Mwenge kuna nini Jamani!!

Mwenge kuna nini Jamani!!

Mwenge ni sehemu rahic kuifikia ndo maana inakua makutano junction,kwahyo na wapenzi wanakutana pale kuelekea huko ma beach..
Ila pia mwenge pabaya jaman unaweza ukatumia mpaka nauli usipokaa vzuri,maana ukigeuka huku viatu,huku nguo lazma uchanganyikiwe
 
we jifanye tu unafanya utafiti, hivi mnajua Ngoswe wa kwenye kile kitabu cha MAPENZI KITOVU CHA UZEMBE alipoteza nyaraka zake maeneo ya wapi? Wachunguzi wa mambo wanasema ilikua MWENGE,

Sasa hivi panaitwa "MWENGE KITOVU CHA UZEMBE"
 
..Mi nkajua ni ule wapinzani wanaotaka UKIMBIzwe kila Baada ya Miaka 5...ili kupunguza matumizi yasiyo ya lazima
 
yaani unafikiri tutakuamini hivi bila kutuwekea picha ya kutudhihiishia kwamba ni kweli upo Mwenge unasagula.................bandika picha haraka sana

kapicha kamegoma kuaplodika!loh!
 
mbona ni pa kawaida tu jamani? hata kariakoo watu wanajiremba na kufanya makutano, nini mwenge?
 
Kubali usikubali kama wewe ni mwenyeji wa Dar au umeshawahi kutembelea maeneo haya lazima ukubaliane na ninachotaka kukisema,.

Mwenge ni kubwa sana ila nitachukua eneo dogo tu nililolifanyia utafiti la mwenge-sokoni na mwenge-kituo cha mabasi,.

Maeneo haya yamekuwa ya muingiliano wa watu wengi sana wakijitafutia mahitaji yao au kufanya biashara zao,.

Kwa utafiti nilioufanya nimeibua yafuatayo:

1.Eneo hili limesheni wadada wengi tena warembo waliojipamba wakapambika, waliotumia vipodozi vikawapodoa,.

2.Eneo hili limekuwa sehemu ya makutano kwa wapenzi wengi ukilinganisha na Mlimani city na maeneo mengine maarufu hapa mjini,

3.Eneo hili limekuwa sehemu ya kupamba miili ya akina dada, ukitaka staili yoyote ya mapambo fahamu Mwenge ndiyo mpango mzima,


Wakina dada wa siku hizi ukiwauliza tuonane wapi bila shaka atakuambia tuonane Mwenge, mambo ya kukutana beach yameshapitwa na wakati!!

@''bado nahitaji kifahamu mwenge zaidi

Nafikiri pia guest nyingi ziko maeneo hayo....yoote hiyo including sinza huwa naiita killing zone
 
Mwenge ni sehemu rahic kuifikia ndo maana inakua makutano junction,kwahyo na wapenzi wanakutana pale kuelekea huko ma beach..
Ila pia mwenge pabaya jaman unaweza ukatumia mpaka nauli usipokaa vzuri,maana ukigeuka huku viatu,huku nguo lazma uchanganyikiwe

we acha tu! Miye hujikutaga nnamianne tu za nauli ! Pabaya palee!!
 
  1. kuna mtoto wa bosi
  2. kuna yule uliyenae mbali
  3. unatamani wa mwenge
tuachie na sisi bhana...kha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom