Attache
Senior Member
- Jul 6, 2012
- 175
- 149
- Thread starter
- #21
Well said King'asti, asnte sana.
Aaah, mie ni mwanamke na wala sikubaliani na hili. Wewe ndo kichwa cha nyumba, na haujaolewa tukuyu bali umeoa. Na uzingatie sio tabia nzuri sana kwa mwanaume kuwa karibu na wakwe zako (actually Paw hawezi kulala kwetu, hata kama ni msiba anaapaswa akalazwe kwa jirani pamoja na mie). Na ni kwa nia nzuri, baba mkwe na mama mkwe wakianza kuzozana ama baba akiamua kumpiga mkeo vibao kwa vile ni mwanae utafanyaje?
Ushauri wangu, muambie mkeo aongee na wazazi. Yeye ana mji wake sasa, mamake nae angekuwa anaendaga kwa baba yake kila xmas inngekuwaje? Pangeni mipango yenu na muitelekeze, kama baba mkwe hana watoto wa kiume mjipange mkiweza pasaka mkawe nao ili wamfaidi mjukuu pia. Kwenda kwenye ubatizo haikuwa mbaya, ni nafasi ya wewe kujuana na ndugu zake pia. Lakini haiwezekani kila xmas ukakae ukweni kaka.