoangamiza Taifa letu changa (Limeadhimisha miaka 50, kwa Tanganyika), ni kitendo cha nafasi nyingi za uteuzi na siasa kushikiliwa na wastaafu ambao kihulka huchukulia nafasi hizo kama sehemu za kujipumzisha baada ya kulitumikia Taifa kwa miaka mingi.

Sifa moja ya mstaafu ni kuhitaji utulivu wa kumwezesha kupumzika. Hawa hawataki mijadala na changamoto za kufikirisha wala kuchangamsha bongo. Wamechoka. Hawahitaji hata kuacha Legacy yoyote nyuma yao katika hizo nafasi zao mpya za kujipumzisha.

Swali la msingi la kujiuliza ni kwamba iwapo Jaji Makame amechoka na anastaafu ili akapumzike. Je, Jaji Lubuva ndiye chaguo mbadala mwenye nguvu, uwezo na fikra mpya za kuhimili changamoto zilizo mbele ya NEC yetu tuliyoshuhudia wataalamu wake wakihindwa hata kutumia teknolojia mpya ya habari na mawasiliano katika kukusanya na kutangaza matokeo katika uchaguzi mkuu uliopita? tujadili....
 
Naomba nimpe uraisi huyo Lowasa wenu lakini kwanza niambieni kiwango cha elimu yake na kiwango cha uafahamu wake.

Munateteeeeaaaa! wakati jamaa anaonekana ni kilaza.

Hebu tena nikumbusheni habari za lile gazeti la miaka mitatu iliyopita, Ni Waziri Mkuu mstaafu yupi aliye na tabia ya USHOGA???? Safari hii hatutaki sifa za kucheka-cheka.
 
Tatizo letu wana JF tunaweka siasa ktk kila jambo

kwa upande wangu kama vigezo vilizingatiwa haina shida,maana kama ni undugu basi kila chama hapa Tz kimejaza ndugu hakuna CCM wala CDM vyama vyoooooooote vimefanya uteuzi kwa kuangalia nani mtoto wa nani,

ndio mambo yetu tz yalivyo

acheni tusonge mbele,no way out juu ya undugu

Nani aseme hapa kuwa CDM hakuna ndugu aliyeteuliwa kwa nafasi yeyote ile nani? ama CCM pia tumeona chaguzi za UVCCM na CDM Mambo ya undugu yamejaaaaaaaaaaaaaaaaaa,

ndio maisha tuliyojichagulia jamani

yale si masuala ya kichama jamani! Ni ya kitaifa.. Chama kitaleta matatizo,watakufa watu 10 sanasana.Lakini suala la kusimamia uchaguzi mkuu,roho za maelfu zaweza kupotea!
 
Pasco,

Tunakuamaini sana kwa michango yako. Lakini kama ni kweli Huyu Lubuva ni shemeji yake na Lowasa amabaye kila mtu anajua malengo yake na ndoto zake za urais, inatia mashaka kidogo. Kuna majaji wengi ambao angeweza kuwachagua bila kuwa na question mark kwenye uteuzi wake. Hivi hujawahi kufirkiria kwa nini teuzi nyingi za JK huwa zinakuwa scrutinised kuliko za enzi za BWM??

By the way, hii post ya mwenyekiti wa NEC ni lazima ishikwe na Jaji mstaafu tu??
Mr. Zero, asante kuniaminia, nitawaomba tuungane kwa ninacho kiamini kwa urais wa 2015.
Nilimuuliza mtoa mada, jee kama jaji Lubuva anazo sifa zote na vigezo, jee anyimwe uteuzi kwa sababu tuu mke wa Lowassa katoka alikotoka Jaji Lubuva?.

Swali la kwanini jaji? ni kwa kwa mujibu wa ibara ya 74 ya katiba ya JMT
74.-(1) Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya
Muungano ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao watakaoteuliwa
na Rais:-
(a) Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya
Rufani, ambaye atakuwa mwenyekiti;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa mtu
anayeshika, aliyewahi kushika au anayestahili
kuteuliwa kushika madaraka ya Jaji wa Mahakama
Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani;
 
Tz iko kazi kweli. Hata mwenyekiti wa TU naye ameteuliwa kimkakati. Nani atakayepona kwa mafisadi maana wana mbinu nyingi kama mashetani weusi. Nadhani wakati ufike sasa Wtz tuseme ''no more these canning people to rule over us!!''
 
Ndugu yangu Pasco, issue hapa sio kuteuliwa kwa ndugu Lubuva kuwa mwenyekiti wa NEC ila ni je, hekima imetumika katika uteuzi huu? Hivi katika mazingira haya na hali kama hii ya ufisadi hapa nchini, unaweza ukamwambia nani mwenye akili timamu juu ya hekima iliyotumika katika uteuzi huu akakubaliana na wewe kirahisi ukizingatia kuwa mgombea mtarajiwa ambaye pia anahusishwa na kashfa kibao za ufisadi ana ukaribu na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi (aliyeteuliwa). Hivi kweli, nyani anaweza kuamulia kwa haki kesi ya ngedere? Hebu tuweni serious kidogo basi linapokuja suala kutetea maslahi ya nchi jaman sio kila kitu mpaka tulumbane
Ndugu yangu kholo, ili hekima katika uteuzi itumike, kwanza si ni lazima hiyo hekima yenyewe iwepo?!. Wewe kama ni mfuatiliaji wa mambo, lazima utakuwa unakijua kiwango cha hekima ya mteuzi!
 
tatizo sura zile zile pasco, yaani tanzania hakuna vichwa vingine?????? hasira ahgaaa!!!! mara mia ningesikia mkuu pasco, au mwanakijiji or fair player au waberoyo or kimbunga kaa!! changes we need more!!
Ndugu yangu masabuda, ni kweli, sura zile zile na watu wale wale daima dumu!, ili kupata mabadiliko, lazima tuwaelimishe Watanzania, wayakubali mabadiliko kwa kuzitisha ajira za watu wale wale watakao tuletea sura zile zile, sasa tuamke, tuwaajiri watu wengine wapya ambao ndio watatuleta sura mpya!.
 
Baada ya uozo wa mwenyekiti aliyepita kushindwa hata kujumlisha namba na kusoma kwa kusita sita, Naomba katiba mpya ilitambue tatizo la tume yetu ni hesabu.

Baada ya hapo tunataka Mwenyekiti aliyesoma hesabu vizuri.
 
Mr. Zero, asante kuniaminia, nitawaomba tuungane kwa ninacho kiamini kwa urais wa 2015.
Nilimuuliza mtoa mada, jee kama jaji Lubuva anazo sifa zote na vigezo, jee anyimwe uteuzi kwa sababu tuu mke wa Lowassa katoka alikotoka Jaji Lubuva?.

Swali la kwanini jaji? ni kwa kwa mujibu wa ibara ya 74 ya katiba ya JMT
74.-(1) Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya
Muungano ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao watakaoteuliwa
na Rais:-
(a) Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya
Rufani, ambaye atakuwa mwenyekiti;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa mtu
anayeshika, aliyewahi kushika au anayestahili
kuteuliwa kushika madaraka ya Jaji wa Mahakama
Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani;
Pasco,tukubaliane kama ni kweli huyu ni Shemeji wa Lowasa lipo tatizo tena zito sana! Hali ya nchi kwasasa tulipofikia si ya kuaminia kabisa,hata mkuu wa nchi alishawahi kukiri hilo na ndio maana hata yeye alitumia familia yake kusimamia kampeni! Anajua hatuaminiani tena kuliko wakati wowote ktk nchi hii na mbaya zaidi anajua nchi inavyowaka moto kwa sababu ya jina la lowasa! Alafu unamteua shemeji yake NEC! Tuna spin nini hapa? Ni bora tupinge si kweli lakini ukishasema hata kama ni kweli eti kwa kuwa anayosifa tutakuelewa kweli? Mnapokuwa na upande jamani jitahidini kucheza kisanyansi japo kidogo bora hata kukaa kimya kulinda Status yako! Tuna akili timamu! shemeji ya Lowasa! Alafu mnachukulia mzaha! Tuache kusimamia tu hoja hata penye ukweli! Kama habari hii ni kweli THIS IS TOTALLY COMPLETELY WRONG!!!!!!
 
