Habari wana JF, hii asubuhi Mbwiga ameshindwa ku peruzi magazeti Clouds fm, sidhani hata kama darasa la saba alimaliza, mwenye CV yake atujuze tafadhari.
Nawakilisha.
Hizo ndizo fursa! Mbwiga anatumia mdomo kama mtaji na mapene anapata! Clauds ni wazee wa fursaaaaaa! Fursa kwanza mengineyo baadae!Wanasaidiana maisha CV za nini sasa?
ni mdharamu wa mwanalumango, class seven, kada wa chama chakavu na mwanachama nguli wa yanga sport club, alikuwa mc wa vigodolo magomeni, kigogo na mwanayamala bas na sasa ni mtangazaji wa blouz fm.. Ndio cv yake hiyo.
Mbwiga si mtangazaji clauds bali ni mshehereshaji wa baadhi ya vipindi.
Kwa ufupi tu Mbwiga ni mtoto wa mjini nawewe kama ni wakuja Dar Mbwiga humuwezi.
sisi binadamu mkuu tupo kimakundi , kuna wanaompinga kwa sababu zao na wanao mkubali vile vile , mbona mr. bean ana tukuzwa uingereza kuna lipi anaelimisha jamii ,zaidi ya kucheka tu. the same to mbwiga habari anaiwekea manjonjo hata wasioenda shule wanapata picha ya kuelewa habari hizo kwa kufurahi na kwa kufuatilia kwangu hakuna mtu watu wanataka kumsikia kama mwiga na ndiyo maana wakamuweka katika kipindi cha power breakfast, mwanzo alikuwa hayupoMbwiga, Mbwiga, Mbwiga unatisha kama radi, elimu yako haijulikani lakini unafanya kazi ktk redio ya mjini. Humu JF, kuna mijitu ina masters inamlilia Kikwete aipe ajira. Na nadhani wengine wanakuomba nauli.
Clouds FM kazeni buti. Naunga mkono falsafa yenu ya kutaka matokeo sio vyeti. Mbwiga wa wa waa