Mwenye uzoefu na hili naomba msaada

Mwenye uzoefu na hili naomba msaada

Hawawezi kuandika kila kitu vingine unajiongeza mwenyewe,waandike wazi inashusha hamu ya ngono watamuuzia nani na wanajua hakuna mwanaume asiyependa kuipoteza hiyo hali na wanaume ndiyo wanaopata vipara?
Sahihii nimekuelewa
 
Bro acha kutumia hiyo dawa. Iko sawa na finasteride. Itakufanya upoteze nguvu zako kabisa!!

Suluhisho la nywele kurudi nyuma ina neno la kisayansi.

Inaitwa Energetic Alopecia.

Kwa lugha rahisi. Ukitaka nywele zako zirudi kama zamani fanya haya:

1. Hakikisha unapunguza muda unaotumia kwenye simu mida ya usiku. Mwanga wa blue wa simu ndio changamoto nzima inaanza hapo.

2. Hakikisha kila siku unalala saa 4 kamili usiku. Nywele huwa zinaota kuanzia 10pm - 2am. Ukikosa hii window sahau nywele kurudi.

3. Hakikisha unaacha kula vyakula vya wanga. Mfano wali. Ugali. Chapati. Maandazi. Chakula chako kiwe NYAMA. SAMAKI. na MATUNDA.

4. Hakikisha JUA La asubuhi (dk 30) Jua la mchana (dk45) na Jua la jioni (30mins) linagonga macho na kichwa KILA SIKU.

5. Usivae KOFIA ya aina yeyote

6. Ondoa simu zote. Na vifaa vya Elekroniki chumbani kwako wakati unaenda kulala usiku

7. Tumia filter NYEKUNDU kwenye simu. Google jinsi ya kubadilisha kioo cha simu kuwa na filter nyekundu.

8. Ukienda kulala usiku hakikisha TAA zote za nyumba umezima. GIZA liwe nene tii.

9. Usivae KOFIA mida ya mchana

10. Ingia Twitter/X alafu search Bowtiedbiohacker. Ingia kwenye ukurasa wake andika Energetic alopceia. Fuata anachosema.

  • Suluhisho ni kuhakikisha JUA linagonga kichwa Asubuhi, Mchana, Na Jioni.
  • Badilisha mfumo wa chakula unaokula kila siku
  • Hakikisha unazima taa zote nyumbani mida ya usiku
  • Ondoa vifaa vyote vya elektroniki unapoenda kulala usiku
  • Sahau kabisa kutumia simu au laptop baada ya saa 4 usiku

Ukitekeleza YOTE yalioandikwa hapo juu.

Nywele zitarudi ndani ya miezi 6.

Goodluck!!
 
1. Upara ni kitu kizuri kwa mwanaume. Upara na ndevu/sharubu tumeumbiwa wanaume. Mwanaume yeyote anayechukia hivo vitu 2 ni mpumbavu sana!

2. Sababu kuu ya wanaume kupata upara huwa ni kwa sababu ya hormone ya TESTOSTERONE ambayo ni MALE HORMONE. Ndiyo maana wanawake hawapatagi upara kwa sababu hawana hii hormone. Hivyo ukitumia dawa ya kuzuia upara maana yake unaenda kushusha kiwango cha hii hormone ambayo ndiyo huwa inawapa wanaume sexual drive yao.
Eti ee kumbe wanawake hawapatagi upara mbona kama kuna Prof wakike anaupara lakini anaufunika na wigi halafu nimewaona kama watatu hv wakike wanaupara..hv nayo inakuwaje hapo mtaalamu.
 
Eti ee kumbe wanawake hawapatagi upara mbona kama kuna Prof wakike anaupara lakini anaufunika na wigi halafu nimewaona kama watatu hv wakike wanaupara..hv nayo inakuwaje hapo mtaalamu.
Ukiona hivyo jua wana some amount ya testosterone.

Pia wanawake hata kama atapata upara basi ni ule wa nywele kupungua tu au zinakuwa nyepesi.

Hawapatagi upara wa kung'aa kama lami wanaopataga wanaume.
 
Wakuu nilianza kupata changamoto ya hairline kurudi nyuma japo umri wangu ni miaka 28 nilijaribu kutumia mafuta mbalimbali but sikupata matokeo. Ni kwamba nywele zangu za mbele zimeanza kuondoka.

Baada ya kufeli nikaamua kutumia Minoxidil kirkland nakimbilia mwezi sasa but changamoto nayikutana nayo ni kwamba hisia zangu wakati wa tendo la ndoa zimekuwa chini sana kitu ambacho sikuwa nimekutana nacho before but sikuwa nmejudge sana nikajua ni mambo ya hisia tu.

Ila sasa leo katika pitaita zangu huko facebook kuna mtu alikuwa anatangaza bidhaa za minoxidil bac kuna mtu akacoment kwamba zilifanya akapoteza kabisa hisia wakati wa tendo la ndoa. Hapo ndipo namimi nikaanza kuunganisha na hali yangu nikaona maybe kuna ukweli.

Ndio sasa nikaamua kuleta hii mada huku nijue kama kuna mtu alishatumia Minoxidil akakutana na hiyo changamoto ya kupoteza hisia na kipi alikifanya ili kumuweka sawaa??

View attachment 3562811
Nywele kuanza potea ( hair loss) ni ishara mkuu una upungufu wa protein aina ya keratin inayounda nywele na kucha. Tuwasiliane kwa 0713 039 875 kwa dozi
 
Back
Top Bottom