Pasco... Hujaona watu wanavyoifagilia Kenya? Au mpaka damu imwagike ndiyo suluhisho la mustakabali wa nchi za Afrika Mashariki? Sijamfuatilia, ila EC ya Kenya inaongozwa vizuri sana. Kwa hiyo hata kama ana sifa kama wengine,ila yule ana ''added advantage.....''
 
Aisee mimi naanza kukerwa na thread za Lowasa. Siku haipiti mpaka atajwe. Ikulu yetu yeyote atakayekaa haitakuwa na mabadiliko as long as ni wa magamba. hata akipewa Bw. Filikunjombe ataweza kuongoza tu. Ilani ya CCM ndo inaiongoza ikulu.
Nadhani wananchi tuwaze jinsi ya kuitoa CCM pale magogoni na tukishindwa basi tukatafute mkate wetu wa kila siku kama machinga.
 
Pasco,tukubaliane kama ni kweli huyu ni Shemeji wa Lowasa lipo tatizo tena zito sana! Hali ya nchi kwasasa tulipofikia si ya kuaminia kabisa,hata mkuu wa nchi alishawahi kukiri hilo na ndio maana hata yeye alitumia familia yake kusimamia kampeni! Anajua hatuaminiani tena kuliko wakati wowote ktk nchi hii na mbaya zaidi anajua nchi inavyowaka moto kwa sababu ya jina la lowasa! Alafu unamteua shemeji yake NEC! Tuna spin nini hapa? Ni bora tupinge si kweli lakini ukishasema hata kama ni kweli eti kwa kuwa anayosifa tutakuelewa kweli? Mnapokuwa na upande jamani jitahidini kucheza kisanyansi japo kidogo bora hata kukaa kimya kulinda Status yako! Tuna akili timamu! shemeji ya Lowasa! Alafu mnachukulia mzaha! Tuache kusimamia tu hoja hata penye ukweli! Kama habari hii ni kweli THIS IS TOTALLY COMPLETELY WRONG!!!!!!

Mshauri Pasco akasome novel ya The Godfather. Ataelewa watu wanafanikiwa namna gani kwa kuimarisha territory zao.. Unahakikisha mabosi wa judicial wako kwenye payroll,wakuu wa idara za usalama,wakuu wa vyuo muhimu,mawaziri,n.k. Huo ni mfano tu.. Akisoma atanielewa.
 
kuna kitu hakiko sawa wakuu,wanahabari,wanasiasa,wanaharakati hawakujua hili? Kama ni kweli habari hii na hao juu wanafahamu nitabakia kuwa sawa na shabiki anayefuatilia matokeo ya mechi tu Unauliza ngapi ngapi kwisha!
 
Huu uteuzi hauna tija yoyote kwa Mh Lowaassa zaidi ya kuendelea kumuongezea maadui wa kisiasa.

Kwa katiba ya sasa hivi mtu yoyote atakayepishwa na CCM ndio atakuwa rais na katiba ikibadilishwa na kuweka usawa kwa wagombea wa vyama vyote possibility ya huyu jaji kuendelea kuwa mwenyekiti ni NONE. Kama JK anataka kusaidia Lowassa kama watu wanavyo amini hapa,angemwachia uenyekiti wa CCM ambapo ndio ngoma nzito ilipo ili kumaliza hii vita ya urais inayoendelea sasa hivi.

Uteuzi wa ndugu na mke wa Lowassa,utaondoa dhana ya kwamba Lowassa anaonewa na kuendelea kujenga picha Lowassa bado ana nguvu na anautaka urais bila ridhaa ya wengi na italeta mwamko kwa kina Sitta na wenzake ku fight kama Taliban.
 
Kama haya yana ukweli.Jaji amechua hatua gani au ndo "kulalamika syndrome" rais hadi mwananchi wa kawaida wanalalamika.
kwa maoni yangu nchi hii imekosa viongozi shupavu.MUNGU tusaidie.
 
NEC hii itaondolewa na KATIBA MPYA tarehe 26. 04. 2014. Msihofu.

Katiba mpya imeshatekwa na CCM tayari na msiwe na mategemeo ya maana kabisa toka hiyo katiba mpya.
Katiba mpya itabaki kulinda mafisadi ya magamba.
 
Back
Top Bottom