Mwenye shida ni mimi au wakwe zangu?

Mwenye shida ni mimi au wakwe zangu?

Attache

Senior Member
Joined
Jul 6, 2012
Posts
175
Reaction score
149
Nimeoa mwanamke wa Tukuyu na hivi sasa tunaishi Tanga ambapo ndio ninafanya kazi na wazazi wa upande wangu wana-reside Tanga pia. Tatizo ni kwamba wakwe wanapenda sana mke wangu awe anarudirudi nyumbani kwao.

Mwaka jana kikazi nilikua Moshi na kipindi cha christmas walikua wanakomalia sana twende au mke wangu aende kusherehekea kule japo kuwa kipindi hicho mke wangu alikua mjamzito wa miezi nane. Ilikua kazi ngumu kuwaelewesha lakini mwishoni wakakubali kishingo upande. Kuna kipindi flania wakakomalia sana twende kwenye ubatizo wa mtoto wa ndugu yao ambapo ikanilazimu niombe ruhusa ya kwenda huko na tukakaa kwa wiki moja.

Sasa mwaka huu mwezi wa tano shirika ninalofanyia kazi liliopen branch Tanga na nikapata uhamisho kuja Tanga na kwa vile tupo karibu sana na wazazi wa upande wangu nikaona ni vyema x mas hii tukasherehekea huku kwa maana haitakua picha nzuri kama tupo huku halafu kwenye sherehe hizi tukachoropoka may be kwa mwakani ndio itaeleweka. Sasa upande wa wakwe kwa juma zima wamekua wakimpigia simu kwamba tuende au yeye aende na yeye ameanza kukubaliana nao. Binafsi sipendelei sana kufanyiwa maamuzi na mtu mwingine na worse still tumeshafanya plan juu ya namna tutakavyo sherehekea huku(Tanga) lakini upande wa pili wale ni wazazi,kukataa kataa pia haileti picha nzuri. Ninawaza niache tu aende japo kuwa wazazi wa huku sidhani kama watafurahia sana kwani ni sherehe yao ya kwanza pia wakiwa na grandson wao na pia tulishaelewana kwamba this holiday tutakua Tanga.

Jambo ambalo sielewi ni kwamba je tatizo lipo kwangu kwamba ninamng'ang'ania sana mke wangu au wao? Ninaomba mchango wenu.
 
kwani wazazi wako wana matatizo?
Kama hawana, Fanya yale wakwe zako wanataka!
Ila kama ni tofauti ya hapo, waambie huendi wewe wala mke,ila wape na sababu zako,
Lazima baba mwenye nyumba awe na maamuzi ya mwisho banah!
 
Aaah, mie ni mwanamke na wala sikubaliani na hili. Wewe ndo kichwa cha nyumba, na haujaolewa tukuyu bali umeoa. Na uzingatie sio tabia nzuri sana kwa mwanaume kuwa karibu na wakwe zako (actually Paw hawezi kulala kwetu, hata kama ni msiba anaapaswa akalazwe kwa jirani pamoja na mie). Na ni kwa nia nzuri, baba mkwe na mama mkwe wakianza kuzozana ama baba akiamua kumpiga mkeo vibao kwa vile ni mwanae utafanyaje?

Ushauri wangu, muambie mkeo aongee na wazazi. Yeye ana mji wake sasa, mamake nae angekuwa anaendaga kwa baba yake kila xmas inngekuwaje? Pangeni mipango yenu na muitelekeze, kama baba mkwe hana watoto wa kiume mjipange mkiweza pasaka mkawe nao ili wamfaidi mjukuu pia. Kwenda kwenye ubatizo haikuwa mbaya, ni nafasi ya wewe kujuana na ndugu zake pia. Lakini haiwezekani kila xmas ukakae ukweni kaka.
 
Tatizo unalo wewe! Inaelekea huna msimamo kutokea mwanzo halafu unasema hupendi mtu akuamulie mambo? Waambie unakula sikukuu na mkeo PERIOD kama wana busara wataelewa kuwa wamevuka mipaka na watajirekebisha
 
Tatizo lipo huko ukweni kwako lakini kosa ni la kwako vile ulivyowazoesha ndio wameshazowea. Inakuwaje eti xmas mkeo akale kwao wakati anaacha nyumba yake na mumewe? Funguka wewe mwanaume na hata huyo mkeo mtizame kwa jicho la tatu. Mwanamke anatakiwa awe na mumewe na hakuna vya kuamrishwa. Mbona wao wakwe hawaji kwenu kula ckukuu.
 
Kama haiwezekani mjulishe mkeo awaambie na msimamo uwe ndio huo uone nini kitatokea.
 
King'asti umesema niliyotaka kusema.

mkaka mzuri just be a man na makeo anapaswa kufwata sheria zako milele na sio wewe kufwata za kwao. tena tumia tone yenye mamlaka unapo-address hili kwa mkeo.
naomba naiakauekee maneno mdomoni mwambie hivi
"" nimesema kwamba wewe hutasafiri kwenda tukuyu wala mm sitokwenda tukuyu kusherehekea sikukuu""

usiseme zaid ya hayo sasa kama binti atapanda basi kwenda utajua na kama atanuna utajua ni mke wa aina gani. binafsi nampenda mwanaume ambaye akisema jambo ndani ya nyumba lazima kauli yake iwe ndo ya mwisho na hakuna atakaye sema zaidi ya hapo. hata baba yangu na mama yangu waheshimu kauli za mume wangu kwamba aliyesema ni mumewe and that's it.
 
Last edited by a moderator:
Mkeo huyo ndio anachochea ili muende kwako, kwanza mkomeshe huyo mkeo aache tabia ya kuwashinikiza wazazi wake kuwaiteni mwende tukuyu...unadhani kama mkeo(mtoto wao wakwe zako) akisema hawezi kwenda kuna hili na hili, unadhani wakwe watang'ang'ania? Deal kwanza na mama watoto aache kuwashinikiza wazazi wake.
 
Nimeoa mwanamke wa Tukuyu na hivi sasa tunaishi Tanga ambapo ndio ninafanya kazi na wazazi wa upande wangu wana-reside Tanga pia. Tatizo ni kwamba wakwe wanapenda sana mke wangu awe anarudirudi nyumbani kwao.

Mwaka jana kikazi nilikua Moshi na kipindi cha christmas walikua wanakomalia sana twende au mke wangu aende kusherehekea kule japo kuwa kipindi hicho mke wangu alikua mjamzito wa miezi nane. Ilikua kazi ngumu kuwaelewesha lakini mwishoni wakakubali kishingo upande. Kuna kipindi flania wakakomalia sana twende kwenye ubatizo wa mtoto wa ndugu yao ambapo ikanilazimu niombe ruhusa ya kwenda huko na tukakaa kwa wiki moja.

Sasa mwaka huu mwezi wa tano shirika ninalofanyia kazi liliopen branch Tanga na nikapata uhamisho kuja Tanga na kwa vile tupo karibu sana na wazazi wa upande wangu nikaona ni vyema x mas hii tukasherehekea huku kwa maana haitakua picha nzuri kama tupo huku halafu kwenye sherehe hizi tukachoropoka may be kwa mwakani ndio itaeleweka. Sasa upande wa wakwe kwa juma zima wamekua wakimpigia simu kwamba tuende au yeye aende na yeye ameanza kukubaliana nao. Binafsi sipendelei sana kufanyiwa maamuzi na mtu mwingine na worse still tumeshafanya plan juu ya namna tutakavyo sherehekea huku(Tanga) lakini upande wa pili wale ni wazazi,kukataa kataa pia haileti picha nzuri. Ninawaza niache tu aende japo kuwa wazazi wa huku sidhani kama watafurahia sana kwani ni sherehe yao ya kwanza pia wakiwa na grandson wao na pia tulishaelewana kwamba this holiday tutakua Tanga.

Jambo ambalo sielewi ni kwamba je tatizo lipo kwangu kwamba ninamng'ang'ania sana mke wangu au wao? Ninaomba mchango wenu.

....weka msimamo wako mezani mbele ya familia yao kitaeleweka (nani kaoa na nani kaolewa)
 
inawezekana wazazi wa mke hawajazoea kuwa mtoto sasa hayupo mikononi mwao.

Cha kufanya ni kuamua kama mwanaume, waeleze hamwezi kwenda kuna mipango mlishapanga, nyie mtafute wakati mwingine kama fedha itakuwepo muende

sababu ya pili kwa nini wazazi wa mke wanafanya hivyo naihifadhi maana nitashambuliwa na kuitwa mkabila loh
 
Siku ya mwisho ya huyo mkeo kuwa chini ya milki ya wazazi wake ni siku ile ya Send Off...baada ya hapo ulikabidhiwa mkeo, maana yake ni kuwa maamuzi yoye juu yake unayo wewe sasa.
Kama wamemiss si waangalie picha zake, khaaa! Tena kuanzia sasa unaposoma comment hii, uanze kujisimamia kama mwanaume na Baba mwenye nyumba.
 
Aaah, mie ni mwanamke na wala sikubaliani na hili. Wewe ndo kichwa cha nyumba, na haujaolewa tukuyu bali umeoa. Na uzingatie sio tabia nzuri sana kwa mwanaume kuwa karibu na wakwe zako (actually Paw hawezi kulala kwetu, hata kama ni msiba anaapaswa akalazwe kwa jirani pamoja na mie). Na ni kwa nia nzuri, baba mkwe na mama mkwe wakianza kuzozana ama baba akiamua kumpiga mkeo vibao kwa vile ni mwanae utafanyaje?

Ushauri wangu, muambie mkeo aongee na wazazi. Yeye ana mji wake sasa, mamake nae angekuwa anaendaga kwa baba yake kila xmas inngekuwaje? Pangeni mipango yenu na muitelekeze, kama baba mkwe hana watoto wa kiume mjipange mkiweza pasaka mkawe nao ili wamfaidi mjukuu pia. Kwenda kwenye ubatizo haikuwa mbaya, ni nafasi ya wewe kujuana na ndugu zake pia. Lakini haiwezekani kila xmas ukakae ukweni kaka.

kha, Kwaiyo unamaana mke ni chombo cha mwanamme na anaweza kukifanyia anavotaka yeye?
Huyo mwanamke kanunuliwa bei gani? dini zote zinasema kwamba unaweza kuachana na kila mtu lakini huwezi kuachana na wazazi, kwaiyo sikubaliani na wewe umepotoshwa na umekubali kuwa mtumwa wa mwanaume. Siku mume wako hakutaki tena, je utakimbilia wapi? au siku unaumwa kila kitu hapo hapo, unajikojolea na kujinyea unafikiri wakwe zako watazoa mavi yako? au huyo mumeo atazoa amvi yako? Kumbuka baba yako tu au dada zako ndio watakusafisha wewe.

Mie naona wanampa matatizo huyo mwanamke, wanamueka njia panda, hajui wapi aende. maana wazazi wake ni muhim kwake na mume ni muhim kwake.

Kama mume anampenda mkewe basi amsaidie waende japo siku 3 wawafurahishe wazee tu na warudi.
yaonesha huyu jamaa anataka kushindana na wakwe, sio kitu kizuri
 
Nadhani kuna kosa umeshafanya - umempa uhuru sana mkeo na amejisahau.
1. Wakwe zako huwa wanapanga haya mambo na mkeo kwanza kabla wewe hujapewa taarifa. Huu ni ushenzi ambao unapaswa kukemewa kwa nguvu zote.
2. Mkeo haoni ni vibaya- bado hajahama kwao huyo at least katika mawazo na roho yake.Ukimuuliza anaona kwa wazazi wake ni kwao. Huyo anahitaji sana kuwekewa mipaka
3. Tatizo ni kubwa kuliko haya tunayoyaona. Unapaswa kufunguka na kupima uwezo wake wa kusema UKWELI na kama anakuhusisha kiasi gani katika huo ukweli.
4. Mkeo hana msimamo na anahitaji kuchagua upande atakaoupa kipaumbele
Vingenevyo una kazi!
 
wakati wanamfanyia sendoff,walifikiria nini?napenda sana wazazi wa kisukuma ukishaolewa umeolewa tena wanakuambia ukigombana na mmeo mshitaki kwa wakwezo,na akikuudhi kimbilia kwa wakwe zako.Sasa hao wa tukuyu na wenyewe wanaleta mambo ya ajabu.binti yao nae ana familia yake bado wanamcontrol tu.
 
Back
Top Bottom